Yanga hii ya Lwandamina, hapana

Yanga hii ya Lwandamina, hapana

DaaaaH umeongea point Sana jamaaa ujue watu wengi sasa wanaendeshwa na mihemko wanashindwa kutambua kuwa mambo yanawakat.. huwez kuwa bora kipnd chote ni lazma tujifunze kuwa wavumilivu kama kocha mbovu itajulikana tu hakuna haja ya kuwa na jazba kwasabab ya mechi mbili za mwanzo


Kuna jambo ambalo watu wengu hawalitambui linalo endelea pale Jangwani.

jambo hilo linaitwa "usimikwaji wa kizazi kipya".

Kinachofanywa hivi sasa na Yanga ni kuandaa na kutengeneza kizazi kipya cha wanajangwani ambao watahakikisha kinafanya makubwa kama hiki kizazi kinachomaliza muda wake pale jangwani na mafanikio lukuki
mfano:- (Yondani, Nadir, Niyonzima, Abdul, O Joshua,).

Tofauti na mtindo wetu wa awali wa recruiting new ready made player, hivi sasa tunajaribu kuandaa wale ambao tunaona huko mbeleni watakuwa msingi bora wa klabu na kuendeleza rekodi ya kutwaa mataji kama ilivyo kawaida yetu.

Kuna jambo mbele ambalo linaonekana hivyo kwa taadhari kubwa ikaonekana ni vyema hii hatua ichukuliwe mapema.

"wabongotumezoea mteremko na shortcut, ndio maana mleta mada ameanza moja kwa moja kumlalamikia GL. "
 
Timu haikuanza kudorora msimu huu tu,bali tangu alipifika lwandamina soka ikavurugika kabisa,tulichukua ubingwa kwa sababu tu ya mistake za simba na matokeo mazuri aliyoanza nayo pluijm.nyie ndio mashabiki ambao ukichunguza ni mashabiki wa arsenal pia,mashabiki wenye subira iliyopitiliza mpaka pale timu ikishadhalilika kiasi cha kupitiliza ndio mtastuka labda.
Timu kumalza dk 45 wanahema pumzi hamn zile pasi rula hamn tena Mi naona kocha viatu vikubwa kwake toka siku ya kwanza amefika

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dah! Kila ninapo itazama timu yangu ikicheza nakosa raha kabisa, sioni timu iliyosifika kwa lile soka tamu ya kampa kampa tena. Timu ipoipo tu sasa hivi na inacheza mradi inacheza

Najua viongozi wanaliona hili lakini wanashindwa kumtimua Lwandamina sababu timu haina pesa Sasa hivi na kuvunja nae mkataba ni gharama kubwa sababu itabidi wamlipe kwahiyo wameamua kubaki wakitizama tu.

Kilichobaki ni kusubiri tu mpaka timu ishuke daraja sasa maana ndiko tunakoelekea, wachezaji hata morali hawana tena japo wapo wachache wanaojitahidi kujituma lakini Mipango hamna kabisa.

Ukihoji unaambiwa story za kwamba sijui timu ilikuwa ikiwategemea kina Msuva kushambulia tokea pembeni. Sasa hivi hawapo kocha bado anatafuta mfumo, atautafuta mpaka mwisho wa ligi kwa staili hii.
Ligi bado mbichi sana yan
 
Back
Top Bottom