Yanga kutoandika majina kwenye jezi

Mpagani

Senior Member
Joined
Oct 8, 2016
Posts
134
Reaction score
66
Wakuu wasalaam,

Kwa heshima na taadhima naomba kuuliza kwa mwenye kufahamu hii kitu leo nilikuwepo uwanja wa taifa kushuhudia mechi ya Yanga na Mwadui nimeona ajabu timu kubwa kama Yanga kutoandika majina katika jezi zake.

Je, ni makusudi au mdhamini hana pesa ya ku print mbona mbele ya jezi zina nembo kulikoni?
 
Hili jambo huwa linanitatiza sana ila ipo siku ukweli utadhihili
 
Hata mi huwa nashangaaa sana kwaani kuandika jina kuna gharama gani kwa club kubwa kama Yanga.
 
Yanga sio leo tu, Mara nyingi huwa hawaandiki majina. Sijui tatizo ni nini
 
Hongera kwa kuingia taifa kwa mara ya kwanza. Kwani matokeo yalikuwaje?
 
Mashabiki wa Yanga wanahitaji matokeo na si upuuzi kama wa Kichuya jina kubwa kwenye jezi uwanjani anakata viuno tu hana lolote.
 
Hili la majina nilishalilalamikia siku nyingi , andikeni bana.
 
Matokeo muhimu kwetu sio majina, na wala sitaki waandike maana watani wetu wameanxa mda kuandika lkn matokeo yao 0
 
Cha msingi na sekondari ni matokeo tu......

wavae chupi wasivae...hilo ni la kwao.


sisi mashabiki tunataka alama muhimu 3.
 
Matokeo muhimu kwetu sio majina, na wala sitaki waandike maana watani wetu wameanxa mda kuandika lkn matokeo yao 0
HUYU JAMAA ANADHANI KUWA JEZI ZA YANGA ZIKIANDIKWA MAJINA BASI NA MAKALI YA YANGA SC NAYO YATAONGEZEKA......

NDIO AINA YA WAPENZI WA SOKA TULIONAO HAPA BONGO...

NO WONDER NA MPIRA WETU WENYEWE UMEDUMAA MITHILI YA MAWAZO YA KWENYE HUU UZI..
 
Walishinda au hawakushinda? Wanaongoza ligi au hawaongozi? Mengine hayo hayakuhusu, au huwajui wachezaji ulitaka jezi zikusaidie.


ALIKUWA ANAWAONA TU KWENYE MAGAZETI HIVYO BAADA YA KUPATA NAFASI KWA MARA YA KWANZA KUINGIA TAIFA ALIPENDELEA AWAONE KWA MACHO NA KUTHIBITISHA KWA MAJINA YAO YA MGONGONI....


Daaahh!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…