Yawezekana kabisa Tanzania inaongozwa na watu ambao hawajawahi kabisa hata kuisoma kabisa!

Yawezekana kabisa Tanzania inaongozwa na watu ambao hawajawahi kabisa hata kuisoma kabisa!

Nyani Ngabu

Platinum Member
Joined
May 15, 2006
Posts
94,296
Reaction score
122,540
Unapoona viongozi wa nchi wanatoa kauli kama ‘Rais Samia ameruhusu maandamano’ au ‘Rais Samia ameruhusu vyama vya upinzani vifanye mikutano ya kisiasa’, wewe Mtanzania uliye mwerevu na uliye na ufahamu wa msingi wa elimu ya uraia, unajisikiaje? Unaonaje?

Huoni kwamba, ama tunaongozwa na viongozi wajinga wasio na ufahamu hata ule wa msingi tu wa elimu ya uraia na jinsi ambavyo nchi inapaswa kuongozwa kwa kufuata katiba ya nchi, au, tunaongozwa na viongozi wasiojali kabisa kufuata katiba ya nchi na sheria zingine za nchi?

Lipi ni lipi hapo?

This country is a hot steaming mess!
 
Lipi ni lipi hapo?
Chawa ni mdudu?
Screenshot_20240307-214527.png
 
Ndio maana miaka 60+ya Uhuru tumeshindwa kusolve hata tatizo la maji na umeme.!!

Position nyingi zimeshikwa na watu ambao uwezo wao kuongoza ni mdogo mno

Kiufupi hatuna viongozi tuna watawala wenye mawazo ya kikoloni bado.

Siku nchi hii ikipata kiongozi ndio mtajua kwamba wote waliopita walikuwa madishi tu.
 
Ni kweli mtoa mada ILA bila push back ,hii status ago itaendelea,maana hizi royal families zimeshaweka mikakati ya kusomesha watoto wao kwenye shule zinazotoa elimu bora ,ili waendelee kutawala kizazi hiki cha poor of the poorest cha hapa lingusenguse, tusilalame ni kufanya push back
 
Huenda wale watu wa zama za mawe wakawa bora zaidi kuliko viumbe tulivyo navyo hapa bongoland...kwa nchi za wenzetu kauli kama hiyo kesho unakabidhi ofisi...
Tuna watawala wenye akili ndogo sana, ni zaidi ya ugonjwa wa akili.
 
Ndio maana miaka 60+ya Uhuru tumeshindwa kusolve hata tatizo la maji na umeme.!!

Position nyingi zimeshikwa na watu ambao uwezo wao kuongoza ni mdogo mno

Kiufupi hatuna viongozi tuna watawala wenye mawazo ya kikoloni bado.

Siku nchi hii ikipata kiongozi ndio mtajua kwamba wote waliopita walikuwa madishi tu.
Facts!
 
Unapoona viongozi wa nchi wanatoa kauli kama ‘Rais Samia ameruhusu maandamano’ au ‘Rais Samia ameruhusu vyama vya upinzani vifanye mikutano ya kisiasa’, wewe Mtanzania uliye mwerevu na uliye na ufahamu wa msingi wa elimu ya uraia, unajisikiaje? Unaonaje?

Huoni kwamba, ama tunaongozwa na viongozi wajinga wasio na ufahamu hata ule wa msingi tu wa elimu ya uraia na jinsi ambavyo nchi inapaswa kuongozwa kwa kufuata katiba ya nchi, au, tunaongozwa na viongozi wasiojali kabisa kufuata katiba ya nchi na sheria zingine za nchi?

Lipi ni lipi hapo?

This country is a hot steaming mess!
Watz wengi Elimu yao ni mbovu mno mtu anasema Pesa za rais zimekuja halafu kuna watu na mindevu yao inapiga makofi.

Elimu,,,,Elimu,,,,Elimu,,,Elimu,,,,,Elimu.
 
Back
Top Bottom