Mzuwanda ''alijifanya'' ameokoka na alikuwa anasali kanisa la mama mchungaji, Dr, Mheshimiwa ,pale Mlima wa moto,pale kanisani alikuwa anakula hindi teke moja la Kisukuma, hilo hindi lilikuwa la kijana mmoja,baadae akaondoka na kuanzisha kanisa lake pale kwenye kituo chake cha mafuta Baruti.Unaambiwa hilo hindi teke lilianza kumfanyia vituko kijana wake baada ya kuwezeshwa na baba ,lakini hali ikabumbuluka na kijana akaamua aangalie hamsini zake na kama haitoshi mzee nae akamtosa baada ya hindi kuanza kuliwa na viserengeti/vimario baada ya hilo hindi teke kuwa na mkwanja wa kufa mtu ambao alikuwa akinufaishwa na mzee,habari zikamfikia mzee na mzee akakata kamba,hindi teke nalo likaanza kunyauku baada ya kukosa mshiko wa baba ,mwishowe hadi hela ya pango akawa hana na amebaki leo kalala Sinza ,kesho Kimara ,keshokutwa Mbagala hata daladala alizozisahau kuzipanda nazo zinamshinda.Hindi teke limekuwa choka mbaya na hata Serengeti nao wameota mbawa.