Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 2,060
- 5,648
Kikosi cha Yanga kimeondoka leo Jumanne Desemba 3, 2024 kuelekea Algeria kwa ajili ya kuivaa MC Alger katika mchezo wa kundi A michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika.
Yanga inaenda kwenye mchezo ikiwa na kumbukumbu mbaya ya kupoteza mchezo wa kwanza dhidi ya Al Hilal nyumbani lakini wakijivunia mastaa wao watano waliokuwa majeruhiwa kurejea.
Mastaa hao ni Dickson Job, Khalid Aucho, Chadrack Boka, Clement Mzize na Aziz Andambwile.
Taarifa za ndani zinasema tayari Hafidhi Saleh ambaye ni mratibu wa timu amewasili Algeria akiwa na Mkurugenzi wa Mashindano wa klabu hiyo, Ibrahim Mohamed kuweka mambo sawa.
Mchezo huo unatarajiwa kuchezwa Desemba 7, mwaka huu katika Uwanja wa Ali La Pointe saa 4:00 za usiku.
Taarifa za ndani zinasema tayari Hafidhi Saleh ambaye ni mratibu wa timu amewasili Algeria akiwa na Mkurugenzi wa Mashindano wa klabu hiyo, Ibrahim Mohamed kuweka mambo sawa.
Mchezo huo unatarajiwa kuchezwa Desemba 7, mwaka huu katika Uwanja wa Ali La Pointe saa 4:00 za usiku.