Yule Mama akaniambia; umekosea kuwahi kuoa. Je, yuko sahihi?

ongea nae vizuri huenda anajua siri mingi za ndoa

hahaaaaa
isijekuwa anataka umpe mkulungeeeee / mkwajuu
 
Miongoni mwa marafiki zangu wanne wamefariki chini ya umri wa miaka 25 mmoja kafariki mwaka jana na watatu mwaka huu, maisha yanachanganya sana Kuna muda unaona ni Bora kuoa utafute hata mtoto mapema Kuna muda unawaza je ikatokea sipo mtt si atateseka sana unaona ni Bora uendelee kwanza kujijenga kiuchumi ili ukioa hata usipo kuwepo familia iwe katka hali nzuri kdogo, lakn mbaya zaid hatuna uhakika kma tutatoboa...
Tomorrow is not promised linalowezekana Leo lisingoje kesho kama una uwezo wa kuoa we oa tu ila kma huna uwezo acha
 
Katika kitu ambacho hakina formula ni ndoa unaweza ukawahi ukapatia na unaweza ukachelewa ukakosea
 


Tena huku kwetu Afrika ndio Kabisa!!

Mambo hayatabiriki hata kidogo,

Nimemuambia hakuna sehemu imeandikwa ikifika umri Fulani kuna fuko la pesa linakusubiri
 
Katika kitu ambacho hakina formula ni ndoa unaweza ukawahi ukapatia na unaweza ukachelewa ukakosea


Umenena.

Unaweza Anza vizuri ukaishia kubaya
wengine wanaanza vibaya wanaishia kuzuri.

Wengine matokeo hubaki Kama yalivyo tangu wanaanza
 
Kuoa/Kuolewa ni kamali kama kama nyingine.
Kuna kula ama kuliwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…