Yanga mna Juhudi, ombeni mpewe majaaliwa!

Yanga mna Juhudi, ombeni mpewe majaaliwa!

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2011
Posts
21,470
Reaction score
40,593
Mnaiona kama vile Simba haina fowadi wa kueleweka, lakini ndiyo inayoongoza kwa kufunga magoli mengi kwenye Ligi kuu Tanzania. Mnaiona simba kama vile ni timu dhaifu lakini Simba na Yanga zote zilikuwa kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika, Yanga ikashindwa kufuzu hatua ya Makundi, Simba ikafuzu.

Leo Yanga iko kwenye Kombe la Shirikisho wanajisahaulisha kwamba kabla ya kwenda huko na wenyewe pia walikuwa kwenye mashindano ya Klabu Bingwa Afrika wakatolewa. Hivi inakuwaje timu dhaifu ya Simba inaendelea kuwemo kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika wakati timu Imara ya Yanga ilitolewa!!??

Bidii kubwa mliyonayo wanayanga, ombeni pia mjaliwe na nasibu ya kufanikiwa, la sivyo kila siku mtaumwa na mafanikio ya Simba mnaowaona ni timu dhaifu lakini wamejaaliwa sudi njema!!
 
Msimu wowote!!!
Kwahiyo ni misimu yote ilikuwa inazungumziwa Simba ni mbovu kuliko Yanga au ni msimu huu ndio imeibuka hiyo hoja? Na kama ni misimu yote inazungumzika hivyo, kwanini kwenye uzi wako hukuongelea kama ni hoja ya misimu badala yake ukaongelea kuhusu msimu wa sasa?
 
Na inabidi uelewe kwenye kila kundi lazima kuwe na giant mmoja,yaani kundi lenu giant alikuwa al hilal na wengine ndo nyie vibonde,kwenye kundi la simba yeye ndo giant na wengine vibonde ndo huwa wanapanga hivyo
Na ndio maana nikasema ni njia. Mpaka hapo umekubaliana na mimi kuwa kilichotofautisha ni njia. Ila jambo la msingi ni ku focus katika michuano uliyopo na kutobwetekea kuwa nimefikia ngazi ipi bali ifikie hatua timu ijitambe kwa kuchukua kombe. Kwa uwezekaji wa timu za Tanzania hilo linawezekana kwasababu ubora wa vilabu unazidi kuimarika na kwasasa hakuna gap kubwa sana wa ubora wa timu imebaki mapengo madogo madogo ya timu zetu kuweka sawa.
 
changaule umenikumbusha wale wahuni wa Ifakara waliokuwa wanajiita changausile.

Tukubali kwamba Simba imeitangulia mbele kwenye masuala ya mashindano ya kimataifa!!
 
Kwahiyo ni misimu yote ilikuwa inazungumziwa Simba ni mbovu kuliko Yanga au ni msimu huu ndio imeibuka hiyo hoja? Na kama ni misimu yote inazungumzika hivyo, kwanini kwenye uzi wako hukuongelea kama ni hoja ya misimu badala yake ukaongelea kuhusu msimu wa sasa?
Kiufundi kama we ni kocha unafikiria ssc Ina udhaifu Gani???
 
Kiufundi kama we ni kocha unafikiria ssc Ina udhaifu Gani???
1) umri wa wachezaji
2) wachezaji kutumika sana, wamechoka
3) kufanya mabadiliko ya kocha katikati kumeathiri.
Ile safari ya Dubai ilikuwa sio ya lazima ilipaswa wachezaji wapate mapumziko walau ya wiki mbili au tatu lakini wameenda kuanza na upya program ya mazoezi na kucheza mechi mfululizo hadi sasa na ukiangalia squad ya Simba hakuna machagua mengi ya wachezaji wakuingia kwenye kikosi cha kwanza. Hivyo ina mlazimu kocha kuwapanga hao hao.

Hizo sababu zote juu inaifanya Simba kutokuwa na muendelelezo mzuri wa mchezo. Leo atacheza vizuri lakini kesho watacheza vibaya.

Haya ni maoni yangu kila mtu ana mtazamo wake
 
Mnaiona kama vile Simba haina fowadi wa kueleweka, lakini ndiyo inayoongoza kwa kufunga magoli mengi kwenye Ligi kuu Tanzania. Mnaiona simba kama vile ni timu dhaifu lakini Simba na Yanga zote zilikuwa kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika, Yanga ikashindwa kufuzu hatua ya Makundi, Simba ikafuzu.

Leo Yanga iko kwenye Kombe la Shirikisho wanajisahaulisha kwamba kabla ya kwenda huko na wenyewe pia walikuwa kwenye mashindano ya Klabu Bingwa Afrika wakatolewa. Hivi inakuwaje timu dhaifu ya Simba inaendelea kuwemo kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika wakati timu Imara ya Yanga ilitolewa!!??

Bidii kubwa mliyonayo wanayanga, ombeni pia mjaliwe na nasibu ya kufanikiwa, la sivyo kila siku mtaumwa na mafanikio ya Simba mnaowaona ni timu dhaifu lakini wamejaaliwa sudi njema!!
Nyie mna kapu la magoli, sisi tuna kapu la points
 
changaule umenikumbusha wale wahuni wa Ifakara waliokuwa wanajiita changausile.

Tukubali kwamba Simba imeitangulia mbele kwenye masuala ya mashindano ya kimataifa!!
Kwani hoja yako ni kutangulia mbele kwa Simba au Simba kushuka kiwango kwa msimu huu? Embu nikumbushe ni lini kwanzia Mo awe mwekezaji Simba, ni lini Simba imefungwa goli tatu kwa bila kwa Mkapa? ni lini Simba wameshinda ushindi kwa Mkapa lakini wanaomba mpira uishe kutokana na presha ya wapinzani? Mashabiki wa Simba walikuwa wana enjoy kutazama mpira unaochezwa na timu yao huku wapinzani wakinyanyasika. Ukiachana na makosa ya kujiamini yaliyofanywa dhidi ya Galaxy na UD Songo, Simba kanyanyasa sana wapinzani pale kwa Mkapa hadi mashabiki wakiombea burudani iendelee refa aongeze hata dakika 45 zingine baada ya kuishia 90.

Simba ameshuka kwa sasa hilo lipo wazi hata kama utaamua kujificha kwenye hoja ya kuendelea na mashindano lakini inaendelea mashinda ya klabu bingwa lakini yupo hapa kwasababu ya aina ya wapinzani aliyokutana nao.
 
Simba ameshuka kwa sasa hilo lipo wazi hata kama utaamua kujificha kwenye hoja ya kuendelea na mashindano lakini inaendelea mashinda ya klabu bingwa lakini yupo hapa kwasababu ya aina ya wapinzani aliyokutana nao.
Kwa nini watu huwa mnaamini kwamba wapinzani wa Simba ni dhaifu!!??
 
Mimi mpaka muda huu ninachofahamu Yanga ndiye Bingwa mtetezi wa Ligi kuu! Na pia atakuwa Bingwa wa AZFC, kwa mara ya pili mfululizo!

Matarajio yangu mpaka sasa; Mfungaji bora atakuwa ni Fiston Mayele! Golikipa bora ni Diarra! Kiungo bora ni Bangala! Kocha bora wa ligi kuu msimu huu ni Profesa Nabi!!

Na wakati timu ikiendelea kung'ara kwenye ligi ya ndani, na Kimatafa pia Yanga ni habari ya mjini. Na hii ni baada ya kumfunga goli 3-1 Tp Mazembe; timu yenye historia kubwa kwenye soka la Afrika.
Mungu awape nini Young Africans, aka Wananchi!!

Hiyo Simba inayofunga magoli mengi; mchezaji wake mwenye magoli mengi ni Moses Phiri (magoli 10)!! Yanga inayofunga magoli machache; mchezaji wake Fiston Kalala Mayele anaongoza kwenye orodha ya wafungaji bora, na magoli yake 15!
 
Back
Top Bottom