Yesu hakupigiliwa misumari kwenye viganja vya mikono!

Yesu hakupigiliwa misumari kwenye viganja vya mikono!

Wachoraji wa picha za Yesu akiwa msalabani mnatakiwa kuelewa historia ya ile adhabu ya kifo enzi zile. Misumari ilikuwa inapigwa hapo mahali unapovaa saa ya mkononi siyo katikatiya kiganja kama picha nyingi zinavyoonyesha.

Sababu ni kwamba wangepiga misumari katikati ya kiganja na kumning'iniza mtuhumiwa msalabani basi misuli ya viganja haingeweza kuhimili uzito wa mwili na viganja vingechanika na msulibiwa kuanguka chini.

Upo ushahidi wa kutosha wa sayansi ya manbo ya kale uliogundua mifupa ya waliosulibiwa ikonyesha mahali misumari ilipopigiliwa.

Ndugu zetu Mashahidi wa Yehova huwa wanachora kwa usahihi japo kuna ubishi kama msalaba ulikuwa ni nguzo moja au mbili. Wachoraji wetu rekebisheni hilo tafadhali.
Sio hayo tu bali pia Yesu hakuchomwa mkuki ubavu wa kushoto, alichomwa ubavu wa kulia na mkuki kutokezea ubavu wa kushoto.
 
Allah katika Quran anahidi kuwa atamuua Yesu kwa natural death then atamfufua baada ya siku 3 na ndivyo ilivyo.

naomba aya ya katika quran kihusu hayo maneno yako?☝️☝️
اِذۡ قَالَ اللّٰہُ یٰعِیۡسٰۤی اِنِّیۡ مُتَوَفِّیۡکَ وَ رَافِعُکَ اِلَیَّ وَ مُطَہِّرُکَ مِنَ الَّذِیۡنَ کَفَرُوۡا وَ جَاعِلُ الَّذِیۡنَ اتَّبَعُوۡکَ فَوۡقَ الَّذِیۡنَ کَفَرُوۡۤا اِلٰی یَوۡمِ الۡقِیٰمَۃِ ۚ ثُمَّ اِلَیَّ مَرۡجِعُکُمۡ فَاَحۡکُمُ بَیۡنَکُمۡ فِیۡمَا کُنۡتُمۡ فِیۡہِ تَخۡتَلِفُوۡنَ

“And when Allah said, ‘O Jesus, I will cause thee to die a natural death and will exalt thee to Myself, and will clear from thee charges of those who disbelieve, and will place those who follow thee above those who disbelieve, until the Day of Resurrection; then to Me shall be your return, and I will judge between you concerning that wherein you differ.’” (Surah al-e-Imran, Ch3: V.56)
 
Madhehebu yote chanzo ni mayahudi.

Mtume hakuwa na dhehebu na hivyo waislam halisi hatuna dhehebu.

Madhehebu nayo hawana yakini.

Kama ilivyokuwa kwa Socrates, yesu nae alikuja kupambana. Na dola ya rumi. Dr Paul akafanya mambo yake.

Kwa kuwa alikuwa ni mwanafalsafa nguli baada ya Socrates, plato, Aristotle.

Ndio wao pekee wenye influence kubwa duniani. Socrates alikunywa sumu kama hukumu kali ya kifo kwa wakati huo. Ktk kipindi cha yesu, kusulubiwa ilikuwa ni adhabu ya laana kwa itikadi ya warumi.

Kumtetea yesu kuwa akiuwawa ni kumtoa ktk adhabu ya laana. Na Quran inamteta hawakumuuwa.

Na hawakumuuwa kwasasa kabla hajaanza mateso aliniomba Allah, au Elio kwa kiibrania. Elio Elio mbona umeniacha.

wakristo wote nchini kama kweli wanataka kuwa ni wafuasi wa kweli wa yesu, basi sunna ni kupigania utawala wa wahalifu. Na ikibidi wakubali kusulubiwa kama ilivyotokea kwa waislam.

Kuanzia uamsho, hadi mzee medi.

Wamesulubiwa.

Je ninyi mko tayari kumfata yesu kwa ku juu ubali kusulubiswa na mapilato wa Enzi hizi.

Naamini damu yenu itakuwa ukombozi. Lkn yale mafundisho ya paulo kuwa yesu atakujomboa okiwa unaimbia na kumtaja saba mchana wa jua kali na maspika ktk maeneo ya watu wenye pesa. Tujue tumeingizwa cha kike.

Kuwa fanya zinaa, kunywa pope beana yesu keshabena sambi sako. Tutafakari ukya.

Kama ilivyo kwa muhamadu alitokea akapinga watawala, akashinda, waktristo kuweni jama yesu na Muhamad. Wote mujipambanue kuwa ni chadema nasi tutakuja kuwaunga mkono.

Yalikuwa ni mazungumzo baada ya kifalsafa.

Bt Take it easy
NIMEKUOMBA VERSE 1 TU TOKA KWENYE KURAN INAYOSEMA YESU HAKUFA BADALA YAKE UMEAMUA KUJA MASHAHIRI MENGI AMBAYO HAYANA KICHWA WALA MIGUU.
ALLAH ANASEMA ALIMUUA YESU SIKU 3,WEWE AMBAYE UNASEMA HAKUFA ILO UMELITOA WAPI?.
umeenda mbali hadi na kunuu Bible kujustify uongo wako.
okay, Yesu alimuomba Baba yake amuondolee kikombe cha mateso.so tukitaka kujua ikiwa baba yake alikiondoa ama hakukiondoa kikombe ni lazima tumuulize yesu(mwombaji) sio muhamad ambaye hamjui yesu.

katika Yohan 18:11
Peter anamkata mtu sikio, na Yesu anamwambia hivi peter:- Basi Yesu akamwambia Petro, Rudisha upanga alani mwake; JE! KIKOMBE ALICHONIPA BABA, MIMI NISIKINYWEE?.

kwa hiyo habari ya kuwa Mungu alimwondolea yesu kikombe cha Mauti ni uwongo.
 
(Mathayo 28:11-15)

Ripoti ya walinzi kuhusu kufufuka Kwa Yesu ndio ilileta mambo haya yote.

Wengine wakasema hakusulubiwa, mwingine asema misumari haikipigwa kwenye viganja vya mikono, wengine hakufufuka, wengine alipotea nk nk.

Ukiwauliza wapi yalipo mabaki ya MWILI wa YESU, hutopata majibu.

Muhimu watu wote wenye dini, wa Pagani, Islam Kwa wakristo wajue kuwa bila kumwamini Yesu aliyezaliwa, akafa, akazikwa na kufufuka, wasahau kuhusu mbingu.
 
Biblia waongo ila wewe uliyezaliwa juzi ndio mkweli?

Biblia haihitaji hata siku.moja tafsiri kutoka mavitabu mengine ya kuokoteza barabarani

Ikiandika msalaba ina maana ya msalaba sio gogo lililosimama wima
Alwambwa mtini, siyo msalabani.

Limsalaba walikuja kulibuni siku za hivi karibuni.
 
Text ya Injili inasema "in the hands." Ya kwako inasema matobo yalikuwa wapi?
Ushahidi wa kiakiolojia unaonyeshs " in the wrist". Kumbuka biblia imeandikwa kwenye zile lugha mama na tafsiri nyingi ni potofu. Ni kama walivyofasiri maneno ya Yesu kwamba mtu ana ruhusa ya kumuacha mke wake kwa sababu yq UZINZI. Walikosa neno sahihi wakaweka neno lisiloakisi maana halisi ya alichosema Yesu!
 
Sio hayo tu bali pia Yesu hakuchomwa mkuki ubavu wa kushoto, alichomwa ubavu wa kulia na mkuki kutokezea ubavu wa kushoto.
Kwa ushahidi upi ila nami nifanye utafiti? Maana lengo la yule askari ilikuwa kuhakiki kama damu na maji vimetengana ili kuthibitisha Yesu amekufa. Vinginevyo wamvunje miguu ili afe.
 
Kwa ushahidi upi ila nami nifanye utafiti? Maana lengo la yule askari ilikuwa kuhakiki kama damu na maji vimetengana ili kuthibitisha Yesu amekufa. Vinginevyo wamvunje miguu ili afe.
Askari wa Kirumi siku zote alifundishwa kumchoma mkuki adui kupitia upande wa kulia kwani upande wa kushoto askari yeyote alifundishwa kuulinda kwa ngao, hivyo ujanja ilikuwa kusukumiza mkuki kupitia upande usiolindwa sana, ndio ule upande wa kulia na kuhakikisha mkuki unakwenda hadi upande wa kushoto kwenye moyo. Japo Yesu hakuwa anajilinda kwa ngao lakini mwiko au fundisho hilo lilitumika hata kwa Yesu Msalabani. Ni ajabu, sio?
 
Askari wa Kirumi siku zote alifundishwa kumchoma mkuki adui kupitia upande wa kulia kwani upande wa kushoto askari yeyote alifundishwa kuulinda kwa ngao, hivyo ujanja ilikuwa kusukumiza mkuki kupitia upande usiolindwa sana, ndio ule upande wa kulia na kuhakikisha mkuki unakwenda hadi upande wa kushoto kwenye moyo. Japo Yesu hakuwa anajilinda kwa ngao lakini mwiko au fundisho hilo lilitumika hata kwa Yesu Msalabani. Ni ajabu, sio?
Asante. Nitatafiti nami kujiridhisha maana askari yule hakuwa anapambana na adui bali alitaka kuthibitisha kama mtuhumiwa amekufa kweli. Thanks for the hint anyway!
 
Wachoraji wa picha za Yesu akiwa msalabani mnatakiwa kuelewa historia ya ile adhabu ya kifo enzi zile. Misumari ilikuwa inapigwa hapo mahali unapovaa saa ya mkononi siyo katikatiya kiganja kama picha nyingi zinavyoonyesha.

Sababu ni kwamba wangepiga misumari katikati ya kiganja na kumning'iniza mtuhumiwa msalabani basi misuli ya viganja haingeweza kuhimili uzito wa mwili na viganja vingechanika na msulibiwa kuanguka chini.

Upo ushahidi wa kutosha wa sayansi ya manbo ya kale uliogundua mifupa ya waliosulibiwa ikonyesha mahali misumari ilipopigiliwa.

Ndugu zetu Mashahidi wa Yehova huwa wanachora kwa usahihi japo kuna ubishi kama msalaba ulikuwa ni nguzo moja au mbili. Wachoraji wetu rekebisheni hilo tafadhali.
Kama concern yako ni uzito wa mwili ungepelekea viganja kuchanika nikutoe hofu ya kuwa uzito wa mwili haukutegemea kubebwa na misumari ambayo ilipigwa kwenye mikono bali uzito wote ulikuwa unabebwa na kigongo ambacho huwa kinakuwa chini ya nyayo pale miguu inapokutanishwa.
Kama umewahi kuwaona wale ngongoti wa sanaa za maonesho vile wanaweka vibao chini ya nyayo zao ndiyo hivyo vilitumika kushikilia mwili wa aliye msalabani na ile misumari mikononi ilipigwa kushikilia tu mikono na sio kubeba uzito wa jumla wa mwili wa aliyetundikwa msalabani
 
Back
Top Bottom