Yanga Kwafukuta

wajibisha

Member
Joined
May 16, 2021
Posts
90
Reaction score
215
Yanga hali si shwari tena.

Kambi mbili zinavutana.

Upande huu ni uongozi uliochaguliwa na wanachama (Msolwa & Mwakalebela)

Upande ule ni wa wadhamini GSM ( Engineer Hersi &Senzo)

Upande wa wananchi wanahisi mamlaka yao yanapokwa kila kukicha. Sasa hivi mambo ya uendeshaji yanafanyika pale Samora Tower sio tena jangwani.

Haji Manara aliletwa na GSM huku viongozi wakiwa hawana furaha. Antonio Nugaz anawekwa pembeni, kina Msolwa hawana na kusema.

Muda si mrefu tutaanza kupata yaliyomo yamo.

Watamwaga mboga muda si mrefu. Mauzo ya JEZI yatawekwa wazi na hapo ndio tutajua janja janja zote.

Mapato ya siku ya wananchi yameenda wapi? Tutajua muda si mrefu.

Kwa nini GSM anajipa majukumu ya uongozi wakati yeye ni mdhamini kama wadhamini wengine pale Yanga?

GSM pia ni mzalishaji na muuzaji wa JEZI za Yanga. Mbona mkataba hauwekwi wazi.

Yajayo yanafurahisha. Mboga inamwaga muda si mrefu.
 
Hao viongozi wanaotaka uwazi wa fedha itakuwa sahihi kama ndo wanaotoa fedha za usajili na kulipa mishaara wachezaji lakini kama hawafanyi hayo wanataka kula tu fedha na hawana jipya.
 
Simba kwenye jezi Wanaingiza Bilioni 2 haijalishi Vunja Bei Kauza au hajauza.Bila shaka Atauza tu. Yanga hawajui chochote Yaani ndo 'Wamepigwa' hivyo...!
[emoji15][emoji15][emoji15]sio Simba anaingiza bilioni 2,Muddy mwenye timu yake ndo anaongiza bilioni 2..
 
Usipoongelewa basi ujue hauna makeke...hongera mwananchi [emoji122]
 
Sisi tuna watu sisi tuna watu, kumbe watu wenyewe wawili tu. Mzee Manara na Mh. Kikwete.
Wengine wote Haji Manara ndiye anajua viumbe gani wale.
 
Wewe ujue unachokisema…. Yanga ile bado ni mmoja na GSM ndio anaendesha timu…. Hata Uongozi unapenda na kubariki….
 
Hao viongozi wanaotaka uwazi wa fedha itakuwa sahihi kama ndo wanaotoa fedha za usajili na kulipa mishaara wachezaji lakini kama hawafanyi hayo wanataka kula tu fedha na hawana jipya.

Mbona Simba ambayo hata haiwahusu mlikua mnataka uwepo uwazi wa fedha bila kuzingatia ni nani anatoa pesa? Kwenu kimeumana mnaanza kuja na vi maneno maneno
 
Mbona Simba ambayo hata haiwahusu mlikua mnataka uwepo uwazi wa fedha bila kuzingatia ni nani anatoa pesa? Kwenu kimeumana mnaanza kuja na vi maneno maneno
Sisi kama washabiki kindakindaki wa Simba hatujawahi kuwa na shida na mwekezaji wetu, waliokuwa wakisema hayo ni washabiki wa Yanga na mianachama ya Simba mijizi inayotaka kujineemesha kupitia klabu yetu.
 
hizi ni habari za ndani sana jikoni
 
Na wewe ni mchawi kama Mshana Jr? Wachawi hawapendi kabisa sehemu ndugu wakikaa kwa amani
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…