LIVE Yanayojiri vita ya Israel dhidi ya Palestina na HAMAS

LIVE Yanayojiri vita ya Israel dhidi ya Palestina na HAMAS

Live coverage on JamiiForums
Hii hoja huwa sielewi? Hamas haipo West Bank je kuna amani? Mbona kila siku wapalestina wanapigwa risasi na kuporwa makazi? Hii hoja kuwa Hamas ndio inaharibu amani inatoka wapi!! Nachojua siku Hamas ikifutwa basi Israel itafanya inachofanya kule Westbank kuongeza makazi ya walowezi kwa kupora ardhi ndogo iliyosalia Gaza!!

Wakiwemo hao wayahudi ambao wamemkataa kumkiri!! Na wao wasipotubu moto wa kuzimu unawahusu. Na kingine Mungu ni wa wote sio wa Israel hiyo ilikua ni specifically agano la kale, ila agano Jipya hakuna tena cha Israel ni kila mtu ana equal chance mbele ya Mungu hakuna favor wala uspecial wa taifa moja.
kuna siku utaelewa.
 
Kwamba wamekufa shahidi wanaenda kupata mabikra ila wavaa kobasi bhana
 
Ina Maana hujui Historia ya kilwa kwamba Iliuzwa kwa Prince wa Iran?

Mkuu unabishana vitu obvious hayo mambo yako ya Sovereign ni vitu vya sasa ni vitu ambavyo vimetengenezwa karibuni, kama sio Berlin Conference basi ni baada ya UN kutengenezwa.

Palestina as Palestina ipo maelfu ya miaka, hata kabla Yesu hajaja.
1. Palestina imetajwa Ancient Greek na Historians wao
2. Palestina Imetajwa Ancient Egpty na Ramesses III
Wote hao kabla ya Yesu kuja.

Kama hao wagiriki sio tu wameitaja hadi mipaka imetajwa hii Ramani ambayo imetengenezwa karne 5 kabla ya kuja Yesu
View attachment 2805646

Hii ni Tablet ya Ancient Egpty ikionesha walikua wanafanya biashara na Palestina

View attachment 2805647

Hii ni Picha Ya Mateka wa Palestina nayo pia ipo Ancient Egpty
View attachment 2805656

Ushahidi upo mwingi mno, huo wote ni kabla ya Roma hawajaja, then Wakaja Roma, Then Waisilamu, then British hadi leo.
Hakuna mahali niliposema kuwa "Palestine" haikuwepo!

Ulileta barua ya Napoleon kama ushahidi kwamba "Palestine" ilikuwepo ingawa sijawahi kupinga popote. Je, umeisoma vizuri hiyo barua? Unakubaliana na Napoleon kwamba "Palestine" ni "Land of Israel" na kutokana na tawala za kimabavu za madola yaliyokuwa yakiitawala "Palestine" zilipelekea Wayahudi kuishi uhamishoni kwa maelfu ya miaka?

Unaionaje hiyo perspective?

Palestine ambayo ilikuwepo maelfu ya miaka ni tofauti na "Palestina" hii inayozungumziwa hivi leo kama "taifa la Waarabu wa Kipalestina". Nimeshafafanua hii hoja kwenye post zilizopita. Na bahati nzuri, umekuwa ukileta ushahidi wewe mwenyewe unaounga mkono baadhi ya hoja zangu.

Kila ambacho umekuwa ukikileta hapa kama "ushahidi" kuhusu "Palestine" iliyokuwepo kabla ya 1947 hakithibitishi utaifa wa kile kinachoitwa "Palestina" hivi sasa kama "taifa la Waarabu wa Kipalestina".
 
Waarabu waliona umewapendelea zaidi Wayahudi na kuwaminya wao.

Isitoshe hata viongozi wa Israel hawakuutaka, walikuwa na agenda ya kujitanua (Zionism).

Ndio maana magaidi wa Kiyahudi (Lehi) chini ya Yithzak Shamir (waziri mkuu wa Israel miaka ya 1980 mwishoni) walimuua Folke Bernadotte - Wikipedia mpatanishi wa kwanza wa UN wa mzozo huu kupinga huo mpango.

OK! Ni kwa sababu gani Waarabu waliona mpango wa UN unawaminya wao? Mbadala wa kile walichokikataa ulikuwa upi?
 
Wana wa Israel (Yakoub) ni tofauti na nchi inayoitwa "Israel" iliyoanzishwa na Muingereza.
Pamoja na kwamba sikubaliani na wewe, I can say the same thing kuhusu "Waarabu wa Kipalestina".

Wapalestina wanaotajwa hivi sasa ni tofauti na Wapalestina waliokuwa wakiishi katika maeneo ya "Palestine" ya kihistoria. Uthibitisho upo kuhusu hili.
 
Hii inamaanisha whether Palestine wangekubali hizo partitions or not bado wangeondolewa tu. Maana licha ya Israel kutwaa maeneo 1948 or 1967 ila kila mwaka inajitanua tu.
I have a different perspective!

Israel kutwaa maeneo ni matokeo ya vita dhidi yake na mataifa ya Kiarabu baada ya mkwamo wa UN partition plan. Ni matokeo ya defensive war, ambapo kwa mtazamo mwingine, ni tofauti na kile kilichofanywa na Urusi nchini Ukraine (war of aggression).

Je, Tanzania ilifanya makosa kuivamia Uganda ili kumfurusha Idi Amin?

Tukumbuke maeneo ambayo ni Gaza na West Bank kwa sasa yalikuwa chini ya utawala wa "wavamizi" Misri na Jordan kabla ya vita ya mwaka 1967. Hayakuwa independent states.
 
Hakuna mahali niliposema kuwa "Palestine" haikuwepo!

Ulileta barua ya Napoleon kama ushahidi kwamba "Palestine" ilikuwepo ingawa sijawahi kupinga popote. Je, umeisoma vizuri hiyo barua? Unakubaliana na Napoleon kwamba "Palestine" ni "Land of Israel" na kutokana na tawala za kimabavu za madola yaliyokuwa yakiitawala "Palestine" zilipelekea Wayahudi kuishi uhamishoni kwa maelfu ya miaka?

Unaionaje hiyo perspective?

Palestine ambayo ilikuwepo maelfu ya miaka ni tofauti na "Palestina" hii inayozungumziwa hivi leo kama "taifa la Waarabu wa Kipalestina". Nimeshafafanua hii hoja kwenye post zilizopita. Na bahati nzuri, umekuwa ukileta ushahidi wewe mwenyewe unaounga mkono baadhi ya hoja zangu.

Kila ambacho umekuwa ukikileta hapa kama "ushahidi" kuhusu "Palestine" iliyokuwepo kabla ya 1947 hakithibitishi utaifa wa kile kinachoitwa "Palestina" hivi sasa kama "taifa la Waarabu wa Kipalestina".
Hoja ya Netanyahu ni kwamba wapalestina ni waarabu walivamia, na ndio hoja za hao mashetani wa west aka Zionism, ni hoja dhaifu ambayo inapingika kirahisi kwa
1. Sayansi
2. Historia
3. Dini.

1. Kisayansi wapalestina si waarabu per Se, ukipima gene zao asilimia hadi 60 zinafanana na wayahudi na watu wa kale wa kaanani, Kifupi wapalestina wana gene kali za kiyahudi kuliko hao wanaojiita wayahudi, ila Netanyahu na washenzi wenzake kila siku wanapingana na hawa wana sayansi.

2. Kidini ukisoma Conquest za kiisilamu maeneo yote Egpty, Nenda mpaka Spain Andalusia, nenda North America, Iran mpaka Mongolia huko waarabu walipeleka tu viongozi hawakujichanganya na raia husika za Hizo nchi ndio maana Egpty mpaka Leo Imepakana na Ghuba ila ukipima Dna Zao ni chini ya Asilimia 20 wana Dna Ya kiarabu.

So waarabu hawapo popote si Egpty, si Palestina, si Algeria si Morocco, Hata ukienda Iran ambayo imepakana karibu na waarabu ni Kama asilimia 2 tu dna yao ni ya Kiarabu.

Hivyo si kweli kwamba wale ni wavamizi toka Nchi za kiarabu

3. Angalia Culture Wapalestina na levant kwa Ujumla hawavai Kanzu, nguo zao tofauti na waarabu wengine, Aina zao za kucheza, vyakula vyao, na mambo mengine tofauti kabisa na waarabu wenyewe.

So wapalestina ni wapalestina, mpalestina wa Leo na aliekuwepo hapo Miaka 3000 aliopita ni yule yule, hatuna Haja ya kuzunguka, DNA pekee Inatosha kuthibitisha hili. Ashkenaz Jews Leo wana DNA dhaifu ya kiyahudi kushinda hao Wapalestina wanao waua.


Ukitaka kuelewa Mchezo wa Zionist/British wana force kila mtu awe mwarabu, Mcopt wa Egpty hataki kuitwa mwarabu ila wanalazimisha, Berbers wa Libya ama Algeria hataki kuitwa mwarabu ila anaitwa hivyo hivyo, Druze, amazhingh, Chechens, kushite, Assyrian, Samaritan na makundi kibao hapo Middle East yoyote yanajumushwa yanaitwa tu waarabu hali ya kuwa waarabu ni wale tu wanaoishi kwenye ile Ghuba.
 
Russia na Israel ni ndugu wa damu, mwaka 1948 Marekani na Russia ziliunga mkono kuanzishwa kwa Israel kwa kishindo
Basi huu udugu wa kinafiki.
Maana huko Ukraine Kuna idadi kubwa ya wayahudi na wanachapika vibaya na Russia.
Na Putin nae anashadadia harakati za Palestina .
Nahisi kiongozi wa Russia alikua na interest zake kipindi hiko kuiunga mkono Israel.
Ila Putin imekuwa tofauti.
 
I have a different perspective!

Israel kutwaa maeneo ni matokeo ya vita dhidi yake na mataifa ya Kiarabu baada ya mkwamo wa UN partition plan. Ni matokeo ya defensive war, ambapo kwa mtazamo mwingine, ni tofauti na kile kilichofanywa na Urusi nchini Ukraine (war of aggression).

Je, Tanzania ilifanya makosa kuivamia Uganda ili kumfurusha Idi Amin?

Tukumbuke maeneo ambayo ni Gaza na West Bank kwa sasa yalikuwa chini ya utawala wa "wavamizi" Misri na Jordan kabla ya vita ya mwaka 1967. Hayakuwa independent states.
Mbona unatudanganya kaka?!
Maeneo aliyoteka Israel yote ni ya kupanua Jewish state na yeye ndiye aliyeanza kuvamia hakuanza kuvaniwa.
Pia Palestine ilitakiwa kupaya uhuru Toka kwa Uingereza sip Jordan na Egypt kama unavyotudanganya hapa.
 
Hizo tawala za Ghuba nyingi ni za kiimla na hazipendwi na raia wao hivyo zinategemea mno ulinzi kutoka kwa Marekani ili kubakia madarakani, ndio maana wanakuwa wagumu kuikosoa Marekani na sera zake kwenye hilo eneo hasa kuelekea Israel na Palestine.

Hata hawa Jordan wanaopiga kelele ni sababu tu wanashinikizwa na raia wao hivyo hawataki kuonekana wapo kimya ndio maana wanajitokeza kupaza sauti.
Hapo unatudanganya.
KABLA RAIA WA JORDAN KUANDAMANA KING ABDULLAH ALISHAMFUKUZA BALOZI WA ISRAEL NA KUIFUNGA BALOZI PALE AMMAN.
NA KUNA MIKUTANO ALIYOIKATAA YA US OFFICIALS MPAKA ALIPOSHAWISHIWA NA ELSISI NA THAMIM AL THANI.
Taifa la ghuba lililokua lategemea ulinzi was US ni Saudi Arabia na wenyewe washapatana na Iran na wameweka mkataba wa kushirikiana kiulinzi.
Labda utaje na Egypt.
 
Hapo unatudanganya.
KABLA RAIA WA JORDAN KUANDAMANA KING ABDULLAH ALISHAMFUKUZA BALOZI WA ISRAEL NA KUIFUNGA BALOZI PALE AMMAN.
NA KUNA MIKUTANO ALIYOIKATAA YA US OFFICIALS MPAKA ALIPOSHAWISHIWA NA ELSISI NA THAMIM AL THANI.
Taifa la ghuba lililokua lategemea ulinzi was US ni Saudi Arabia na wenyewe washapatana na Iran na wameweka mkataba wa kushirikiana kiulinzi.
Labda utaje na Egypt.
Nimeshataja Jordan...

Mapatano ya saudia na Iran hayahusiana na huu mzozo.
 
Ndio maana tunawaambia ,hawa watu .
Kuna watu wahuni waliopotosha Sana ethnic axis ya huu ulimwengu .
Huwezi kuniambia mimi mzungu mmoja (Zionist ) toka Ulaya huko convert aliyeadopt uyahudi Leo hii ajiite myahudi , na awe na haki ya kuex
terminate jamii iliyokaa hapo palestina na yenye originality ya hapo miaka maelfu iliyopita .
Kwanza mtu akiamua kudig deeper ,real Jews si hao Ashkenazi , hao wahuni hawana genetic linkup wala uhusiano wowote na uyahudi wenyewe huo wanaoutumia kufanya uhalifu .
Ukiuliza hao wahuni wanatoka kabila gani la Israel ,hawana majibu ,
Ndio maana kuna scholar mmoja aliwaita kabila la 13
Ili kuonyesha jinsi walivyo feki
Real jews wametapakaa kwenye jamii tofauti na hao wahuni waliopo hapo Israel kwa sasa ukitoa Mizraim na Beta Israel wa Ethiopia , Eritrea ,Sudan na Djibouti
Mfano hapa Afrika tu kuna real jews mfano kabila la Lemba toka kule Zimbabwe na South Afrika , wale wana real and undiluted Jewish traditions za miaka mingi ,kuna Yibir kule Somalia wale ni real jews kwa traditions zao hadi genetic linkup .,kuna jews wa west Africa
Kuna real Jews wapo kule kwenye mpaka wa Burma na India ,wanaitwa Bnei Menashe yaani wa toto wa Manase , hawa wanatoka kabila la Manase ,moja kati ya makabila 12 original ya kiyahudi
Kuna wayahudi kule Sahara ndani ya kabila la Tuareg , DawAsak ,hao ni real jews
Kuna wayahudi west Africa ndani ya makabila kama Igbos ,wale traditions zao ni za ule uyahudi pure na wanaji identify kama kabila la Dan moja kati ya kabila la wayahudi original .
Wayahudi wapo ila wametapakaa sehemu tofauti kabisa na wala hawashadadii huo uzayuni wa hao reptilians au uzao WA mijusi/ ibilisi Ashkenazi ambao wanautumia kutimiza agenda zao za kishetani .
Watu wamelishwa Matango pori na elimu feki na mainstream media ambazo ni nyenzo za wazayuni / reptilians uzao wa Ibilisi .
Jitu limoja tapeli linakuja kuua watoto na wazee na kupora ardhi kwa kisingizio cha uyahudi .
Sokapo hapo ! myahudi wa nioko
Una hoja fikirishi mkuu...

Hata Wayahudi wa hapo Ethiopia waliohamishiwa Israel miaka ya 1980 ni wa kabila la Dani pia.

Hata Iran wapo wayahudi (japo inasemekana ni wachache kwa sasa), hawa walihamishiwa huko na mfalme wa Babeli na wameishi huko Uajemi (Iran ya sasa) chini ya tawala kadhaa za kiajemi.

Hawa Ashkenazi Jews ni wa kabila gani hasa ?

zitto junior Mathanzua
 
Politico:

The number of US soldiers injured as a result of the resistance attacks rose to 46 in total.
IMG_20231106_204035.jpg
 
Back
Top Bottom