Baada ya kuanza majukumu yake kwenye kikosi cha Yanga, kocha Charles Mkwasa amewataka wachezaji kutambua ukubwa na thamani ya kucheza Yanga
Mkwasa amewahakikishia wachezaji kuwa kama watajituma na kujitolea kwa moyo mmoja, hakuna sababu ya timu kutopata matokeo mazuri "Niwahakikishie wote mlisajiliwa na Yanga kwa sababu mlionyesha ubora na kuwa na sifa ya kuichezea timu hii. Jukumu langu mimi ni kuwasaidia ili muweze kutimiza malengo ya timu," amesema "Fahamuni mpo hapa kuipigania klabu hii na kubeba vikombe, hilo ndio lengo kuu kwa kila mchezaji anayeitumikia klabu hii" "Tunapaswa kuishi katika utamaduni huu na ili kutimiza dhamira hii ni lazima tuanze kushinda michezo yetu" "Tutakaposhinda kila kitu kitarejea katika hali yake, uwanja utajaa na furaha kwa mashabiki itarejea"
Mkwasa ataiongoza Yanga kwenye mchezo wake wa kwanza kesho dhidi ya Ndanda Fc ambao utapigwa uwanja wa Nangwanda Sijaona mkoani Mtwara
Kikosi cha Yanga kilitua Mtwara jana, leo wanatarajiwa kufanya mazoezi ya mwisho katika uwanja huo