Maua mengi kwake Luqman..
Pamoja na historia ndogo ya maisha ya Manji, basi tumpe sifa ndugu yetu Luqman Maloto.
Hakika ni mwandishi wa viwango vya juu na vilivyotukuka. Anajua kumshawishi msomaji aendelee kumsoma. Mtiririko wake hauchoshi. Uchaguzi wake wa maneno ni wa viwango vya juu.
Uunganishaji wake wa visa na mikasa vya wahusika inavutia sana kuendana nayo. Vijana wa sasa wangesema mdundo na biti lake halina mfano. Ni hodari kweli kweli.
Ni mwandishi ambaye kwa hakika siwezi kuacha makala yake inipite bila kuimaliza. Ana taarifa nyingi za kweli, ambazo hakika hutotoka bure, hutojutia muda wako.
Alale salama tycoon Manji.