Yusuf Manji; kielelezo cha “malaika waliogeuzwa shetani”

Yusuf Manji; kielelezo cha “malaika waliogeuzwa shetani”

Maisha ya fahari, utata na kusikitisha sana.
 
Ila haya maisha. Jamaa nasikia alifanya booonge ya pati baada ya kusikia jiwe amevuta. Unaambiwa jamaa alifurahi utafikiri alihakikishiwa na Allah kwamba atakuwa Hafi ng'oo

..sasa kuna kitu gani cha ajabu hapo?

..Jpm alijaribu kumuua Manji, sasa unashangaa au unalaumu nini Manji kufurahia kifo cha Jpm?

..Yeye Jpm hakuwa akifurahia kuteka, kutesa, na kuua, aliohisi ni maadui zake?

..Kauli ya Jpm kwamba waliokuwa wakishi kama malaika wataishi kama mashetani inakueleza nini?

..Jpm alikuwa binadamu. Kuna watu aliwatendea wema hao lazima walisikitishwa na kifo chake. Jpm pia aliwakosea watu fulani hivyo tusiwashangae waliofurahia kifo chake.
 
..sasa kuna kitu gani cha ajabu hapo?

..Jpm alijaribu kumuua Manji, sasa unashangaa au unalaumu nini Manji kufurahia kifo cha Jpm?

..Yeye Jpm hakuwa akifurahia kuteka, kutesa, na kuua, aliohisi ni maadui zake?

..Kauli ya Jpm kwamba waliokuwa wakishi kama malaika wataishi kama mashetani inakueleza nini?

..Jpm alikuwa binadamu. Kuna watu aliwatendea wema hao lazima walisikitishwa na kifo chake. Jpm pia aliwakosea watu fulani hivyo tusiwashangae waliofurahia kifo chake.
Ngoja nikuache kwa muda. Nitakurudia
 
Hadithi hii inatukumbusha ukuu wa MUNGU. Vyote tunavyosumbukia duniani ni bure tu,ni ubatiri tu. Ni vya muda mfupi tu. Unatamba navyo kwa muda mfupi sana.

Kitu ambacho watu wengi hatujifunzi ukuu wa MUNGU ni namna ya kuishi. Matajiri wengi wanaishi kwa wasiwasi sana,wanaishi kwa mashaka sana tofauti na masikini au mwenye ukawaida. Na zaidi matajiri wengi hata viongozi walio matajiri wamedhurumu sana hapa. Wametanya mambo ya kutisha ya kuogofya huko gizani. Lakini MUNGU anawaona. Kwa hiyo wanaishi kwa mashaka hapa duniani hawana Amani na huko mbinguni (kama kuna adhabu) wanatumikia adhabu kubwa.
Tofauti na masikini. Mara nyingi masikini ndie anaefurahia maisha. Ksbb hana baya. Na huko mbinguni pia atafurahia maisha,(kama kuna maisha baada ya hapa). Ukuu wa MUNGU.

Ukuu mwingine wa MUNGU ni kwamba tajiri anakula nyama na masikini anakula nyama pia. Kwa hiyo kilichopo hapa duniani kinacholiwa, MUNGU kawapa wote wakile. Na bahati kubwa masikini wa kijijini huko,pamoja na umasikini wake MUNGU kamuongezea vyakula vya asili na hali ya hewa nzuri ya asili huko kijijini. Na ndio maana masikini wa huko kijijini ana maisha marefu kuliko tajiri huku mjini.
Mkumbuke MUNGU siku za ujana wako na uhai wako
 
FEBRUARI 8, 2017, ilikuwa Jumatano. Paul Makonda, wakati huo akiwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, alitaja orodha ya aliowatuhumu kuwa vigogo wa biashara ya dawa za kulevya Tanzania.

Ilikuwa kutaja majina zigzaga. Taifa likazizima. Askofu Josephat Gwajima wa Kanisa la Ufufuo na Uzima ndani. Halafu, Uchaguzi Mkuu 2020, Gwajima alipitishwa na CCM kugombea ubunge Kawe. Makonda, mtaja majina ya wauza unga, alienguliwa na CCM Kigamboni. Gwajima, mtuhumiwa wa dawa za kulevya ni mbunge leo.

Waruke wengine, kisha mlete Yusuf Mehbub Manji, tycoon wa Quality Group. “Niliowataja Ijumaa waripoti central,” Makonda alitoa amri. Kama mzaha, huo ndiyo ulikuwa mwanzo wa mwisho wa bilionea Manji. Kijana aliyepata kuwa na “miguvu” mingi Afrika Mashariki. Miguvu ya pesa.

Alipofika central Manji hakutoka. Yakaanza maisha ya mahabusu. Safari ya kwa mkemia mkuu kupimwa mkojo. Ooh, majibu ni chanya. Ukafuata mchuano wa fedha na mamlaka. Bonge la mechi. Sijui nani alishinda!

Vuta nikuvute mahakamani; madaktari wakatoa uthibitisho kuwa ile chanya ya mkonjo wa Manji wala si mihadarati, bali dawa mfululizo ambazo bilionea huyo alikuwa akitumia kutokana na maradhi aliyokuwa nayo. Fedha ni mfalme wa kila rasilimali. Ikiwemo rasilimali watu.

Mawakili wa nchi hadi nchi nyuma ya Manji dhidi ya wale wa Serikali. Halafu, mahabusu akawa hakai, muda mwingi ripoti za madaktari zilielekeza apewe uangalizi hospitali. Akapelekwa Aga Khan Hospital, Dar es Salaam. Wodi ya kitajiri. Ukiisogelea muda wote inanukia moshi wa sigara. Bingwa alikuwa zake ndani anachoma, hakuwa na wasi!

Ikapenyezwa kuwa hata polisi waliomlinda Manji hospitalini sababu alikuwa mahabusu, nao walineemeka. Posho Sh150,000 kila siku. Kila ofisa wa polisi alitamani kupangiwa zamu ya kumlinda mahabusu Manji, alipokuwa “akipatiwa matibabu” Aga Khan. Wenye mamlaka walitaka ateseke. Fedha ikatumika kugeuza mchezo.

Ikanyunyizwa na ikadhihirika, Makonda alikuwa rimoti tu. Mwenye rimoti alikuwa Mkuu wa Nchi, Jibaba Dk John Pombe Magufuli. “Ni vita ya kisasi”, ndivyo ilinong’onwa. Eti, enzi hizo Magufuli akiwa Waziri, alimkabili Manji, ambaye alimjibu: “Siongei na mbwa, naongea na mwenye mbwa.”

Wakati huo, Rais madarakani alikuwa Jakaya Kikwete. Ndiye alikuwa mwenye mbwa siyo? Novemba 5, 2015, aliyeambiwa “siongei na mbwa”, akageuka mwenye mbwa. Akaanza kutuma “mbwa wake” wamng’ate Manji. Hawakumbakisha salama.

Kesi mfululizo za uhujumu uchumi, faini za mabilioni ya fedha kwa ukwepaji kodi, malimbikizo ya kodi, kumiliki hati za kusafiri za nchi zaidi ya moja, halafu akakamatwa kwa kukutwa na sare za jeshi. Eti, alishinda zabuni ya kusambaza sare za Jeshi la Wananchi, kisha akakamatwa kwa kosa la kukutwa na sare za jeshi!

Manji wa sopsop, akageuka Manji madevu. Maisha ya mahabusu hakuzoea. Mtoto wa kitajiri, akaanzisha safari ya utajiri wake binafsi akiwa na umri wa miaka 20, akageuka bilionea mkubwa. Maisha nyuma ya nondo kwenye jela ya Keko, ilikuwa kumwonjesha jehanamu kabla ya mauti.

Haijulikani alikubaliana nini na wenye mamlaka. Ghafla, baada ya msoto mrefu, taarifa ya Mkurugenzi wa Mashitaka ya Umma (DPP), ikaeleza nia ya kuendelea na mashitaka dhidi ya Manji haikuwepo tena. Akaachiwa. Huyooo, akasafiri kwenda Marekani. Biashara zake akahamisha.

Kabla ya zama za mwenye visasi, ungefika jengo la Quality Plaza, Nyerere Road, ofisi zilikuwa nadhifu. Yale mazuria sakafuni na sanaa kubwa iliyotumika kusanifu mwonekano wa jengo kwa ndani, ungejua kuwa pesa nyingi ilikuwepo ndani yake. Quality Plaza siku hizi limekuwa jengo la PSSSF.

Namkumbuka Manji kwenye nyakati zake za heri. Alimshusha Raila Odinga kutoka Kenya, kuzindua Quality Centre Mall. Ilikuwa sehemu ambayo ungepata kila kitu. Siku hizi Quality Centre limebaki kuwa jengo la kumbukumbu za kihistoria.

Zama kabla ya mwenye visasi, ungemwona Manji ziarani na Rais Kikwete. Alikuwa alama ya sekta binafsi Tanzania. Manji alipata kuwa fahari ya nchi katika uwekezaji, hasa barani Afrika.
Magufuli, kiongozi aliyehisi watu wanamdharau au walimdharau alipokuwa waziri, hata hotuba zake ziliashiria kuwa kifua chake kilibeba visasi. “Wale waliokuwa wanaishi kama malaika, wataishi kama Shetani,” alitamka waziwazi Rais Magufuli.

Yaliyompata Manji, ndiyo tafsiri ya wengi kuwa alikuwa akiishi kama malaika kabla, akapewa msoto uliomfanya aishi mithili ya Shetani. Manji, maisha yake yalivyobadilika, ni kielelezo cha utawala wa Magufuli, jinsi alivyobomoa jumuiya ya kibiashara na kuwaning’iniza wengi “msalabani”.

Kesi nyingi za uhujumu uchumi kwa wafanyabishara, walipoambiwa watengeneze mwafaka nje ya mahakama (plea deal), fedha walizolipa, kumbe zikapelekwa kufichwa China. Dhuluma kwa wafanyabishara wa Bureau de Change na wengine. Manji alishushiwa ankara zenye zaidi ya Sh12.3 bilioni. Akalipa!

Jambo la kusikitisha, si Manji wala Magufuli aliye hai leo. Magufuli alifumba macho tangu Machi 2021 na taifa likatangaziwa kifo Machi 17, 2021. Manji, naye aliingia usingizini Juni 29, 2024. Wenye ukweli kamili wa hadithi ya “mbwa na mwenye mbwa”, wote wameshalala usingizi wa mauti. Pengine, maisha baada ya kifo yatawakutanisha na wataombana msamaha. Mungu ndiye anajua.

Ameondoka Manji, kwa familia yake alikuwa baba, kaka na mtoto, kwa taifa la Tanzania, alikuwa raia aliyejenga athari chanya kwenye maisha ya wengi. Kupitia biashara zake, aliajiri maelfu ya Watanzania. Kadhalika mamia ya Wahindi walioshushwa kutoka India.

Katika soka, Manji alipata kuwa oksijeni ya Yanga. Alianza na udhamini wa mchezo wa kubahatisha wa Lotto Kitita, baadaye akawa mfadhili mkuu, kisha Mwenyekiti wa Klabu. Kipindi chake, Yanga ilipata mafanikio makubwa uwanjani kwa kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara, misimu mitatu mfululizo (2014-2015, 2015-2016 na 2016-2017).

Manji jeuri sana; Juni 28, 2016, Yanga ilicheza mechi ya Kombe la Shirikisho (Caf), dhidi ya TP Mazembe, hatua ya makundi. Mechi ilichezwa Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam. Kwa kuwa Yanga walikuwa wenyeji na kwa sababu Manji alikuwa na mvutano dhidi ya uongozi wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), aliagiza mashabiki waingie bure ili TFF wakose mapato. Halafu upande wa Yanga, alibeba gharama zote yeye mwenyewe.

Manji, nyakati zake za heri, alimpeleka puta mfanyabiashara gwiji Tanzania, Reginald Mengi. Waliendeshana kwenye vyombo vya habari hadi mahakamani. Halafu, Manji kwa jeuri ya fedha, aliwang’oa Original Comedy, East Africa TV, akawapeleka TBC. Yote kumkomoa Mengi. Manji, alikuwemo ndani ya orodha ya “Mafisadi Papa Tanzania”, iliyosomwa na Mengi.

Manji mtata sana; alimburuza Mengi mahakamani kwa kumchafulia jina, halafu akaomba fidia alipwe Shilingi Moja ya Tanzania. Hii ilimaanisha kuwa Manji hakutaka fedha za fidia, isipokuwa alitaka kumshughulisha Mengi. Inasikitisha kuwa leo, wote, Mengi na Manji hawapo duniani. Mengi alivuta pumzi ya mwisho Mei 2, 2019. Pengine maisha baada ya kifo yatawafanya Manji na Mengi kuwa marafiki. Nani anajua?

Manji ni mada nzito; mwaka 2000, akiwa kijana mwenye umri wa miaka 25, aliingia kwa kishindo kugombea ubunge, jimbo la Kigamboni. Fedha alizomwaga zilimtikisa aliyekuwa Mwenyekiti CCM, Rais Benjamin Mkapa, ambaye ilibidi aingilie kati kumdhibiti. Haitoshi, Mkapa amesimulia kuhusu Manji kwenye kitabu chake, “My Life, My Purpose” – “Maisha Yangu, Kusudi Langu.”

Hakuna aliyejua kuwa mwisho wa Manji ungekuwa namna hii. Baada ya kuhamia Marekani, Julai 29, 2019, alifunguliwa mashitaka ya kuendesha gari akiwa na kilevi (Driving Under Influence “DUI”), kwenye jimbo la Florida. Mwaka 2021, baada ya Magufuli kufariki dunia, alirejea Tanzania akiwa na matumaini. Akawekwa mahabusu. Alipotoka, aliondoka zake.

Miaka 49 ya kuishi duniani, imetosha Manji kuhitimisha safari. Aliandika Franz Kafka, mwandishi wa Ujerumani: “The meaning of life is that it stops.” – “Mantiki ya maisha ni kwamba hukoma.” Ingekuwa uhai hauna mwisho, maisha yasingekuwa na maana yoyote. Nasadiki.

Shairi la faraja kutoka kwa mwandishi na mwinjilisti wa Marekani, Max Lucado, likujenge imani kuwa kifo si hasara: “We see a hearse; we think sorrow. We see a grave; we think despair. We hear of a death; we think of a loss. Not so in heaven. When heaven sees a breathless body, it sees the vacated cocoon & the liberated butterfly.”

Kiswahili: “Tunaona gari la maiti; tunajisikia majonzi. Tunaona kaburi; tunajisikia kukata tamaa. Tunasikia kuhusu kifo; tunajisikia kupoteza. Haipo hivyo mbinguni. Mbingu inapoona mwili usiopumua, huona kiumbe kilicho huru na kipepeo aliyekombolewa.”

Usiku mwema Yusuf Mehbub Manji.

Source : Luqman Maloto
Mwandishi ana kalamu nzuri sana ya uandishi
 
Maua mengi kwake Luqman..

Pamoja na historia ndogo ya maisha ya Manji, basi tumpe sifa ndugu yetu Luqman Maloto.

Hakika ni mwandishi wa viwango vya juu na vilivyotukuka. Anajua kumshawishi msomaji aendelee kumsoma. Mtiririko wake hauchoshi. Uchaguzi wake wa maneno ni wa viwango vya juu.

Uunganishaji wake wa visa na mikasa vya wahusika inavutia sana kuendana nayo. Vijana wa sasa wangesema mdundo na biti lake halina mfano. Ni hodari kweli kweli.

Ni mwandishi ambaye kwa hakika siwezi kuacha makala yake inipite bila kuimaliza. Ana taarifa nyingi za kweli, ambazo hakika hutotoka bure, hutojutia muda wako.

Alale salama tycoon Manji.
Mi naipa heshima hii comment huenda ningeamua kumpongeza msimuliaji nisingeweza Kutumia maneno mazuri kama haya
 
Kauli ya kutoongea na mbwa ilikuwa ya Manji au Hans Pope kwenye mgogoro wa wamiliki wa malori enzi za JK huku Magu akiwa Waziri wa ujenzi
 
Kauli ya kutoongea na mbwa ilikuwa ya Manji au Hans Pope kwenye mgogoro wa wamiliki wa malori enzi za JK huku Magu akiwa Waziri wa ujenzi

mkuu ni story ya kijiweni ambayo kila aliekuwa mbaya wa magu alikuwa anapachikiwa.
 
FEBRUARI 8, 2017, ilikuwa Jumatano. Paul Makonda, wakati huo akiwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, alitaja orodha ya aliowatuhumu kuwa vigogo wa biashara ya dawa za kulevya Tanzania.

Ilikuwa kutaja majina zigzaga. Taifa likazizima. Askofu Josephat Gwajima wa Kanisa la Ufufuo na Uzima ndani. Halafu, Uchaguzi Mkuu 2020, Gwajima alipitishwa na CCM kugombea ubunge Kawe. Makonda, mtaja majina ya wauza unga, alienguliwa na CCM Kigamboni. Gwajima, mtuhumiwa wa dawa za kulevya ni mbunge leo.

Waruke wengine, kisha mlete Yusuf Mehbub Manji, tycoon wa Quality Group. “Niliowataja Ijumaa waripoti central,” Makonda alitoa amri. Kama mzaha, huo ndiyo ulikuwa mwanzo wa mwisho wa bilionea Manji. Kijana aliyepata kuwa na “miguvu” mingi Afrika Mashariki. Miguvu ya pesa.

Alipofika central Manji hakutoka. Yakaanza maisha ya mahabusu. Safari ya kwa mkemia mkuu kupimwa mkojo. Ooh, majibu ni chanya. Ukafuata mchuano wa fedha na mamlaka. Bonge la mechi. Sijui nani alishinda!

Vuta nikuvute mahakamani; madaktari wakatoa uthibitisho kuwa ile chanya ya mkonjo wa Manji wala si mihadarati, bali dawa mfululizo ambazo bilionea huyo alikuwa akitumia kutokana na maradhi aliyokuwa nayo. Fedha ni mfalme wa kila rasilimali. Ikiwemo rasilimali watu.

Mawakili wa nchi hadi nchi nyuma ya Manji dhidi ya wale wa Serikali. Halafu, mahabusu akawa hakai, muda mwingi ripoti za madaktari zilielekeza apewe uangalizi hospitali. Akapelekwa Aga Khan Hospital, Dar es Salaam. Wodi ya kitajiri. Ukiisogelea muda wote inanukia moshi wa sigara. Bingwa alikuwa zake ndani anachoma, hakuwa na wasi!

Ikapenyezwa kuwa hata polisi waliomlinda Manji hospitalini sababu alikuwa mahabusu, nao walineemeka. Posho Sh150,000 kila siku. Kila ofisa wa polisi alitamani kupangiwa zamu ya kumlinda mahabusu Manji, alipokuwa “akipatiwa matibabu” Aga Khan. Wenye mamlaka walitaka ateseke. Fedha ikatumika kugeuza mchezo.

Ikanyunyizwa na ikadhihirika, Makonda alikuwa rimoti tu. Mwenye rimoti alikuwa Mkuu wa Nchi, Jibaba Dk John Pombe Magufuli. “Ni vita ya kisasi”, ndivyo ilinong’onwa. Eti, enzi hizo Magufuli akiwa Waziri, alimkabili Manji, ambaye alimjibu: “Siongei na mbwa, naongea na mwenye mbwa.”

Wakati huo, Rais madarakani alikuwa Jakaya Kikwete. Ndiye alikuwa mwenye mbwa siyo? Novemba 5, 2015, aliyeambiwa “siongei na mbwa”, akageuka mwenye mbwa. Akaanza kutuma “mbwa wake” wamng’ate Manji. Hawakumbakisha salama.

Kesi mfululizo za uhujumu uchumi, faini za mabilioni ya fedha kwa ukwepaji kodi, malimbikizo ya kodi, kumiliki hati za kusafiri za nchi zaidi ya moja, halafu akakamatwa kwa kukutwa na sare za jeshi. Eti, alishinda zabuni ya kusambaza sare za Jeshi la Wananchi, kisha akakamatwa kwa kosa la kukutwa na sare za jeshi!

Manji wa sopsop, akageuka Manji madevu. Maisha ya mahabusu hakuzoea. Mtoto wa kitajiri, akaanzisha safari ya utajiri wake binafsi akiwa na umri wa miaka 20, akageuka bilionea mkubwa. Maisha nyuma ya nondo kwenye jela ya Keko, ilikuwa kumwonjesha jehanamu kabla ya mauti.

Haijulikani alikubaliana nini na wenye mamlaka. Ghafla, baada ya msoto mrefu, taarifa ya Mkurugenzi wa Mashitaka ya Umma (DPP), ikaeleza nia ya kuendelea na mashitaka dhidi ya Manji haikuwepo tena. Akaachiwa. Huyooo, akasafiri kwenda Marekani. Biashara zake akahamisha.

Kabla ya zama za mwenye visasi, ungefika jengo la Quality Plaza, Nyerere Road, ofisi zilikuwa nadhifu. Yale mazuria sakafuni na sanaa kubwa iliyotumika kusanifu mwonekano wa jengo kwa ndani, ungejua kuwa pesa nyingi ilikuwepo ndani yake. Quality Plaza siku hizi limekuwa jengo la PSSSF.

Namkumbuka Manji kwenye nyakati zake za heri. Alimshusha Raila Odinga kutoka Kenya, kuzindua Quality Centre Mall. Ilikuwa sehemu ambayo ungepata kila kitu. Siku hizi Quality Centre limebaki kuwa jengo la kumbukumbu za kihistoria.

Zama kabla ya mwenye visasi, ungemwona Manji ziarani na Rais Kikwete. Alikuwa alama ya sekta binafsi Tanzania. Manji alipata kuwa fahari ya nchi katika uwekezaji, hasa barani Afrika.
Magufuli, kiongozi aliyehisi watu wanamdharau au walimdharau alipokuwa waziri, hata hotuba zake ziliashiria kuwa kifua chake kilibeba visasi. “Wale waliokuwa wanaishi kama malaika, wataishi kama Shetani,” alitamka waziwazi Rais Magufuli.

Yaliyompata Manji, ndiyo tafsiri ya wengi kuwa alikuwa akiishi kama malaika kabla, akapewa msoto uliomfanya aishi mithili ya Shetani. Manji, maisha yake yalivyobadilika, ni kielelezo cha utawala wa Magufuli, jinsi alivyobomoa jumuiya ya kibiashara na kuwaning’iniza wengi “msalabani”.

Kesi nyingi za uhujumu uchumi kwa wafanyabishara, walipoambiwa watengeneze mwafaka nje ya mahakama (plea deal), fedha walizolipa, kumbe zikapelekwa kufichwa China. Dhuluma kwa wafanyabishara wa Bureau de Change na wengine. Manji alishushiwa ankara zenye zaidi ya Sh12.3 bilioni. Akalipa!

Jambo la kusikitisha, si Manji wala Magufuli aliye hai leo. Magufuli alifumba macho tangu Machi 2021 na taifa likatangaziwa kifo Machi 17, 2021. Manji, naye aliingia usingizini Juni 29, 2024. Wenye ukweli kamili wa hadithi ya “mbwa na mwenye mbwa”, wote wameshalala usingizi wa mauti. Pengine, maisha baada ya kifo yatawakutanisha na wataombana msamaha. Mungu ndiye anajua.

Ameondoka Manji, kwa familia yake alikuwa baba, kaka na mtoto, kwa taifa la Tanzania, alikuwa raia aliyejenga athari chanya kwenye maisha ya wengi. Kupitia biashara zake, aliajiri maelfu ya Watanzania. Kadhalika mamia ya Wahindi walioshushwa kutoka India.

Katika soka, Manji alipata kuwa oksijeni ya Yanga. Alianza na udhamini wa mchezo wa kubahatisha wa Lotto Kitita, baadaye akawa mfadhili mkuu, kisha Mwenyekiti wa Klabu. Kipindi chake, Yanga ilipata mafanikio makubwa uwanjani kwa kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara, misimu mitatu mfululizo (2014-2015, 2015-2016 na 2016-2017).

Manji jeuri sana; Juni 28, 2016, Yanga ilicheza mechi ya Kombe la Shirikisho (Caf), dhidi ya TP Mazembe, hatua ya makundi. Mechi ilichezwa Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam. Kwa kuwa Yanga walikuwa wenyeji na kwa sababu Manji alikuwa na mvutano dhidi ya uongozi wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), aliagiza mashabiki waingie bure ili TFF wakose mapato. Halafu upande wa Yanga, alibeba gharama zote yeye mwenyewe.

Manji, nyakati zake za heri, alimpeleka puta mfanyabiashara gwiji Tanzania, Reginald Mengi. Waliendeshana kwenye vyombo vya habari hadi mahakamani. Halafu, Manji kwa jeuri ya fedha, aliwang’oa Original Comedy, East Africa TV, akawapeleka TBC. Yote kumkomoa Mengi. Manji, alikuwemo ndani ya orodha ya “Mafisadi Papa Tanzania”, iliyosomwa na Mengi.

Manji mtata sana; alimburuza Mengi mahakamani kwa kumchafulia jina, halafu akaomba fidia alipwe Shilingi Moja ya Tanzania. Hii ilimaanisha kuwa Manji hakutaka fedha za fidia, isipokuwa alitaka kumshughulisha Mengi. Inasikitisha kuwa leo, wote, Mengi na Manji hawapo duniani. Mengi alivuta pumzi ya mwisho Mei 2, 2019. Pengine maisha baada ya kifo yatawafanya Manji na Mengi kuwa marafiki. Nani anajua?

Manji ni mada nzito; mwaka 2000, akiwa kijana mwenye umri wa miaka 25, aliingia kwa kishindo kugombea ubunge, jimbo la Kigamboni. Fedha alizomwaga zilimtikisa aliyekuwa Mwenyekiti CCM, Rais Benjamin Mkapa, ambaye ilibidi aingilie kati kumdhibiti. Haitoshi, Mkapa amesimulia kuhusu Manji kwenye kitabu chake, “My Life, My Purpose” – “Maisha Yangu, Kusudi Langu.”

Hakuna aliyejua kuwa mwisho wa Manji ungekuwa namna hii. Baada ya kuhamia Marekani, Julai 29, 2019, alifunguliwa mashitaka ya kuendesha gari akiwa na kilevi (Driving Under Influence “DUI”), kwenye jimbo la Florida. Mwaka 2021, baada ya Magufuli kufariki dunia, alirejea Tanzania akiwa na matumaini. Akawekwa mahabusu. Alipotoka, aliondoka zake.

Miaka 49 ya kuishi duniani, imetosha Manji kuhitimisha safari. Aliandika Franz Kafka, mwandishi wa Ujerumani: “The meaning of life is that it stops.” – “Mantiki ya maisha ni kwamba hukoma.” Ingekuwa uhai hauna mwisho, maisha yasingekuwa na maana yoyote. Nasadiki.

Shairi la faraja kutoka kwa mwandishi na mwinjilisti wa Marekani, Max Lucado, likujenge imani kuwa kifo si hasara: “We see a hearse; we think sorrow. We see a grave; we think despair. We hear of a death; we think of a loss. Not so in heaven. When heaven sees a breathless body, it sees the vacated cocoon & the liberated butterfly.”

Kiswahili: “Tunaona gari la maiti; tunajisikia majonzi. Tunaona kaburi; tunajisikia kukata tamaa. Tunasikia kuhusu kifo; tunajisikia kupoteza. Haipo hivyo mbinguni. Mbingu inapoona mwili usiopumua, huona kiumbe kilicho huru na kipepeo aliyekombolewa.”

Usiku mwema Yusuf Mehbub Manji.

Source : Luqman Maloto
Uandishi mzuri, ila kumtaja taja Magufuli na kumuelezea sifa zake kwa kupotosha na kuweka kinyongo, yaonesha wazi kuwa wewe ni mtu wa visasi usiyesamehe.
 
Mwandishi nafahamu ulifaudika na mgogoro wa Manji na Mengi.Hebu tufafanuliwe japo kiduchu
Hapana, ni mmoja wa waliokutana na madhila ya Musiba baada ya kupora sehemu yao ya kupatia kipato pale maeneo ya Gerezani karibu na uwanja wa netiboli miaka ya nyuma.

Maisha haya cha muhimu ni kujifunza kunyenyekea hata kama unapata ugumu sana kujishusha na kupokea maumivu ya kile unachofanyiwa na binadamu mwenye pumzi ya Mungu.
 
Nimejifunza kadhaa kwenye uzi huu.
Mosi paragraph ya mwisho nukuu ya huyo mwinjilisti ilifaa kuwa uzi mwingine.

Pili sikuwa na kumbukumbu nzuri kesi ya manji na mengi kumbe aliye shinda ni manji.

Tatu Magufuli aliacha athari kubwa sana hapa nchini athari chana na hasi, atakuwa kwenye ndimi za watu na kalamu za waandishi miaka na miaka, kila mmoja akielezea engo yake vile avyomchukulia na kumdhaania magufuli, wa mabaya ataelezea yake wa mazuri ataelezea yake wa mrengo wa kati kadhalika.

Mwisho jitihada hazizidi kudra, unaweza ukawa na kila aina ya nyenzo lakini kuna jambo dogo litakushinda , kuonyesha binadamu pamoja kujiinua na kujishusha kwake ni mdhaifu kwa wakati wote.

Wapuzike kwa amani wote walio tangulia walio tajwa kwenye uzi huu.
 
Pamoja na uandishi wake mzuri ila kuna taarifa hana msifie sana kwamba anajua siri nyingi. Hivi unajua ile kauli ya Mama kwamba kuna mtu alikopa benki tano akakimbia nchi ilikuwa inamlenga nani?
Watanzania kuna muda tunapumbazika na kuwaamini watu haraka hususan huku kwenye mitandao.

..Manji alishughulikiwa ktk kesi ambazo hazikuhusisha vigogo wa Ccm.

..Na hizo ndio kesi ambazo zina mashiko na zingeweza kumtia Manji hatiani, ila tatizo zingewaumiza pia vigogo wa Ccm.
 
..Manji alishughulikiwa ktk kesi ambazo hazikuhusisha vigogo wa Ccm.

..Na hizo ndio kesi ambazo zina mashiko na zingeweza kumtia Manji hatiani, ila tatizo zingewaumiza pia vigogo wa Ccm.
Tuishie hapa
Kila mtu aendelee kufahamu anachokifahamu
 
Maua mengi kwake Luqman..

Pamoja na historia ndogo ya maisha ya Manji, basi tumpe sifa ndugu yetu Luqman Maloto.

Hakika ni mwandishi wa viwango vya juu na vilivyotukuka. Anajua kumshawishi msomaji aendelee kumsoma. Mtiririko wake hauchoshi. Uchaguzi wake wa maneno ni wa viwango vya juu.

Uunganishaji wake wa visa na mikasa vya wahusika inavutia sana kuendana nayo. Vijana wa sasa wangesema mdundo na biti lake halina mfano. Ni hodari kweli kweli.

Ni mwandishi ambaye kwa hakika siwezi kuacha makala yake inipite bila kuimaliza. Ana taarifa nyingi za kweli, ambazo hakika hutotoka bure, hutojutia muda wako.

Alale salama tycoon Manji.
Jama ana kitabu kipo sokoni bei ni 75k
 
Makonda amechangia pakubwa kifo cha Manji pamoja na kufilisika
Alikuwa anafuata order kutoka kwa Boss Kubwaa ...
Hata kama ni wewe ungefanya aliyofanya Makonda kumfurahisha Boss ..
Boss kubwa alimkausha Manji kiasi kwamba hakuna aliyeamini tajiri amekwisha ... Alifreez account zote za Tsh na US dollar bila kupepesa macho..

Ikawa haitoshi akachukua viwanja vikubwa alivyokuwa akimiliki Chanika, Kigamboni ... Alikuwa na kampuni ya kununua mazao mashambani na kupeleka nje ikafutiliwa mbali ...
Ilikuwa hatari sana..
 
Back
Top Bottom