Yapi ni Mavazi sahihi kwa Mwanaume kwaajili ya Mtoko wa kukutana na Mwanamke kwa mra ya kwanza?

Kama unapenda perfume tafuta za kupoa harufu isiwe kali au bodyspray harufu iwe ya kupoa na ukijispray unatakiwa uspray kidogo sana ili harufu isikere na mtu awe anaisikia kwa mbali sana , usisahau na deodorant kufanya kwapa ziwe kavu sio unamkumbatia tayari kwapa limeloa lote sio sawa
 
Sneakers, Jeans and T-shirt.
Makobazi na moka au buti No Way!
 
Vaa suruali kama kadeti iwe safi isiwe imepauka kama imeanikwa kweny paa la nyumba kama ni jeans yenye rangi iliyotulia sijui imechanika au Ina mipauko .


Kama kadeti Vaa na shati na kama jeans tafuta fulana imetulia isiwe na rangi mbili na zaidi kama mavi ya kuku.

Perfume nzuri achana na hizi yeboyebo chukua unisex PEGASUS
 
Nyoa nywele zako vizuri zilingane usiweke mtindo
Vaa suruali cadet
Shati la mikono mirefu litapendeza zadi liwe jeupeeee
Rangi ya mkanda wa suruali iendane na rangi ya kiatu

Saa nzuri mkononi
Nukia vizuri
Ukikutana nae ongea vitu vya maana

Epuka kumuita majina ya hovyo kama oya n.k
 
Inaonekana bado amateur kwenye hii kada..hata hivyo usijali fanyia kazi mawazo ya wadau hapo juu.
 

T-Shirt na Jeans ni Universal Code..!!
Chini viatu simple visiwe vya kiofisi.

#YNWA
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…