Kurunzi
JF-Expert Member
- Jul 31, 2009
- 9,753
- 10,747
Ushindi wa mabao 2-1 walioupata Simba jana dhidi ya Vita Club umewapeleka robo fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika.
Hakika wanastahili pongezi kwa mafanikio hayo
Watani zetu wametufundisha jambo kubwa sana, ili kuweza kufanikiwa tunahitaji uwekezaji wa fedha, akili, muda, hali na mali pasipo kukata tamaa
Kama Simba wangekata tamaa baada ya kupigwa zile dozi za tano tano sidhani kama wangekuwa na ubavu wa kushinda michezo yao miwili waliocheza nyumbani dhidi ya vigogo wa soka Barani Afrika.
Lakini pia nyuma ya mafanikio hayo yupo mwekezaji wao Mohammed Dewji 'Mo' ambaye alimwaga fedha za kutosha kutengeneza kikosi ambacho leo kimewafanya waweze kutembea kifua mbele.
Simba ndio klabu pekee kutoka ukanda wa Afrika Mashariki na Kati kutinga hatua ya robo fainali ya michuano hiyo ya ligi ya mabingwa.
Wana Yanga yatupasa kupambana juu chini kuhakikisha nasi tunafanya mabadiliko katika timu yetu ili tuweze kuwavutia wawekezaji walete fedha.
Mpango huu wa kuchangia uliopendekezwa na kocha Mwinyi Zahera sio wa kudumu, utaisaidia Yanga kusimama wakati ikijiweka sawa.
Mabadiliko ya mfumo wa uendeshaji ndio kila kitu, kwani mabadiliko waliyofanya Simba tumeona jinsi yalivyokuwa na faida kwao.
Uwekezaji aliouweka Mo katika kipindi cha misimu miwili kwenye klabu ya Simba umekuwa na faida kubwa kwake na kwa Simba pia.
Kwa kutinga hatua ya robo fainali tu Simba itavuna zaidi ya Bil 1.5 fedha ambazo ni zaidi ya fedha walizotumia kukijenga kikosi chao(bil 1.3)
Ukiongeza na fedha walizovuna kupitia mashabiki ambao waliujaza uwanja wa Taifa katika michezo yote mitatu waliocheza jijini Dar es salaam pamoja na mauzo ya jezi, timu hiyo itakuwa imetengeneza fedha nyingi sana.
Simba wametuonyesha kumbe haya yote yanawezekana, ukijipanga vizuri na ukafanya uhamasishaji wa kutosha unaweza kufanya mambo makubwa kuliko wengi tulivyokariri.
Nani alitegemea kama Simba itaweza kuifunga Al Ahly, mabingwa mara nane barani Afrika? Al Ahly ambayo ilicheza fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika msimu uliopita.
Nani alidhani kama Simba itapata ushindi dhidi ya Vita jana? Hawa Vita walicheza fainali ya kombe la shirikisho msimu uliopita.
Simba haikupewa nafasi ya kupenya katika kundi D lililozijumuisha JS Saoura, Al Ahly na Vita lakini wamepita.
Hivi kuna atakayeshangaa tena kama Simba itatwaa ubingwa wa Afrika? kwani hatua waliyofikia lolote linaweza kutokea.
Jambo la muhimu kwa Wana Yanga ni kupata somo kutokana na mafanikio haya. Kama hatua hazitachukuliwa, Yanga haiwezi kushindana na Simba katika nyanja zote.
Ni wazi msimu ujao huenda ukawa mgumu zaidi kupambana na Simba kwani watakuwa bora mara dufu kuliko walivyo sasa.
Sababu mpaka hapa walipofikia wameyajua mapungufu yao na tayari wanao ushawishi wa kumsajili mchezaji yeyote wanayemtaka kutokana uwepo wa fedha na mafanikio waliyopata.
Itakuwa muujiza kwa Yanga yetu hii kushindani na wenzetu ambao kimsingi mpaka sasa wameshatuacha mbali sana.
Sent using Jamii Forums mobile app
Hakika wanastahili pongezi kwa mafanikio hayo
Watani zetu wametufundisha jambo kubwa sana, ili kuweza kufanikiwa tunahitaji uwekezaji wa fedha, akili, muda, hali na mali pasipo kukata tamaa
Kama Simba wangekata tamaa baada ya kupigwa zile dozi za tano tano sidhani kama wangekuwa na ubavu wa kushinda michezo yao miwili waliocheza nyumbani dhidi ya vigogo wa soka Barani Afrika.
Lakini pia nyuma ya mafanikio hayo yupo mwekezaji wao Mohammed Dewji 'Mo' ambaye alimwaga fedha za kutosha kutengeneza kikosi ambacho leo kimewafanya waweze kutembea kifua mbele.
Simba ndio klabu pekee kutoka ukanda wa Afrika Mashariki na Kati kutinga hatua ya robo fainali ya michuano hiyo ya ligi ya mabingwa.
Wana Yanga yatupasa kupambana juu chini kuhakikisha nasi tunafanya mabadiliko katika timu yetu ili tuweze kuwavutia wawekezaji walete fedha.
Mpango huu wa kuchangia uliopendekezwa na kocha Mwinyi Zahera sio wa kudumu, utaisaidia Yanga kusimama wakati ikijiweka sawa.
Mabadiliko ya mfumo wa uendeshaji ndio kila kitu, kwani mabadiliko waliyofanya Simba tumeona jinsi yalivyokuwa na faida kwao.
Uwekezaji aliouweka Mo katika kipindi cha misimu miwili kwenye klabu ya Simba umekuwa na faida kubwa kwake na kwa Simba pia.
Kwa kutinga hatua ya robo fainali tu Simba itavuna zaidi ya Bil 1.5 fedha ambazo ni zaidi ya fedha walizotumia kukijenga kikosi chao(bil 1.3)
Ukiongeza na fedha walizovuna kupitia mashabiki ambao waliujaza uwanja wa Taifa katika michezo yote mitatu waliocheza jijini Dar es salaam pamoja na mauzo ya jezi, timu hiyo itakuwa imetengeneza fedha nyingi sana.
Simba wametuonyesha kumbe haya yote yanawezekana, ukijipanga vizuri na ukafanya uhamasishaji wa kutosha unaweza kufanya mambo makubwa kuliko wengi tulivyokariri.
Nani alitegemea kama Simba itaweza kuifunga Al Ahly, mabingwa mara nane barani Afrika? Al Ahly ambayo ilicheza fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika msimu uliopita.
Nani alidhani kama Simba itapata ushindi dhidi ya Vita jana? Hawa Vita walicheza fainali ya kombe la shirikisho msimu uliopita.
Simba haikupewa nafasi ya kupenya katika kundi D lililozijumuisha JS Saoura, Al Ahly na Vita lakini wamepita.
Hivi kuna atakayeshangaa tena kama Simba itatwaa ubingwa wa Afrika? kwani hatua waliyofikia lolote linaweza kutokea.
Jambo la muhimu kwa Wana Yanga ni kupata somo kutokana na mafanikio haya. Kama hatua hazitachukuliwa, Yanga haiwezi kushindana na Simba katika nyanja zote.
Ni wazi msimu ujao huenda ukawa mgumu zaidi kupambana na Simba kwani watakuwa bora mara dufu kuliko walivyo sasa.
Sababu mpaka hapa walipofikia wameyajua mapungufu yao na tayari wanao ushawishi wa kumsajili mchezaji yeyote wanayemtaka kutokana uwepo wa fedha na mafanikio waliyopata.
Itakuwa muujiza kwa Yanga yetu hii kushindani na wenzetu ambao kimsingi mpaka sasa wameshatuacha mbali sana.
Sent using Jamii Forums mobile app