Yanga nafasi mmetengeneza lakini umakini umewaangusha

Yanga nafasi mmetengeneza lakini umakini umewaangusha

Mtanzanias

JF-Expert Member
Joined
Jul 30, 2021
Posts
1,747
Reaction score
3,725
Nitawalaumu kwa umakini mdogo mlioonyesha leo kufumania nyavu, nafasi 4 za wazi zingetosha kuwafanya muondoke na ushindi Leo hii, huwezi kupoteza nafasi kama hizo halafu ukategemea eti usonge mbele kwenye michuano mikubwa Kama hii, ukichezea nafasi basi ujue utaadhibiwa tu, pia sikuona mantiki ya kocha kumpeleka nje Makambo na kumuacha Mukoko ndani, ambae eneo lake na Mauya lilikuwa dhaifu sana.

Palikuwepo na haja ya kumuingiza Bangala kuituliza safu ya kiungo cha ukabaji, yote kwa yote nafikiri kocha amepata kipimo sahihi kinachomuonyesha ni kitu gani anatakiwa afanye kwenye mechi ya marudiano, hakuna kinachoshindikana Kama wamepata matokeo hapa basi hata yanga wanao uwezo wa kupata matokeo Nigeria pia, kilichopo ni kujipanga ipasavyo, makosa ya umakini na upangaji wa kikosi vinatakiwa kuchukuliwa kwa umakini mkubwa, kila la kheri!
 
Yanga wanafeli sana kwa mtindo huu mashindano ya CAF watateseka
Feisal kashindwa kuonyesha uwezo anapaisha karibu na goli wakati pale ni kutulia tu na kuweka mpira kambani
Tutashuhudia mengi san san kuhusu yanga
Return of the looser, what a shame!!
 
Yanga wana bahati sana, walitakiwa wafe 3 bila.

Vipi watangazaji na wachambuzi (takataka) mlio waajiri kuwatetea redioni, wameshindwa kuwatetea kwa wapopo?
 
Yanga wametengeneza nafasi ipi ya maana.!? Zaidi ya ile ya Fei Toto aliyopaisha....

Wakulaumiwa Rivers.... Wametucheleweshea sherehe.... Rivers wangekuwa makini Ilikuwa ni 4 kavu.....
Nafasi ya Makambo na Mauya hazikuwa nafasi za kufunga? Au wewe umeangalia mechi yako tofauti, kwa mchezaji makini zile zilikuwa ni goli safi kabisa
 
Mimi ni Yangaaaaaaa
Screenshot_20210913-012122.jpg
 
Nafasi ya Makambo na Mauya hazikuwa nafasi za kufunga? Au wewe umeangalia mechi yako tofauti, kwa mchezaji makini zile zilikuwa ni goli safi kabisa
Siyo kukosa umakini, ni uwezo wao. Huyu Makambo bado yuko vilevile alivyokuwa
 
Nafasi ya Makambo na Mauya hazikuwa nafasi za kufunga? Au wewe umeangalia mechi yako tofauti, kwa mchezaji makini zile zilikuwa ni goli safi kabisa
Kama kila mpira ukikaribia gorini kwako wewe unaita ni nafasi ya wazi kumbe basi kila siku timu zingekuwa zinafungana hata 20 kwa 20. Clear chance hapo ni ile ya yule mpemba pekee.
 
Hii mech kwanafasi tullizo kosa, sio tu hatukustahili kufungwa Ila hatukustahili ata kutoa sare
 
Back
Top Bottom