Yanga sc kumsajili Jonas Mkude ni matumizi mabaya ya fedha

NALIA NGWENA

JF-Expert Member
Joined
Oct 6, 2016
Posts
10,587
Reaction score
13,425
NALIA NGWENA huwa sipendi kupepesa macho katika Jambo la ukweli.

Yanga Sc inaviungo wengi wakabaji na ninadhani kwa pale Yanga ndiyo eneo lenye viungo wengi.
Namba 6,8 Kuna Khalid Aucho, Sureboy, Zawadi Mauya,Yaniki bangala na Yahya Mudathir.

Jonas Mkude kwa asilia ni namba 6 ambapo kwa Yanga Kuna Mudathir, bangala, na nikitazama kiwango Cha Mkude sidhani Kama ataweza kumuweka benchi bangala au Mudathri hata Kama atawekwa namba 8 acheze bado naiona nafasi ya Sure boy mbele ya Jonas Mkude.

Kama hizi tetesi ni kweli Yanga watamsajili Jonas Mkude Basi ni matumizi mabaya ya fedha huo ni ukweli usiopingika.

Usajili wa Jonasi Mkude ni siasa ya mpira tu sidhani Kama ana umuhimu /uhitaji mkubwa katika kikosi Cha Yanga Sc.

Nawasilisha hoja.
 
Wenye timu wanajua mahitaji ya Mkude.
Huenda miongoni mwa hao uliowataja wakaachwa na timu.
 
Si mna faida ya mil. 500
 
haya yawe matumizi mabaya na iwe wamemsajili,inakuhusu nini wewe?
 
Mkude kama ana ndoto za kuwa mto yeyote pale Simba hapo baadae, asiende Yanga.
 
Hata Hamisi Gaga ilikua hivi hivi, lakini alipotua Uto na kukiwasha, Makolo yalipoteana na kulaumiana.
Performance si kipaji pekee, Kuna aina ya kocha ulienae, wachezaji wanaokuzunguuka, aina ya uongozi wa klabu, mazingira nje ya uwanja etc.
 
Hata Hamisi Gaga ilikua hivi hivi, lakini alipotua Uto na kukiwasha, Makolo yalipoteana na kulaumiana.
Performance si kipaji pekee, Kuna aina ya kocha ulienae, wachezaji wanaokuzunguuka, aina ya uongozi wa klabu, mazingira nje ya uwanja etc.
Gaga aliondoka Simba akiwa na kiwango kikubwa
 
Hata Hamisi Gaga ilikua hivi hivi, lakini alipotua Uto na kukiwasha, Makolo yalipoteana na kulaumiana.
Performance si kipaji pekee, Kuna aina ya kocha ulienae, wachezaji wanaokuzunguuka, aina ya uongozi wa klabu, mazingira nje ya uwanja etc.
Hamisi Gaga huwezi kumfananisha na Mkude au Niyonzima aliporudi Yanga.

Gaga alikuwa bado ana kiwango kikubwa mno.

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Y Yanga na Simba sajili zao ni za kukomoana
 
Kwani hizo hela Ni zako. Mpaka zikutie uchungu. Kajifungue,shubamiti!
 
Mkude akiamua kucheza bado yuko vizuri
 
Hata Hamisi Gaga ilikua hivi hivi, lakini alipotua Uto na kukiwasha, Makolo yalipoteana na kulaumiana.
Performance si kipaji pekee, Kuna aina ya kocha ulienae, wachezaji wanaokuzunguuka, aina ya uongozi wa klabu, mazingira nje ya uwanja etc.
Hamis Thobias Gaga hakwenda Yanga kwa kuachwa na simba kwasababu ya kwamba hakuwa na kiwango cha kuchezea simba. Alienda kwa fitina za mpira wa hivi vilabu viwili. Alitoka simba akiwa anakiwasha sana yule jamaa .
 
Acheni ujinga... Yanga inasajili wachezaj wa aina ya mkude ili wawe wanacheza mechi za ndani ambapo wachezaj tegemewa wanawakuwa wamechoka baada ya kucheza mechi nyingi za kimataifa...
Hamjaona msimu huu wachezaj walivyoteseka...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…