Yupo wapi dereva teksi alyefichua njama za kumpindua Nyerere mwaka 1982? Je, alilipwa chochote kama ‘asante’?

Yupo wapi dereva teksi alyefichua njama za kumpindua Nyerere mwaka 1982? Je, alilipwa chochote kama ‘asante’?

Kuna ubaya gani mfano JWTZ kuwa na chama? Huoni ni kutengeneza safety net kuliko say chama tawala kiangushwe na radicalists kama CUF ya 1990s?
Umeona cuf ya 90s ni radicalists,ndo mlivyokua mnaambiana kanisani!?.. radicalists kwa misingi gani!?..by the way hoja ilikua vyama vya upinzani ni Mali ya serikali,yaani wafuasi mnaruka mkojo manakanyaga makimba
 
.by the way hoja ilikua vyama vya upinzani ni Mali ya serikali,yaani wafuasi mnaruka mkojo manakanyaga makimba
Kuwa na TISS kwenye chama ndio kuwa Mali ya serikali? The worst case ni hao TISS waliopo Chadema kuvujisha Siri za vikao kwa Samia ila zaidi ya hapo kuwa na mbea kwenye familia haifanyia familia Yako kuwa Mali ya anayepelekewa umbeya.
Umeona cuf ya 90s ni radicalists,ndo mlivyokua mnaambiana kanisani!?..
Mbona Kuna clip ya Lipumba msikitni akisema "alimuokoa JK 2010". Same case na ule mdahalo wa CUF vs CHADEMA 2011, CUF kupitia hamad Rashid walisema hawawezi shirikiana na Chadema maana kimekaa kikatoliki sana!!
 
Miaka hiyo idara nyeti ndio pekee ilikua ikimiliki taksiii nzuri na mpya na zilitapakaa mjini Kwa lengo Moja tu kuwanasa vigogo mana kipindi hicho hapakua na usafiri binafsi ..... lengo kuu lilitimia na mipango yote miovu ilifichukiwa.

Usiku mwema
 
Kwani nchi zote zenye amani Nyerere alizaliwa humo?. Hata asingezaliwa Tanzania huyo nyerere, nchi hii ingekuwa imesimama ilivvyo, pengine ingekuwa bora zaidi. Inawezekana kuwepo Nyerere ktk nchi hii ndio chanzo cha matatizo yote tuliyonayo Leo. Alizima ndoto/mawazo mbadala ya akina Tuntemeke Sanga, Oscar Kambona, Edwin Mtei etc. Mawazo ya hawa wazalendo na wengineo yangepokelewa, yawezekana leo Tanzania ingekuwa mbali. Ila kwa udikteta/uroho wa madaraka wa Nyerere hawa waliishia kizuizini au kutoroka nchi.
Nyerere kafa miaka mingapi mpaka leo tunatembeza mabakuli duniani?
Kama hatuwezi badilisha chochote alichofanya Nyerere maana yake sisi na batamzinga hatutofautiani akili.

Nyinyi ndio walewale mnasema Ruge alikuwa ananyonya wasanii, kafariki na sasa hivi hata wa kuwanyonya hawamuoni.

Huo unaoita uroho wa madaraka ndio uliokoa nchi, hakuna nchi inaongozwa na watu from nowhere wakijisikia inafanikiwa. Kisa mtu kasoma nje anataka awe Rais sasa tungekuwa na Marais wangapi.
Nigeria ambao wamebadilisha Marais mara 14 wana nini cha maana ukilinganisha na rasilimali zao zote?

Sudan waliopata mapinduzi mara 7 na mara nyingine zaidi ya kumi wakifeli wanatuzidi nini zaidi ya kugawana nchi, kupigana civil wars mara tatu na kuzalisha wakimbizi?

Nyerere hakuwa malaika alikuwa mkosefu kama hao wote ambavyo wangekuwa. Kujifanya unaamini wangekuwa tofauti na yeye ni kutoelewa ngozi nyeusi tulivyo. Marais watano wamemfuata Nyerere mbona hakuna maajabu. Hadi katiba aliyoacha anadai imechoka bado ipo baadae miaka 25 amefariki.
 
Kwani Edward Mondlane na Samora Machel walipouawa, Msumbiji (au FRELIMO) kulitokea ombwe la uongozi? Kwame Nkrumah alipopinduliwa, hatimaye Ghana yakafuatia mapinduzi mengine mengi, imezuia nchi hiyo kuendelea? Pengine mapinduzi Yale yangefanikiwa tusingekuwa na hiki 'kijitabu' cha 1977, ambacho ndio chanzo cha nchi kuwepo ukoloni mamboleo. Mapinduzi mengine yanaweza kuleta matokeo chanya. Ndio maana leo marehemu Jerry Rawlings anaheshimika Ghana
Msumbiji unaona wana maendeleo sana kwamba unatamani ungekuwa kama wao?
Au Ghana unaona wana maendeleo sana kwa leo tofauti na miaka ya Nkrumah? Yani unailinganisha hii Ghana ya leo ya Nana Akufo Ado ambayo imedefault mwaka jana dhidi ya Ghana ya Nkrumah iliyokuwa inatoa misaada kwa nchi za Afrika.

Sasa nenda kafanye ufuatiliaji mfupi sana kwa Msumbiji uulize nani kiongozi wao bora wa muda wote. Kisha waulize Ghana nani kiongozi wao bora wa muda wote kisha jiulize kwanini haohao unaowakataa ndio wanakubalika zaidi. Nkrumah kafanya miradi miaka ya 1960s ambayo hamna serikali yeyote iliyofuata ilijaribu hata kukaribia.
Kama mapinduzi yangekuwa ya maana kwanini Ghana waliachana nayo baada ya third republic? Kwamba kitu kizuri mnaachana nacho mnarudi cha zamani mlichodai ni kibaya.
 
Kwa nini hayo hayakutokea U.S.A, China, Russia, France ?
Hapo unalinganisha nchi za ulimwengu wa kwanza dhidi ya nchi moja masikini iliyosubiri COVID 19 itokee ikapeleka data ipewe hela za kujenga vyoo.
Unaanzaje kuliganisha nchi isiyo hata na uwezo wa kujitosheleza kuhifadhi kiyesi chake bali mpaka ugonjwa uibuke duniani na wazungu watoe hela za pole dhidi ya nchi kama Marekani
 
Back
Top Bottom