Vawulence
JF-Expert Member
- Jan 4, 2009
- 1,930
- 2,118
Niwapongeze Yanga kwa "kuuza" haki zao za matangazo kwa bilioni 41 kwa Azam TV.
Tumeona kwenye mitandao wachambuzi wengi na washabiki wa Yanga wakiidhihaki Simba kuwa ina thamani ya 20B hivyo wamepigwa na Mo.
Wanachofanya ni kuendeshwa na hisia na kutokuona ukweli. Wanakurupuka na kusahau kuwa Simba hawajatangaza kuwa wameza haki zao za matangazo kwa nani na kwa bei gani.
Tumeona Mo Dewji anadhihakiwa bila kuzingatia kanuni za uchumi. Wanasahau kuwa 20B ya leo itakuwa ni maradufu miaka kumi ijayo ilihali wao wataishia kupata 41B miaka 10 ikitimia. Wafanya biashara wenzangu watakubaliana na mimi kuwa kwa miaka 10 mbele 20B ya Simba itakuwa imezalisha sio chini ya 100B ikiwa thamani ya pesa itabaki ilivyo sasa.
Mtu mwenye milioni 2 leo hii anaweza kufanya makubwa ndani ya miaka 10 kuliko anayepata laki 5 kila mwaka na kupata milioni 10 ndani ya miaka 10.
Niwakumbushe tu Yanga kuwa Azam wanamiliki timu yao Azam FC, je, timu hiyo inareflect kile wanachokitarajia wao?
Nirudie tena kuwapongeza Yanga kwa kufungua Milango ya timu kujiongeza thamani lakini wasidhani kuwa wenzao hawana mipango na wao.
Yanga msikurupuke kuwadhihaki wengine.!
Tumeona kwenye mitandao wachambuzi wengi na washabiki wa Yanga wakiidhihaki Simba kuwa ina thamani ya 20B hivyo wamepigwa na Mo.
Wanachofanya ni kuendeshwa na hisia na kutokuona ukweli. Wanakurupuka na kusahau kuwa Simba hawajatangaza kuwa wameza haki zao za matangazo kwa nani na kwa bei gani.
Tumeona Mo Dewji anadhihakiwa bila kuzingatia kanuni za uchumi. Wanasahau kuwa 20B ya leo itakuwa ni maradufu miaka kumi ijayo ilihali wao wataishia kupata 41B miaka 10 ikitimia. Wafanya biashara wenzangu watakubaliana na mimi kuwa kwa miaka 10 mbele 20B ya Simba itakuwa imezalisha sio chini ya 100B ikiwa thamani ya pesa itabaki ilivyo sasa.
Mtu mwenye milioni 2 leo hii anaweza kufanya makubwa ndani ya miaka 10 kuliko anayepata laki 5 kila mwaka na kupata milioni 10 ndani ya miaka 10.
Niwakumbushe tu Yanga kuwa Azam wanamiliki timu yao Azam FC, je, timu hiyo inareflect kile wanachokitarajia wao?
Nirudie tena kuwapongeza Yanga kwa kufungua Milango ya timu kujiongeza thamani lakini wasidhani kuwa wenzao hawana mipango na wao.
Yanga msikurupuke kuwadhihaki wengine.!