Yanga ina matatizo makubwa kimataifa

Yanga ina matatizo makubwa kimataifa

Analysis nzuri isipokuwa kwenye ball control Kwa Wachezaji wa mbele. Mayele na Ki ni ball holders Kwa hiyo hujawatendea haki kuwaweka kapu moja na Kisinda na Moloko.
Sina hakika km umewafuatilia vizuri. Mayele ni mfungaji mzuri lakini anapoteza sana mpira kirahisi. Nakuomba umfatilie Jumapili na Mazembe. Aziz ki naomba na yeye umfatilie utaungana na mimi.
 
Wakati nikikubaliana na hoja zako kwa asilimia kubwa, nina swali kwenye yako ya kwanza. Kwenye hiyo hoja umesisitiza umuhimu wa wachezaji wenye maumbo makubwa.

Swali ni inakuwaje nchi zenye wachezaji wasio na maumbo makubwa kama Japan na Korea Kusini zinaweza kupata matokeo dhidi ya giants kama Cameron na Ujerumani ?

Sent from my SM-A6050 using JamiiForums mobile app
 
Sina hakika km umewafuatilia vizuri. Mayele ni mfungaji mzuri lakini anapoteza sana mpira kirahisi. Nakuomba umfatilie Jumapili na Mazembe. Aziz ki naomba na yeye umfatilie utaungana na mimi.
Naongea nikiwa nimewaona na kuwafuatilia Sana. Mayele ana uwezo mkubwa wa kuhold mpira, sema Kwa vile yeye ndo last man anawahi kuachia ili akakae sehemu yake na hapo ndo anakosa Nani ampokee majukumu. Jana umeona tofauti alipokuwa Peke yake na alipoingia Musonda?
 
Simba sasa mmekuwa wachambuzi wa kikosi cha Yanga mnasahau juzi mmepigwa. Kwa Yanga hii ndio ilikuwa mechi ngumu kuliko zote, ni sawa na Raja wanavyowasubiri nyumbani.

Sent from my SM-A6050 using JamiiForums mobile app
Ya juzi tumeyasahau tena wala hayatuumizi

Kwani we yale maneno mliyokuwa mnatutolea juzi hujayasahau?

Hao Raja sijui kina Roja waache waje ila hapa Lupaso haiwezi kuwa simple kwao hata siku moja
 
Wakati nikikubaliana na hoja zako kwa asilimia kubwa, nina swali kwenye yako ya kwanza. Kwenye hiyo hoja umesisitiza umuhimu wa wachezaji wenye maumbo makubwa. Swali ni inakuwaje nchi zenye wachezaji wasio na maumbo makubwa kama Japan na Korea Kusini zinaweza kupata matokeo dhidi ya giants kama Cameron na Ujerumani ?

Sent from my SM-A6050 using JamiiForums mobile app
Mbinu tu za uchezaji.....
 
Mbinu tu za uchezaji.....
Unapokuwa na wachezaji wafupi kuna vitu makocha huwa wasisitiza kwa wachezaji wake.
1. Kuepuka kufanya faulo maeneo ya hatari.
2. Kuepuka mipira ya kona.
3. Kufanya taiti markings.

Km unakumbuka ile Barcelona ya kina Xhavi,Iniesta na Messi walikuwa wanakwepa sana kona au faulo kwenye eneo lao,muda mwingi walikuwa wanamiliki wao mpira. Wakipoteza ndani ya sekunde chache wanaurudisha kwenye himaya yao. Tujiulize je sisi tuna hao wachezaji wafupi na mafundi km kina Xhavi na Iniesta wa kuwafanya timu pinzani wateseke ndani ya uwanja? Kwa sababu ukiwa na wachezaji wafupi silaha kubwa ni kumiliki mpira,akili nyingi na nidhamu kubwa.
 
Unapokuwa na wachezaji wafupi kuna vitu makocha huwa wasisitiza kwa wachezaji wake.
1. Kuepuka kufanya faulo maeneo ya hatari.
2. Kuepuka mipira ya kona.
3. Kufanya taiti markings.

Km unakumbuka ile Barcelona ya kina Xhavi,Iniesta na Messi walikuwa wanakwepa sana kona au faulo kwenye eneo lao,muda mwingi walikuwa wanamiliki wao mpira. Wakipoteza ndani ya sekunde chache wanaurudisha kwenye himaya yao.
Kwa maana hii unasema tatizo siyo vimo vya wachezaji ila mbinu za mwalimu?

Sent from my SM-A6050 using JamiiForums mobile app
 
Ukiitazama Yanga vizuri utagundua kuwa timu inamatatizo mengi ndani ya uwanja kuliko ubora na sifa inazopewa. Kwanini? Naomba unifuatilie kwa makini.

1. Kuwa na mabeki wafupi eneo la kati ni tatizo kubwa. Ukiangalia timu nyingi zinazoshiriki haya mashindano zimejidhatiti kwa kucheza kimbinu ikiwamo kutumia set-peaces(mipira ya kutenga)kupata ushindi. Hivyo wanatumia washambuliaji warefu eneo la mbele. Yanga wameenda kwenye mashindano wakitumia walinzi wale wale wa eneo la kati. Unaweza kuwatumia Job na Bangala kwenye ligi yetu nzima na usiadhibiwe kwa mipira ya juu lakini si kwenye mashindano haya makubwa. Ukiondoa Yanga, timu zingine zote TP Mazembe,Monastery,na AFC Bamaco zote zina watu kweli kweli! Ni mijitu haswaaa! Kocha atake asitake lazima apange walinzi warefu hata km wanamangufu mengine hasa Mamadou na Mwamnyeto. Vinginevyo tutawalaumu bure akina Job.

2. Si sawa Kumtumia Kibwana eneo la kushoto. Unapomtumia Kibwana eneo la kushoto unaongeza idadi ya mabeki wafupi. Lakini pia kwenye kushambulia kibwana si mzuri. Hivyo unapata hasara mara mbili. Ni bora kumtumia Lomalisa mwenye kimo kizuri na tabia ya kupanda kushambulia ukaongeza kiungo wa kumsaidia kukaba.

3. Yanga inakosa viungo wakabaji wenye mapafu ya Mbwa. Aucho hana kasi na kwenye kukaba si mzuri na hawezi kukimbia eneo kubwa la uwanja. Hata Sureboy anashida hiyo hiyo. Mudathiri anaweza kukaba lakini anapiga pasi mkaa nyingi. Msimu ujao atafutwe kiungo mkabaji ila kwa waliopo sioni wa kuziba hili pengo.

4. Ubunifu mdogo na viungo wasio na kasi eneo la mbele. Yanga inakosa viungo wabunifu na wenye kasi eneo la mbele. Kwa namna viungo wa Yanga wanavyocheza kama mpinzani ana mkakati mzuri wa kujilinda mechi inaweza kuchezwa wiki nzima bila Yanga kupata goli. Timu inatabirika kirahisi sana kwenye kushambulia. Hakuna viungo wanaoweza kulazimisha mabeki kufanya makosa. Kimataifa hii ni "disadvantage" kubwa.

5. Mawinga wa Yanga wana kiwango duni. Winga pekee pale Yanga mwenye hadhi ya kucheza kwenye mashindano makubwa ni "Kichaa" Morrison. Twisila na Moloko hawana viwango vya kucheza haya mashindano. Huwezi kuwa na winga ambaye yeye ndo anaongoza kufanya faulo kuliko yeye kufanyiwa faulo.

6. Mipira kupotea kirahisi eneo la mbele. Viungo na washambuliaji wote wa Yanga wanatatizo la ama kupiga pasi mkaa na "poor ball control ". Mayele, Tuisila, Aziz Ki,Msonda, Faridi na Moloko wote wana hili tatizo. Unapokuwa na pasi mkaa nyingi na uwezo mdogo wa kumiliki mpira unakuwa unawasaidia mabeki wa timu pinzani kujilinda. Ndio maana kumkaba Mayele huwa kazi rahisi. Fuatilia mechi nyingi za kimataifa Mayele huwa hana madhara na hugeuka mzurulaji.

7. Kushambulia kwa idadi ndogo. Viungo washambuliaji wanaotakiwa kumsaidia Mayele huwa hawasogei jirani na goli. Hata km Mayele atajitahidi kupambana bado anajikuta yupo peke ake. Sijui ndo mbinu ya kocha au ni uzembe wa wachezaji wenyewe! Hapa ndipo napowapongeza Simba. Simba wakiamua kumtafta mpinzani Shabalala,Kapombe,Sakho,Chama,Bocco na Mzamiru wote utawaona wanaingia kushambulia. Hiki kitu hakipo Yanga.

8. Yanga wanacheza staili moja mwanzo mwisho. Haya si mashindano ya kujisifu kumiliki mpira au kipiga chenga. Haya ni mashindano ya mabingwa kila timu inauwezo wa kuchezea mpira,muhimu ni mkakati wa kukufanya ushinde. Timu zetu za Kitanzania bado zina "mentality" ya kumiliki mpira. Hata tufungwe ngapi utasikia mashabiki wanasema tumeupiga mwingi sana. Wenzetu wameshahama huko na sasa wanacheza kimalengo na kimkakati zaidi. Kila tendo analolifanya mchezaji analifanya kwasababu sio kukimbia kimbia na mpira tu.

Timu haijengwi siku moja. Yanga wamefanikiwa kujenga timu ya ushindani kwa mashindano ya ndani sasa wanatakiwa kutengeneza timu kwa mashindano ya kimataifa. Hizi mechi mzitumie kuona mapungufu na si kufikiria kushindana pekee. Hata Simba nao hawako salama nimeitumia Yanga km reference pointi tu.

Nawasilisha.
Hiyo namba 7 ukweli mtupu 100%
 
Back
Top Bottom