Yanga Haina ugomvi na Fei Toto, bali na Timu inayomtaka

Yanga Haina ugomvi na Fei Toto, bali na Timu inayomtaka

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
13,778
Reaction score
14,214
Yanga inafahamu kuwa kunguru Hana kibiongo, kama ukiona kibiongo basi ameinamatu anaokota kitu.

Wazazi, Ndugu, jamaa, marafiki na wapenda mpira wote lazima wafahamu hili. Yanga ni timu kubwa sana kuweza kumuonea Faisal Salum. Yanga haitapendi kuua kipaji Cha mtoto Fei, LAKINi Yanga inafahamu kuwa Fei Toto haendi kuvua samaki baharini bali anaenda kucheza mpira kwenye timu mojawapo nchini au nje ya nchi baada ya kumalizana na Yanga.

Yanga, wazazi, ndugu, jamaa, marafiki na wapenda mpira wote wanaomtakia mema mtoto Faisal wailani hiyo timu inayomtaka mchezaji nje ya taratibu za mpira.

Kama hiyo timu haramu itafanikiwa kumpata mchezaji kwa njia hii baasi mpira wetu utavurugika sana. Kila timu itatumia njia hii kupata wachezaji inayowataka.

Chaajabu hakuna anaeitaja Wala kuitafuta hii timu inayomtaka Faisal kwa njia hii, sio Wazazi wake Faisal, ndugu, mawakili wala TFF. Wala hakuna mtu anaetaka kujua Yanga imepata hasara gani kwa kumlea na kumkosa mchezaji wake kwa muda huu wote. Wala hakuna anaetaka kujua ni wapi Fei Toto alipata pesa za kununulia mkataba wake kwa njia haramu kabisa.

Yanga wako Smart, hiyo timu haramu ilidhani watampata Fei Toto kwa mchezaji kufukuzwa Yanga, au kupewa adhabu ya kulipa fidia. Kifupi Fei Toto, hiyo timu, mawakili, wazazi, wapambe na hata TFF wamenasa kwenye urimbo wa Yanga hadi 2024.

TFF kuruhusu Fei Toto kuitwa timu ya taifa maana yake na wao ni kati ya wadau ambao wamenasa kwenye mtego wa Yanga, wanasononeka sana Fei na "timu yake" mpya kunasa kweñye mtego wa Yanga, na wakati huohuo Yanga inaelekea kutwaa ubingwa bila Fei Toto.
 
Na wewe umeshindwa kuitaja hiyo timu inayomtaka fei unaogopa nn? Ninachojua mm fei hatakiwi na timu yoyote zaidi ya utopolo wenyewe na yeye madai yake ni kuongezewa pesa vingonevo ni bora abaki zenji ale urojo.
 
nimemsikiliza shangazi ivi ile ni sauti yake au kuna kitu anatumia
Mpira una sheria zake na mambo yake, ajira ya mpira sio kama ajira nyingine. Baada ya kunasa kwenye mtego sasa hivi akina shangazi wanatafuta huruma ya umma na busara.

Mbaya zaidi ni pale kijana wao anachina nje ya mpira wakati Yanga ikiendelea kupata matokeo makubwa sana bila Fei. Kama TFF ingekuwa na kaupenyo kwenye hili walaaah ingeshamsaidia kuvunja mkataba.
 
Mmelowaa wapenda vya ubwete
Wameloowa kwelikweli. Yanga wametoa njia 3 za kulimaliza hili tatizo, ambazo ni ama mchezaji arudi Yanga bila masharti yoyote acheze mpira ama mchezaji aje awasilishe ombi lake la kuvunja mkataba au timu inayomtaka mchezaji iende Yanga kuwasilisha ombi lake, Lakini sio mchezaji wala timu inayokwenda Yanga kulimaliza tatizo kwa njia za kimpira wa miguu za Yanga, TFF, CAF na FIFA badala yake wanadhani TFF wana uwezo wa kuisaidia timu kupata mchezaji kwa njia zisizo za kimpira.

Kwanini Fei toto na timu yake mpya hakuna anaekwenda Yanga kulimaliza tatizo kwa njia za kimpira? Nadhani sababu/nadhalia zifuatazo zinahusika sana ambazo ni:

1. Mfanikio ya Yanga bila Fei Toto: Kuna watu waliokuwa wanadhani kuwa Fei ana mchango mkubwa katika ushindi wa Yanga, hivyo wakimchukua Fei kipindi kile Yanga itazorota. Na hii inatiwa nguvu na FEI kuondoka Yanga siku 2 kabla ya mechi na Azam FC wakizani watanusurika kufungwa tena na Yanga kupitia Fei. Baada ya Yanga kuendelea kupata matoe uwanjani ndani na nje ya nchi, dhana ya kwamba yanga itazorota kwa kumkosa Fei haipo tena. Hawamtaki tena.

2. Kiwango cha Fei Toto kushuka: Thamani ya Fei imeshuka sana baada ya kukaa nje, Hivyo hakuna timu itakubali kwenda Yanga kulipishwa fedha nyingi kwa mchezaji wa kiwango hiki cha sasa cha fei.

3. Ligi kwenda ukingoni: Tayari mshindi wa ligi anafahamika na dirisha kubwa la usajili linakaribia, hivyo hiyo timu haioni ni kwaanini iende yanga ikapigwe fedha nyingi kumpata Fei badala ya kwenda kutafuta wachezaji wengine ndani na nje ya nchi.

4. Kosa la kuwasiliana na mchezaji mwenye mkataba: Hiyo timu inayomtaka Fei inafahamu kuwa imetenda kosa kufanya maongezi nA MCHEZAJI MWENYE MKATABA mbichi kabisa, adhabu yake wanaifahamu.

5. Fei hana pesa ya kuvunja mkataba na na kiwango chake kimeshuka wote tumeona alivyocheza timu ya taifa juzi, timu inayomtaka imeanza kupoteza interest ya kumsajili kwa pesa kubwa.

6. Fei ku feel guilty (kujiona mkosaji kwa yanga na wachezaji wenzake kuondoka yanga kwa njia ile: Fei anashindwa kurudi kucheza yanga baada ya mambo yote yale, anaonekana kama mchezaji aliyekuwa na nia mbaya na timu yake isifanye vizuri. Yaani hana tofauti na Gundus aliyetaka kumsaliti ndugu yake osman kwa kuhamia kambi ya maadui wa Wakai. Hii inatiwa nguvu na Sauti ya Bernard Morrison iliyosiikika akimwambia Fei kuwa unataka kuleta matatizo Yanga acha acha kabisa. Hii inaonyesha kuwa hata wachezaaji wezake walimuonya asifanye vile. Anaona aibu kurudi Yanga.

7. Utovu wa nidhamu: Come easy going easy. Hakuna timu makini na hadhi itapenda kuwa na mchezaji anaepatikana kwa njia hii katika zama hizi. Haaminiki hata kidogo, anaweza kuhamia timu nyingine wakati wowote bila kujali timu iko kwenye kipindi gani na nafasi gani kwenye mashindano.

Dhambi ndogo kwake ni kurudi yanga na kuomba msamaaha na aongeze bidii ma 3 kwenye mazoezi ili amshawishi kocha tena kwa kiwango chake.
 
Yanga inafahamu kuwa kunguru Hana kibiongo, kama ukiona kibiongo basi ameinamatu anaokota kitu.

Wazazi, Ndugu, jamaa, marafiki na wapenda mpira wote lazima wafahamu hili. Yanga ni timu kubwa sana kuweza kumuonea Faisal Salum...
Una akili sana.
 
Wameloowa kwelikweli. Yanga wametoa njia 3 za kulimaliza hili tatizo, ambazo ni ama mchezaji arudi Yanga bila masharti yoyote acheze mpira ama mchezaji aje awasilishe ombi lake la kuvunja mkataba au timu inayomtaka mchezaji iende Yanga kuwasilisha ombi lake, Lakini sio mchezaji wala timu inayokwenda Yanga kulimaliza tatizo kwa njia za kimpira wa miguu za Yanga, TFF, CAF na FIFA badala yake wanadhani TFF wana uwezo wa kuisaidia timu kupata mchezaji kwa njia zisizo za kimpira.

Kwanini Fei toto na timu yake mpya hakuna anaekwenda Yanga kulimaliza tatizo kwa njia za kimpira? Nadhani sababu zifuatazo zinahusika sana ambazo ni:
1. Mfanikio ya Yanga bila Fei Toto: Kuna watu waliokuwa wanadhani kuwa Fei ana mchango mkubwa katika ushindi wa Yanga, hivyo wakimchukua Fei kipindi kile Yanga itazorota. Na hii inatiwa nguvu na FEI kuondoka Yanga siku 2 kabla ya mechi na Azam FC wakizani watanusurika kufungwa tena na Yanga kupitia Fei. Baada ya Yanga kuendelea kupata matoe uwanjani ndani na nje ya nchi, dhana ya kwamba yanga itazorota kwa kumkosa Fei haipo tena. Hawamtaki tena.

2. Kiwango cha Fei Toto kushuka: Thamani ya Fei imeshuka sana baada ya kukaa nje, Hivyo hakuna timu itakubali kwenda Yanga kulipishwa fedha nyingi kwa mchezaji wa kiwango hiki cha sasa cha fei.

3. Ligi kwenda ukingoni: Tayari mshindi wa ligi anafahamika na dirisha kubwa la usajili linakaribia, hivyo hiyo timu haioni ni kwaanini iende yanga ikapigwe fedha nyingi kumpata Fei badala ya kwenda kutafuta wachezaji wengine ndani na nje ya nchi.

4. Kosa la kuwasiliana na mchezaji mwenye mkataba: Hiyo timu inayomtaka Fei inafahamu kuwa imetenda kosa kufanya maongezi nA MCHEZAJI MWENYE MKATABA mbichi kabisa, adhabu yake wanaifahamu.

5. Fei hana pesa ya kuvunja mkataba na na kiwango chake kimeshuka wote tumeona alivyocheza timu ya taifa juzi, timu inayomtaka imeanza kupoteza interest ya kumsajili kwa pesa kubwa.

5. Fei ku feel guilty (kujiona mkosaji kwa yanga na wachezaji wenzake kuondoka yanga kwa njia ile: Fei anashindwa kurudi kucheza yanga baada ya mambo yote yale, anaonekana kama mchezaji aliyekuwa na nia mbaya na timu yake isifanye vizuri. Yaani hana tofauti na Gundus aliyetaka kumsaliti ndugu yake osman kwa kuhamia kambi ya maadui wa Wakai. Hii inatiwa nguvu na Sauti ya Bernard Morrison iliyosiikika akimwambia Fei kuwa unataka kuleta matatizo Yanga acha acha kabisa. Hii inaonyesha kuwa hata wachezaaji wezake walimuonya asifanye vile. Anaona aibu kurudi Yanga.

Dhambi ndogo kwake ni kurudi yanga na kuomba msamaaha na aongeze bidii ma 3 kwenye mazoezi ili amshawishi kocha tena kwa kiwango chake.
Safi kabisa.
 
Yule Mwanasheria wa Fei ni kolaza.

Uwa hao Wanasheria/Mawakili wanajihita wasomi ila huyu ni dhaifu.
 
Yanga ni sawa na Domo zege demu kakukataa unamngangania
 
Yanga ni sawa na Domo zege demu kakukataa unamngangania
wewe jamaa huna akili ya mambo ya mpira hata kidogo. kama ingekuwa hivyo bro hata akina pogba, mmbape, messi wangeshaondoka kwenye timu zao na kwenda kule wanakopenda. Mfano, hakuna mchezaji Simba ambae hapendi kucheza Yanga kwa sasa, kama ingekuwa rahisi kuhama hivyo kama wanavyotaka mawakili wa Fei basi Kanoute na Inonga wangeshahamia yanga kitambo. Kama ingekuwa rahisi kiasi hicho timu inayomtaka Fei ingeshamchukua, lakini hebu ona imejificha uvunguni mwa kitanda cha mkwewe ikisikilizia kwa mbaali akina shangazi wakipambana.
 
Yanga inafahamu kuwa kunguru Hana kibiongo, kama ukiona kibiongo basi ameinamatu anaokota kitu.

Wazazi, Ndugu, jamaa, marafiki na wapenda mpira wote lazima wafahamu hili. Yanga ni timu kubwa sana kuweza kumuonea Faisal Salum. Yanga haitapendi kuua kipaji Cha mtoto Fei, LAKINi Yanga inafahamu kuwa Fei Toto haendi kuvua samaki baharini bali anaenda kucheza mpira kwenye timu mojawapo nchini au nje ya nchi baada ya kumalizana na Yanga.

Yanga, wazazi, ndugu, jamaa, marafiki na wapenda mpira wote wanaomtakia mema mtoto Faisal wailani hiyo timu inayomtaka mchezaji nje ya taratibu za mpira.

Kama hiyo timu haramu itafanikiwa kumpata mchezaji kwa njia hii baasi mpira wetu utavurugika sana. Kila timu itatumia njia hii kupata wachezaji inayowataka.

Chaajabu hakuna anaeitaja Wala kuitafuta hii timu inayomtaka Faisal kwa njia hii, sio Wazazi wake Faisal, ndugu, mawakili wala TFF. Wala hakuna mtu anaetaka kujua Yanga imepata hasara gani kwa kumlea na kumkosa mchezaji wake kwa muda huu wote. Wala hakuna anaetaka kujua ni wapi Fei Toto alipata pesa za kununulia mkataba wake kwa njia haramu kabisa.

Yanga wako Smart, hiyo timu haramu ilidhani watampata Fei Toto kwa mchezaji kufukuzwa Yanga, au kupewa adhabu ya kulipa fidia. Kifupi Fei Toto, hiyo timu, mawakili, wazazi, wapambe na hata TFF wamenasa kwenye urimbo wa Yanga hadi 2024.

TFF kuruhusu Fei Toto kuitwa timu ya taifa maana yake na wao ni kati ya wadau ambao wamenasa kwenye mtego wa Yanga, wanasononeka sana Fei na "timu yake" mpya kunasa kweñye mtego wa Yanga, na wakati huohuo Yanga inaelekea kutwaa ubingwa bila Fei Toto.
tusikitike wote kwa kusema FEI KAINGIZWA CHA KIKE NA WASIOJUA MPIRA NA TARATIBU ZAKE
 
tusikitike wote kwa kusema FEI KAINGIZWA CHA KIKE NA WASIOJUA MPIRA NA TARATIBU ZAKE
Mawakili wake Fei waache kufananisha ajira ya mpira na ajira nyingine na ajira ya mpira na ndoa. Vina tofauti kaaabisa. Wanajuwa ni kwanini mambo ya mpira hayaingiliwi na serikali wala na chombo chochote? wasimptoshe kijana wetu mdogo anaechipukia kutafuta riziki kwa miguu yake. Ningewaona wana akili nyingi na kumtakia kijana mema kama wangemwambia avumilie abaki yanga aendelee kucheza hadi mkataba wake uishe na asikubali kuongeza mkataba mpya tena. Lakini sasa hivi kila mtu anakuwa na mashaka na taaluma yao ya sheria. Waaanaonekana wamekosea na hata tusiokuwa na taaluma ya sheria.
 
Yanga inafahamu kuwa kunguru Hana kibiongo, kama ukiona kibiongo basi ameinamatu anaokota kitu.

Wazazi, Ndugu, jamaa, marafiki na wapenda mpira wote lazima wafahamu hili. Yanga ni timu kubwa sana kuweza kumuonea Faisal Salum. Yanga haitapendi kuua kipaji Cha mtoto Fei, LAKINi Yanga inafahamu kuwa Fei Toto haendi kuvua samaki baharini bali anaenda kucheza mpira kwenye timu mojawapo nchini au nje ya nchi baada ya kumalizana na Yanga.

Yanga, wazazi, ndugu, jamaa, marafiki na wapenda mpira wote wanaomtakia mema mtoto Faisal wailani hiyo timu inayomtaka mchezaji nje ya taratibu za mpira.

Kama hiyo timu haramu itafanikiwa kumpata mchezaji kwa njia hii baasi mpira wetu utavurugika sana. Kila timu itatumia njia hii kupata wachezaji inayowataka.

Chaajabu hakuna anaeitaja Wala kuitafuta hii timu inayomtaka Faisal kwa njia hii, sio Wazazi wake Faisal, ndugu, mawakili wala TFF. Wala hakuna mtu anaetaka kujua Yanga imepata hasara gani kwa kumlea na kumkosa mchezaji wake kwa muda huu wote. Wala hakuna anaetaka kujua ni wapi Fei Toto alipata pesa za kununulia mkataba wake kwa njia haramu kabisa.

Yanga wako Smart, hiyo timu haramu ilidhani watampata Fei Toto kwa mchezaji kufukuzwa Yanga, au kupewa adhabu ya kulipa fidia. Kifupi Fei Toto, hiyo timu, mawakili, wazazi, wapambe na hata TFF wamenasa kwenye urimbo wa Yanga hadi 2024.

TFF kuruhusu Fei Toto kuitwa timu ya taifa maana yake na wao ni kati ya wadau ambao wamenasa kwenye mtego wa Yanga, wanasononeka sana Fei na "timu yake" mpya kunasa kweñye mtego wa Yanga, na wakati huohuo Yanga inaelekea kutwaa ubingwa bila Fei Toto.
Umeongea point tu. Umegusa sana mfupa wa mikia. Hasa hasa huyu bobansunzu siku hizi anajiita chama + baleke
 
Kesi ya Fei haitakiwi kumalizwa kwa kutumia hekima Wala busara. Hii ni kesi ya kwanza TFF, CECAFA, CAF na FIFA mchezaji kutaka kuvunja mkataba kwa kukosa furaha TU kwenye timu yake. Tujuavyo sisi kukosa furaha ni kichaka TU wanachokitumia wapambe wake lakini tunafahamu kuwa Kuna mtu ametoa pesa za kuvunjia mkataba wa Fei. Kuna rundo la wachezaji, viongozi wa timu na wadau wanasubiri kuona hili jambo litakwisha vipi. Kama tutatanguliza busara kwenye hili ni sawa na kuanza safari kwa mguu mbaya.

Ni kweli kwamba kijana wetu tunatakiwa kutunza kipaji chake lakini tutaharibu sana kama tutatumia busara kwenye hili. Ni heri tumtose mchezaji mmoja kwa faida ya mpira wetu. TFF Hana ubavu wa kuvunja mkataba wa mchezaji, ila TFF ndiye mwenye mamlaka ya kuitangaza kuwa mchezaji Hana mkataba, Yuko huru kutokana na vipengele fulani kati ya mchezaji na klabu yake. Hawa mawakili wa Fei wamekielewa kile kifungu Cha kanuni ya TFF. Kifungu kile kinamaanisha kuwa baada ya mambo yooooote ya ndani ya klabu kuhusu mchezaji na timu TFF ndio watu wa mwisho wa kuhalalisha mkataba au kufunjika kwa mkataba.
 
Back
Top Bottom