Yanga ilikuwaje wakaitwa Kandambili na Pan Africa wakaitwa Raizoni?

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2011
Posts
21,470
Reaction score
40,593
Mpaka leo wachora katuni hutumia picha ya Kandambili kuwakilisha timu ya Yanga. Nakumbuka ni utani kati ya Yanga na Pan African, ndiyo ulileta jina la Kandambili Yanga na Raizoni Pan African.

Raizoni ndiyo vilikuwa viatu vya maana sana zama hizo, na Kandamimbili zilikuwa zinavaliwa na watu maskini na hohe hahe. Ni kwa nini Yanga huwa inapewa majina ya kuonesha kuwa wao ni watu wa Makasiriko??
 
Me sijui ila subiri waje wakina kaka Mshana Jr watupe history kdg
 
Pondamali afungue account huku Jamii forums atupe historia za zamani,hili Swali fasta tu angejibu. Halafu jamaa ni msimuliaji mzuri.
 
Kuna dhana mbili. Moja ni kuwa mashbiki wa Yanga huvua kandambili zao na kuzishika mkononi wakisukuma basi lao kutoka Karume au taifa mpaka Jangwani. Wakawa wanaitwa kandambili.

Dhana ya pili, ni wakati wa mgawanyiko, Kina Shiraz na Mangara wakawa wanawaambia wachezaji waliobaki na Tambwe Leya kuwa achaneni na hao kandambili., jina walilokuwa Malo kabla ya mgawanyiko mje huku Raizoni.

Mashbiki wa Simba pia walikuwa wakijiita Raizoni.

Halafu Yanga hatuchukii tukiitwa kandambili. Tulipokea jina hilo with pride kutoka kwa wazee wetu. Nakumbuka tawi la Yanga mtaa wa Mkumba Temeke lilikuws linaitwa "Msichoke" na lilikuws na picha ya Kandambili kubwa tu ya kuchora kwenye ubao.
 
Ilikuwaje Simba mkajiita QUEENS FC kwa kupenda wenyewe???????
 
Nahc baada ya kuhama kucheza peku walichezea kandambili....mtanirekebisha kama siko sahihi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…