Yanayosemwa huko Algeria kuhusu tuhuma za kufix mechi ya Tanzania vs Algeria

Yanayosemwa huko Algeria kuhusu tuhuma za kufix mechi ya Tanzania vs Algeria

Kwenye hili kundi, timu iliyostahili kufuzu ni Algeria pekee! Hizo timu 3 zote zilizobakia ni vibonde tu. Angepita Uganda naye angeenda kubebeshwa kapu la magoli tu kwenye hizo fainali, kama itakavyo tokea kwa timu yetu ya Taifa Stars.

Hivyo hata huyo kocha wa Uganda aache kulia lia! Hakuna timu pale. Yule Striker wao Emmanuel Okwi hana tofauti yoyote ile na mzee mwenzake John Bocco.
 
Kiuhalisia kwanza Algeria walibebwa sana. Tanzania tumecheza soka na tumeonesha ukomavu ambao nilikuwa nikitaka uoneshwe siku zote. Hata kama tungefungwa bado timu ya Taifa stars ilijitahidi vya kutosha.
Kwanza goli letu lilikataliwa eti offside
 
Mengi yanasemwa kuhusu matokeo ya mechi ya Tanzania vs Algeria iliyoisha kwa suluhu na kuipeleka Tanzania AFCON 2023 huku Uganda ikikosa nafasi hiyo. Nimechukua kama lisaa kufuatilia nini kinasemwa huko nje na nakileta kwenu muone jinsi wanavyotuchafua na kutuona kama hatukuwa na uwezo wa kuwafunga. Naomba niseme kuwa sisemi wala sijawahi kusema Tanzania imenunua hii mechi, hili naomba nilisisitize sana.

Nianze kwa kusema kuwa tuhuma za kufix mechi ni tuhuma nzito sana katika ulimwengu wa soka na siyo tuhuma za kuzichukulia kwa mzaha.

Katika mechi hiyo, Algeria walimiliki mpira kwa asilimia 80, ambazo ni asilimia kubwa sana katika mchezo na pia ukiangalia idadi ya pasi na usahihi wa pasi zao ukilinganisha na sisi ilikuwa ni mbingu na ardhi. Pamoja na hayo Waalgeria wengi wanadhani hiyo ni moja ya mechi mbaya zaidi kwa timu yao katika miaka 5 iliyopita. Wakati sisi tunaona walitawala mchezo, wenyewe wanaona waliboronga mnoo. Nadhani wenzetu wamejiwekea viwango vikubwa mno kwa timu zao.

“It's the 3rd or 4th worst game for the Algerian team since Belmadi's arrival. You could never have guessed that the national team would have such a level. We clearly did not feel that it is a team that occupies the first places in the FIFA rankings.....,” said Yassine Maloumi, a journalist and football specialist.

Algeria Tanzania – “One of the worst matches in Belmadi”

Nadhani wanaodhani hii mechi ilinunuliwa imechangiwa pia na mazingira yaliyozunguka mechi yenyewe. Kwanza kuna maamuzi ya kocha kuamua siku chache kabla ya mechi kutotumia uwanja uliotumika kwa mechi hiyo kwa ajili ya mazoezi ya timu yao. Tukumbuke huu uwanja eneo lake la kuchezea halikuwa kwenye kiwango kizuri na kocha huyo alikuwa anajua hilo na kwa hiyo wachezaji wa Algeria ambao wengi wamezoea kucheza kwenye viwanja vyenye viwango vya juu wangehitaji kufanyia mazoezi pale ili kuuzoea ila kocha wao alibadili mawazo na hakuwapa hiyo fursa.

Algerian team: a new strange decision by Djamel Belmadi causes a scandal

Kabla ya hapo, kuna maamuzi mengine ambayo Belmadi alikuja kujilaumu ya kuipeleka timu kuweka kambi mji tofauti na utakaochezewa mechi jambo ambalo liliongeza usumbufu kwa wachezaji.

A bitter regret for Djamel Belmadi just a few days from Tanzania!

Mtu mmoja alicomment kuwa anadhani kocha wa Algeria alikuwa anataka kumsaidia kocha wa Tanzania ambaye ni Mualgeria mwenzake akigusia kuwa inaonyesha kila wakicheza na timu inayoongozwa na kocha wa kutoka Algeria inaonekana kama wanawafanya feva.

"I noticed every time we play against Algerian manager we do favors , and I think Belmadi was trying to help the new Algerian coach for Tanzania Amrouche"

Kuna wengine wanamtuhumu pia refa alihusika katika kuipendelea Tanzania. Kocha wa Algeria Belmadi alisema refa alikuja kwenye mechi hiyo akiwa na dhamira ya kuibeba Tanzania. Mchezaji wa zamani wa Morocco Abdessalam Ouaddou amemkingia kifua Belmadi kuwa hawezi kuhusika na kufix mechi hiyo ila naye amemtuhumu refa.

“I watched the match and I have to say it’s not true. I know the two coaches and it is not in their values. […] Stop this misinformation. Algeria was weighed down by a referee who clearly came on a mission during qualifying and was certainly appointed for the cause. Algeria fights for integrity and transparency and clean football ,” Ouaddou.

The Algerian team accused of fixing

Kilichobeba uzito zaidi katika tuhuma hizi ni kocha wa Uganda Milutin Sredojević amenukuliwa akisema waziwazi kuwa mechi hiyo imekuwa fixed ili Tanzania iweze kufuzu. Kocha huyu anayejulikana zaidi nchini kama "Micho" amewahi kuifundisha Yanga kwa hiyo tuhuma hizi zinabeba uzito zaidi kutokana na hiyo historia yake. Micho amesema kilichotokea ni aibu kwa mchezo wa soka na ameahidi kufichua zaidi siku za mbele kuhusu tuhuma hizi.

“What happened during the match between the greens and Tanzania is a shame for football… Algeria was complacent with Tanzania and offered them qualification for the Cup from Africa.”

Controversy! Algeria openly accused of having fixed its match against Tanzania

Inawezekana Micho anajaribu kulinda kibarua chake ila tuhuma hizi ni nzito kutoka kwa mtu kama yeye.

Hili jambo nawaachia wakulungwa, mimi kazi yangu imeisha.
Wanasimba punguzeni roho mbaya
 
Kocha wa Niger alisema wataiachia Uganda ili ishinde iende AFCON baada ya mechi yao na Tanzania. Na jana Uganda wakashinda hawakupanga matokeo?
SAYVILLE n
Yaani mkeka wako wa 3+ kuchanika ndiyo unatuletea makelele hapa? Mbona humsemi kwamba Uganda na Niger walipanga matokeo? Nakocha wa Niger alisema kwenye Press Kwa mkapa hapo kwamba watawaachia Kwa madai tulebebwa taifa
Huyu ni mwanasimba,alitaka Kapombe na kenge wenzie wachezeshwe,hivyo timu kufuzu bila hao kenge wake roho inamuuma

Alitamani tutolewe Ili aseme tulijua hawezi kufuzu bila ya wachezaji wa Simba
 
Kama wamechukia basi tubadilishe matokeo.
Tufanye Mahlezi kafunga 1 na Mzize wa Staz nae kafunga 1. Full time 1 : 1 halafu tuone nani kafuzu ndotoni. Nyambafu zao...
 
Wazee wa kubeti mnatema sumu na hasira baada ya kuiua Stars haikufa,huyo Micho anatetea ugali wake.
Kuna Fainali za Kombe la Dunia nadhani mwaka 2002 Senegal alimkanda Ufaransa 1-0. Watu hawakuamini wakabaki kusema wachezaji wa Ufaransa wameuza mechi kwa vile wengi wao wana asili ya Afrika Magharibi. Visingizio hivyo huwa vipo sana kwenye mpira wa miguu hasa timu maarufu na yenye uwezo mkubwa inapopata matokeo mabovu.
 
Mbona yanga iliwafunga wa Algeria kwao.
Upuuzi mtupu , journalist wanamshutumu kocha kwa kupanga matokeo na kocha anamshutumu refa kwa kupanga matokeo.
Mchezo kuhamishiwa uwanja mungine wakwanza kulalamika alikuwa kocha wa Tanzania .
underdog kuleta upunzani sio kitu kipya Kwenye Mpira , Mbona wao algeria walimsumbua Sana Germany Kwenye World Cup ya 2014 au Mbona Morocco aliwafunga vigogo World Cup ya 2022.
Lakini ni masikitiko kuna kundi la watanzania huku Mitaani na Hata mitandaoni hawajaamini kuwa stars iliizuia Algeria aidha walitamani stars ifungwe .
 
SAYVILLE n

Huyu ni mwanasimba,alitaka Kapombe na kenge wenzie wachezeshwe,hivyo timu kufuzu bila hao kenge wake roho inamuuma

Alitamani tutolewe Ili aseme tulijua hawezi kufuzu bila ya wachezaji wa Simba
Wanasimba punguzeni roho mbaya
Mkuu, mbona nimekuwa positive sana kwenye huu uzi aisee? Nionyeshe wapi na lini niliwahi kulilia wachezaji wa Simba waongezwe katika kikosi hiki kilichocheza na Algeria? Tena sana sana nilihoji utegemezi wa wachezaji kama Boko, niambie huyo ni mchezaji wa klabu gani?

Pia ukumbuke uzalendo haupo tu kwa Watanzania. Hata wao kama wameona kuna chengachenga wana haki ya kuhoji kama ambavyo na sisi tungehoji kama hali tusiyoielewa ingetukuta kwa hiyo tusiwashangae kihivyooo. Kuna video ukitaka nitakupostia ya Amrouche, kocha wa Tanzania ambaye ni mualgeria anarushiana maneno na mchezaji wa Algeria baada ya mechi kuisha. Unadhani hiyo inasababishwa na nini?
 
Mpira wa miguu ni mchezo ambao ukiuzingatia utakufanya ufe kwa presha. Barcelona wakiwa na Messi walipigwa 8 na Bayern. Zambia ya kina Chris Katongo walichukua ubingwa wa Afrika dhidi ya Ivory Coast iliyokuwa na mastaa wote kina Drogba. Yanga ilikula 6 mwaka 1998 dhidi ya Raja. Ukiwa shabiki wa mpira wa miguu punguza hisia.
yanga iliyokula sita bil;a ilistahili
 
Kwa hiyo na hapa walifix match?
 

Attachments

  • images.jpeg
    images.jpeg
    36 KB · Views: 2
Ukweli usemwe Taifa star bila msaada wa third party hatuwezi kuenda Afcon kumbukeni vizuri, kipindi kilicho pita hao Waganda ndo walio tuachia mechi na ka fuzi Afcon kule hatukufanya chochote.
Team ya taifa ni dhaifu ndo ukweli watanzania hawataki kuusikia na hu udhaifu umechangiwa na ushabiki wa timu mbili mnazijua vizuri, pale taifa star nimeangalia mpira sikuona kipaji chochote, Algeria walituachia ile match kiasi kwamba tulipaswa tuofunge kabisa 2-0 ila tulipoteza ata zile chances tulivyo achiwa ndo tukatoka sare.
Sahihi...Kuna chance walituachia kabisa.
 
Back
Top Bottom