Kurunzi
JF-Expert Member
- Jul 31, 2009
- 9,753
- 10,747
Tshepo Gumede beki wa Marumo Gallants ambaye Mayele alimfanyia ukatili mkubwa akimuwekea mpira mbele kisha kuanza kumkimbiza na akampita na kuwahi mpira licha ya beki huyo kuwa mbele yake kabla ya kuanza mbio hizo.
Haikuwa kukimbiza pekee Mayele akaenda kutoa pasi ya maana akimlipa Kennedy Musonda ambaye naye alimtengenezea bao la kwanza kisha Mzambia huyo akafunga kikatili bao ambalo liliwapa ushindi Yanga ugenini wakitinga hatua ya Fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika.
Gumede amezungumza na Mwanaspoti jana Jijini hapa akisema bado haamini kama Mayele ana nguvu na kasi za kawaida kwa jinsi alivyomtoka kwenye tukio lile ambapo hakudhani kama anaweza kuwa na mbio za kiasi kile.
Gumede alisema; "Tulikuwa na taarifa za kila aina juu ya ubora wake ndio maana uliona ule mchezo wa kule Tanzania hakufanikiwa kufunga japo alitoa pasi ya bao la pili lakini huku alichofanya bado nakosa majibu sahihi ya ubora wake halisi."
"Tulidhani ana nguvu pekee ndio maana ukaona alipokuwa nyuma yangu nilidhani hataweza kuja kufanya alichofanya lakini kumbe ana kasi kubwa pia, sio rahisi kwa mchezaji mwingine kuwa na kasi ya namna ile.
"Nilitamani kumvuta lakini nikagundua naweza kupewa kadi nyekundu kwa kuwa nilikuwa mtu wa mwisho na alipokaa mbele yangu sikuwa na la kufanya tena,"aliongeza beki huyo aliyegeuka gumzo kwa mashabiki wa Yanga.
Aidha Gumede aliongeza kuwa wala hashangazwi kusikia taarifa kuwa Mayele anaongoza kwa ufungaji kwa ligi ya Tanzania wala Afrika kwa kuwa aina ya mshambuliaji huyo wako wachache duniani.
"Unaona ubora wa Christiano Ronaldo ni kama huyu (Mayele) anajua kufunga na ana kasi, mshambuliaji wa namna hiyo ni rahisi kufanikiwa na kuwa Bora kwa kuwa wanajua kwamba mabeki wengi hawana kasi na huwa tunakutana na wakati mgumu kukabiliana na mshambuliaji wa namna hiyo.
"Kwangu Mimi nawapongeza Yanga kwa kushinda lakini nawaona wanaweza kuwa watu bora kuchukua hili kombe mbele ya USM Alger, tumecheza nao wale tunawajua."
Haikuwa kukimbiza pekee Mayele akaenda kutoa pasi ya maana akimlipa Kennedy Musonda ambaye naye alimtengenezea bao la kwanza kisha Mzambia huyo akafunga kikatili bao ambalo liliwapa ushindi Yanga ugenini wakitinga hatua ya Fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika.
Gumede amezungumza na Mwanaspoti jana Jijini hapa akisema bado haamini kama Mayele ana nguvu na kasi za kawaida kwa jinsi alivyomtoka kwenye tukio lile ambapo hakudhani kama anaweza kuwa na mbio za kiasi kile.
Gumede alisema; "Tulikuwa na taarifa za kila aina juu ya ubora wake ndio maana uliona ule mchezo wa kule Tanzania hakufanikiwa kufunga japo alitoa pasi ya bao la pili lakini huku alichofanya bado nakosa majibu sahihi ya ubora wake halisi."
"Tulidhani ana nguvu pekee ndio maana ukaona alipokuwa nyuma yangu nilidhani hataweza kuja kufanya alichofanya lakini kumbe ana kasi kubwa pia, sio rahisi kwa mchezaji mwingine kuwa na kasi ya namna ile.
"Nilitamani kumvuta lakini nikagundua naweza kupewa kadi nyekundu kwa kuwa nilikuwa mtu wa mwisho na alipokaa mbele yangu sikuwa na la kufanya tena,"aliongeza beki huyo aliyegeuka gumzo kwa mashabiki wa Yanga.
Aidha Gumede aliongeza kuwa wala hashangazwi kusikia taarifa kuwa Mayele anaongoza kwa ufungaji kwa ligi ya Tanzania wala Afrika kwa kuwa aina ya mshambuliaji huyo wako wachache duniani.
"Unaona ubora wa Christiano Ronaldo ni kama huyu (Mayele) anajua kufunga na ana kasi, mshambuliaji wa namna hiyo ni rahisi kufanikiwa na kuwa Bora kwa kuwa wanajua kwamba mabeki wengi hawana kasi na huwa tunakutana na wakati mgumu kukabiliana na mshambuliaji wa namna hiyo.
"Kwangu Mimi nawapongeza Yanga kwa kushinda lakini nawaona wanaweza kuwa watu bora kuchukua hili kombe mbele ya USM Alger, tumecheza nao wale tunawajua."