Yanga yawafuata Waarabu ikiwa fulu mkoko

Yanga yawafuata Waarabu ikiwa fulu mkoko

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Kikosi cha Yanga kimeondoka leo Jumanne Desemba 3, 2024 kuelekea Algeria kwa ajili ya kuivaa MC Alger katika mchezo wa kundi A michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

1733229104472.png
Yanga inaenda kwenye mchezo ikiwa na kumbukumbu mbaya ya kupoteza mchezo wa kwanza dhidi ya Al Hilal nyumbani lakini wakijivunia mastaa wao watano waliokuwa majeruhiwa kurejea.
Mastaa hao ni Dickson Job, Khalid Aucho, Chadrack Boka, Clement Mzize na Aziz Andambwile.

Taarifa za ndani zinasema tayari Hafidhi Saleh ambaye ni mratibu wa timu amewasili Algeria akiwa na Mkurugenzi wa Mashindano wa klabu hiyo, Ibrahim Mohamed kuweka mambo sawa.

Mchezo huo unatarajiwa kuchezwa Desemba 7, mwaka huu katika Uwanja wa Ali La Pointe saa 4:00 za usiku.

1733229133620.png
 
Yanga na full mkoko havitakiwi kutajwa katika sentensi moja.

Kuweni wazalendo msimwage yale mambo yenu airport ya Dar au ya Algeria ili kuwadhuru wachezaji wa Simba. Ninachojua ni timu moja tu ya TZ itashinda huko Algeria weekend hii na timu hiyo haivai rangi ya majani kibichi.
 
Back
Top Bottom