Yuko wapi producer Ambangile Mbwanji maarufu kama Producer Amba?


Ndipo hapa tunapokosea WaTZ wengi, muziki haulipi basi atumie hiyo fursa ya umaarufu kupitia muziki kufanya mengine yatayomlipa zaidi!!

Mfano! Angetumia jina lake lililojijenga kwenye sanaa yake ya kuzalisha muziki kuhakikisha anauza mikate kwa wingi nchini!! "Mikate ya Amba ndiyo habari ya mjini" nani angeacha?? Ingeweza kumpeleka level nyingine kimaisha!!

Angeweza kabisa, kupata kazi za muda mfupi zinazolipa kama mwenzie Mchagga yule alivyojishikiza kwenye Bongo Star Search na Salama!!

Ni mawazo yangu na akili za pilau la Eid!
 
Achana na marlaw kuna wasanii kama
Yaki
E2k
Roby G
Ibu
Ibra nation
Rohosaba

Walikua wanafanya kazi bure.
Amber amewasaidia wengi sana ndio mana anaanza kufanikwa nnje ya mziki

Kuna mwenzio alikua anashoot video anaitwa mecky kaloka

Yaki ana ngoma moja kali sana!! Siifahamu jina ila ina kasauti ka kutengeneza na computer kwenye chorus
 
Kurekebisha kidogo mkuu.Producer Amba hakuwahi kuja dar kufanya kazi yoyote ya mziki. Kama producer. Amba Aliwahi kusema kuwa hakuna haja ya kuja ama kuhamia dar ili uwe producer mkali. Ila kama unafanya kazi nzuri,basi popote unaweza sikika.hivyo Mkali Amba habari za dar hazikuwahi kuwa katika maisha yake.Vinginevyo Amba alikuwa mkali kuliko neno lenyewe sema wasanii wake visu kama roho saba na Yaki. Waliitosa game mapema nadhani nayo ilidhoofisha morale ya production yake.na sababu nyingine zikapelekea yeye kuachana na music production.
 
Amba bado anafanya production but kwenye upande wa gosper. Anatengeneza sana nyimbo za Ambwene mwasongwe.
 
Yaki ana ngoma moja kali sana!! Siifahamu jina ila ina kasauti ka kutengeneza na computer kwenye chorus

Amba ni producer mkali sana, kila ninapoisikiliza ngoma ya Roho 7-Nakupenda Hiphop nasemaga itabikia kuwa moja namba kwangu kwa flow na midundo. Lakini achana na hiyo kuna ngoma kama Tonight na Wangu ft Ree K Farida alizofanya na Yaki yaani zote ni balaa kwa flow na midundo. Humo utaisikia zile autotunes unazosema... ambazo originally nadhani ni sauti za Farida wa Pesa na upendo wa mama.
 
Okay Ambangile Mbwanji

Mtoto wa mchungaji,

Aliwahi ishi Sweeden wakiwa wadogo, nadhan baba ake alikuwa anasoma,

Studio yake iliitwa AB records huku ikiwarokod wakali wa enz hizo akina YAKI (ambae siku hiz utamuona anashinda sana na project za Masoud kipanya kama Video director) but enz hizo alikuwa ni rapper na dancer mzur sana, Man kichefu, OB na wengine

Studio ya 2D thomas haikuwa hiyo, yeny
 
Studio ya 2D ilikuwa inapatikana Jengo la Motto family, ambako kulikuwa na ofis za country fm,

Humo alikuwepo mtu anaitwa Temmy G,ndo alie mfundisha kaz 2D

Wasanii waliokuwa wanarekod huko ni IBranation,Marlaw,Baraka BuX etc

Kulikuwa na producer mwingine anaitwa Fadhil,wa Father records

Huyu jamaa alikuwa sana anapiga kaz na ManFissa (my best underground rapper of all times)

It was so so so good living in Iringa those days,

You know what it is..
 
Miaka ya 2013-2015 Amba alikuwa Dar

Na studio yake ikawa maeneo ya Ukonga

Nadhan ndiko album ya Ambwene Mwasongwe ilipotengenezwa

By this time Amber alikuwa ameamua kufocus na gospel music tu

Saiv yes yupo Iringa,nasikia ana hyo Bakery na inafanya vyema
 
Mkuu obeid aka OB yuko wapi sikuhizi naikumbuka ngoma yake yake ya songa
 
Siwezi kumzungumzia amba, kiwajihi, but nachoweza kusema jamaa alikuwa producer mzuri sana. Sijawahi kumuona live, ila kupitia kazi ndo nimemfahamu. Ukisikiliza beat zake za kihisia kama zile za roho saba na yaki.....yamkini inaleta ari na hamu ya kuendelea kumsikiliza katika hizi zama.
 
Mkuu mbona nilishawahi sikia alihamia dar na studio yake ilikua majumba sita huko dar?
Sina uhakika wa hili lakini
 
Kipindi fulani alikua anafanya kazi pamoja na Producer KidBway wa Tetemesha Records akitengeneza wimbo kama Disco wa Mr VS.
Kwa sasa nadhani amejikita kwenye kutengeneza nyimbo za Gospel tu kwamfano album yote ya Atosha Kissava "Kila MTU anasema U Mwema" kaitengeza yeye
 
Mkuu hapa nadhani umewapotosha watu....Amba kaenda kaenda Dar kufanya mziki kwa vipindi viwili...kipindi cha kwanza alikuwa chini ya studio ya mtu akakaa huko baadaye akarudi Iringa ndipo akafungua studio ya AB record ambayo ilimilikiwa na Amba pamoja na Ben..baada ya hapo akarudi tena kufanyia shughuri zake Dar ndipo akapotea moja kwamoja karudi kufanya shughuli zake
 
QUOTE="pinno, post: 31721001, member: 120134"]
Studio ya 2D ilikuwa inapatikana Jengo la Motto family, ambako kulikuwa na ofis za country fm,

Humo alikuwepo mtu anaitwa Temmy G,ndo alie mfundisha kaz 2D

Wasanii waliokuwa wanarekod huko ni IBranation,Marlaw,Baraka BuX etc

Kulikuwa na producer mwingine anaitwa Fadhil,wa Father records

Huyu jamaa alikuwa sana anapiga kaz na ManFissa (my best underground rapper of all times)

It was so so so good living in Iringa those days,

You know what it is..
[/QUOTE]
Umemsahau na Marlaw - Bembeleza!!
Bembeleza imetengenezwa studio za Country FM chini ya Toddy thomas na Twmmy G si kwa Amba
 
Basi unamjua
 
Bila kuweka ngoma za Yaki hujautendea haki uzi wako..
 
Man Fissa πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚kitambo sana
Kama sikosei amesoma pommerin secondary enzi hizo ilikua shule ya moto kishenz
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…