Thanks Gagnija and FUGWE,
Kwa Gagnija, ssm imeshahukumiwa kwa matendo yake tayari, ya kukandamiza upinzani, kutenga wanassm wenye moyo wa kitaifa ambao wanaichallenge ssm, na kulea mafisadi ndani ya chama. Tunajaribu kujitafutia ukombozi binafsi ila vikwazo ni vingi sana, na ambavyo vinaletwa na system ya uongozi tulionao. Wote kwenye campaign wanatudanganya sana kwa maneno ya mgongo wa chupa, na watanzania tunakubali, walishajua tu kwa maneno matamu kwa watz hata kama hayatekelezeki basi kura umepata. Huko Tarime kunafuka Moshi sasa, juzi NSSR walivamiwa, sijaelwa Chadema itakuwaje? CUF ndo niko bubu kabisa!! Kwa hapo huoni kuwa ssm kwao ni advantage? Sasa ukombozi binafsi ni upi au ni fujo tuu? Ndiyo maana nimesema upinzani ni tabu kupata madaraka makubwa TZ kwa sasa.
Kwako Fugwe,
Kweli tunao wanamapinduzi na wasiogopa na ssm ni kama chama hakina matatizo kama ulivyosema. Wasiwasi wangu ni kuwa ssm ikishaona hivyo inajaribu kutafuta namna ya kuwanyamazisha wapiganaji kama hao, na si ukashangaa kuona 2010 wanaenguliwa wasigombee. Na kwa sababu ssm inakumbatia mafisadi wanao finance election basi ni heri waondoke hao wapiganaji, na nguvu ya kuwanyamazisha inafadhiliwa na haohao mafisadi. Majority wa ssm ukianzia uvccm na uwt wote wanafadhiliwa na mafisadi, kuna kijana mmoja katika kinyang'aniro cha uvccm majuzi tu RA alimfadhili 20 mil na atahakikisha atapita. Hivyo basi kupata rais au PM mwana mapinduzi toka ssm ni ngumu sana, sana sana ssm kama suala la mtandao na makundi llitaendelea basi litokee kundi lenye nguvu la wapiganaji ndani ya ssm then ssm yenywe ijigawe ssm 1 and ssm2 then wadau tuelismishe umma ubaya wa makundi hayo then tunaweza kung'oa ule upande haswa unatumikia mafisadi. At the same time tusubiri 2010 si wenyewe wamesema watu watenganishe biashara na siasa? Fisadi anaweza kutokuwa kiongozi wa kisiasa au mwenye madaraka but akafinance uchanguzi ili kulinda interest zake na kuwa na power fulani fulani kama afanyavyo RA kwa sasa japo ameshakuwa mpole kidogo. Sasa naomba wale ambao mko karibu na akina Mwakyembe, Kilango Seleli, na wengineo kama hao mpeane mawazo ya kishujaa tuone cha kufanya hata kama haitawezekana 2010 then 2015 tufanikishe. Long live JF.