Yupo wapi Askofu Zacharia Kakobe? Hajaonekana tangu Desemba 2021

Ni mtu wa mwanzo kuanzisha haya mauzauza ya unabii katika kuombea watu . Alivuna za kutosha sasa analia kivulini hizo pesa za mazuzu.
Amepumzika kwenye kasri lake pale njia ya chini Kona Mbezi beach kuelekea mara mara ya Kawe. zamanii tuliliita White House ila naona likadrawal attention ikabidi alibadilishe liwe cream house. Bwana Yesu Asifiwe
 
Alisaliti wokovu akafungamana na shetani.

Labda anafanya toba.

Labda yuko kwa mkewe.

Nenda kwenye lile kasri lake kamuulizie
 
Yupo HQ anachapa kazi, mlitaka aende KK!!
 
ASKOFU wa Kanisa la Full Gospel Bible Felloship (BGBF), Zachary Kakobe yupo wapi?

Ni mwaka wa pili sasa haonekani Kanisani. Hata Mke wake anaweza kuja Kanisani mara Moja kwa mwezi.

Je, kuna aliyemuona Askofu huyu huko mliko au kukutana naye?

Na wanaosambaza habari eti kapoteza kumbukumbu, naomba hizo habari msinipe mimi kwani nyie sio wasemaji wa Familia au Kanisa.

Kama anaumwa augue pole ila Kakobe ni Baba yetu wa Kiroho na tunamtegemea kwa Huduma.

Kanisa au Familia ijitokeze iseme yupo wapi ili kuondoa minong'ono isiyo furahisha. Baba yetu yupo wapi?

Kakobe anachunga kanisa Kubwa sana Dar-Es-Salaam, ambalo ni kanisa mama na amewafundisha yeye mwenyewe na kuwatuma kwenye mashamba ya Bwana zaidi ya wachungaji 700.

Jumapili, tarehe 7 Machi, 1993; aliwatawadha kundi la kwanza la wachungaji 28 (Wachungaji 19 na Wachungaji Wasaidizi 9); na kuwapa mamlaka ya kufungua makanisa tanzu ya kwanza 19 (au makanisa mtoto), katika makao makuu ya mikoa yote 19 iliyokuwepo Tanzania bara enzi hizo;

Na Februari 2000, Kakobe tayari alikuwa ameshaanzisha zaidi ya Makanisa tanzu 400 (au Makanisa mtoo) yaliyo tapakaa mikoa na wilaya yote ya Tanzania bara.

Mara ya mwisho mimi kumuona alikuwa na Hayati Magufuli katika hafla ya makabidhiano ya Mfumo wa Kudhibiti Mawasiliano ya Ndani na Nje ya Nchi (TTMS) iliyofanyika makao Makuu ya TCRA Jijini Dar es salaam
 
Bado anaomboleza msiba wa nduli magufuli akiwa kanisan kwake mawasiliano barabara ya kawe maana kipindi cha awamu ya tano aligeuka mpiga zumari kama masukuma gang na wale nguruwe wa uvccm.
 
Lengo lilisha timia, amezipiga za wajinga, amepumzika. Hana haja ya kupayuka tena mana alikuwa anjua kuwa anawadanganya wajinga! Nasikia ana jengo matata kwake hata New York halipo πŸ˜€ πŸ˜€ πŸ˜€ πŸ˜€

Sasa zinapigwa na Mwamposa, wajinga bado wengi na wanazidi kuzaliwa!
 
Kuna Uzi Fulani uliletwa humu JF mtoto wake wa Kiume nae anamtafuta,hajaonana nae miaka mingi sana na ameandika barua zaidi ya 300 na kuzifikisha Kanisani ila majibu hajapata,ni mtu mzima kidogo,sasa unaweza kuona ilivyo kazi kujua alipo.
 
Anatumbua tu hela za mambugila +wjngaaa
Anakula maisha tu

Ova
 
Safi sana acha apge Hela alizovuna Kwa wajinga,Sasa hvi ni wakati WA mwingine kuvuna
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…