Yusuph Manji anakodi Yanga, Mo Dewji anachukua bure Simba

Yusuph Manji anakodi Yanga, Mo Dewji anachukua bure Simba

Waswahili utawajua tu!Ndio maana maendeleo hakuna kwa sababu ya uchambuzi wa kiswahili swahili tu
 
Wanachama wa Simba na Yanga wote wana Tatizo moja la msingi. Tatizo Hilo ni "MAARIFA NA WELEDI" juu ya soko la soka.

Suala la kununua au kukodi klabu sio Tatizo. Tatizo ni kwa kiasi gani unaweza kufanya "mapatano" ya kuuza au kukodi kitu ambacho hujui thamani yake. Chifu Mangungo wa Msovero alifanya hivyo, serikali imefanya hivyo, ni ajabu na aibu kwa wanachama wa Simba na Yanga kurudia makosa yale yale.

Mbali ya majengo na rasilimali zenye kuonekana Simba na Yanga wana rasilimali kubwa isiyoonekana ambayo kitaalamu inaitwa "GOODWILL". Je, ni nani kati yetu ajuae thamani ya vilabu hivi viwili. Tunahitaji kwa hakika na bila shaka kujua thamani halisi ya vilabu hivi ili mchakato ima wa kukodisha au kuuza hisa ufanyike.

Yanga na Simba ni migodi inayotembea, tuitendee haki. Wapo watu waliozifanya klabu hizi kuwa hapo zilizopo, ni aibu na fedheha kubwa kwetu kudharau michango ya wazee wetu hao na kuzitoa klabu hizi bure. Kama sio kutetemeka basi watatikisika huko "MAKABURINI".
Kaka naona kama umechanganyikiwa na hauelewi wala kujua unachojaribu kujitia ujuaji.

Uchumi ni nini na fedha na uhasibu ni nini?

Goodwill is not sth that can be quantified like any tangible asset, na wala c brand name ni ile hali ya let’s say kampuni kama coca na umaarufu wake wote iuze kwa bei ya kutupa au kampuni kama banana wine inunuliwe na giant wine manufacturer kama Diageo kwa bei kubwa kuliko uhalisia hvo ndo aidha vinaleta positive au negative goodwill! Hyo taswira unayoitajka wewe ni brand equity na sio goodwill.


#Jipange
 
Kaka naona kama umechanganyikiwa na hauelewi wala kujua unachojaribu kujitia ujuaji.

Uchumi ni nini na fedha na uhasibu ni nini?

Goodwill is not sth that can be quantified like any tangible asset, na wala c brand name ni ile hali ya let’s say kampuni kama coca na umaarufu wake wote iuze kwa bei ya kutupa au kampuni kama banana wine inunuliwe na giant wine manufacturer kama Diageo kwa bei kubwa kuliko uhalisia hvo ndo aidha vinaleta positive au negative goodwill! Hyo taswira unayoitajka wewe ni brand equity na sio goodwill.


#Jipange
Tatizo letu Watanzania "matusi" tumeyaweka mbele. Kisomi na kitaalamu unapombinga mtu huwa tunajenga hoja. Lakini mtu makini hujitahidi kujieleza kwa lugha moja, mtu mwenye kuchanganya lugha ni wazi na bayana kuwa "dhana" anayoijadili haijui.

Uchumi ni nini? Fedha ni nini? Na uhasibu ni nini?
Ukitaka kuyajua haya nenda chuo kikuu uwaulize kwa nini wanatoa shahada ya uchumi, shahada ya masuala ya fedha na shahada ya uhasibu. Lakini pia Jiulize kwa nini Kuna bodi ya wahasibu nchini?
 
Ndiyo. Kaona biashara ya mazao haitoshi sasa anataka kuingia kwenye biashara ya wanyama
ni mpigaji sana yule jamaa, Sikiliza vizuri sana maelezo yake utaona boshen za wazi kabisa
 
Wanachama wa Simba na Yanga wote wana Tatizo moja la msingi. Tatizo Hilo ni "MAARIFA NA WELEDI" juu ya soko la soka.

Suala la kununua au kukodi klabu sio Tatizo. Tatizo ni kwa kiasi gani unaweza kufanya "mapatano" ya kuuza au kukodi kitu ambacho hujui thamani yake. Chifu Mangungo wa Msovero alifanya hivyo, serikali imefanya hivyo, ni ajabu na aibu kwa wanachama wa Simba na Yanga kurudia makosa yale yale.

Mbali ya majengo na rasilimali zenye kuonekana Simba na Yanga wana rasilimali kubwa isiyoonekana ambayo kitaalamu inaitwa "GOODWILL". Je, ni nani kati yetu ajuae thamani ya vilabu hivi viwili. Tunahitaji kwa hakika na bila shaka kujua thamani halisi ya vilabu hivi ili mchakato ima wa kukodisha au kuuza hisa ufanyike.

Yanga na Simba ni migodi inayotembea, tuitendee haki. Wapo watu waliozifanya klabu hizi kuwa hapo zilizopo, ni aibu na fedheha kubwa kwetu kudharau michango ya wazee wetu hao na kuzitoa klabu hizi bure. Kama sio kutetemeka basi watatikisika huko "MAKABURINI".



Ngwananzengo, wanachama wa timu hizi lazima waanzie mahali fulani.
Hatua ya kwanza kabisa ni kukubali kuwa mifumo waliyonayo sasa haifai tena. Kunahitajika mabadiliko. Hicho ndicho walichokifanya. Baada ya hapo ni kuainisha wafuate mfumo gani kulingana na mazingira yao. Hapo ndio ninyi wataalamu sasa ndio mnapoingia. Fanyeni uchambuzi. Leteni faida na hasara ya mifumo hii mipya ya uendeshaji. Ikiwezekana sio mbaya pia kuonyesha njia, ni wapi wanachama wapite kufikia malengo yao.

Kuwalaumu tu wanachama haitoshi na haisaidii. Kwa mfano kumtaka mwanachama wa kawaida kutoka Mpigwa huko Urambo au hata Tandare Uzuri hapa jijini ajue thamani halisi ya Simba, ni kumtwisha mzigo sui wake!!
 
Ngwananzengo, wanachama wa timu hizi lazima waanzie mahali fulani.
Hatua ya kwanza kabisa ni kukubali kuwa mifumo waliyonayo sasa haifai tena. Kunahitajika mabadiliko. Hicho ndicho walichokifanya. Baada ya hapo ni kuainisha wafuate mfumo gani kulingana na mazingira yao. Hapo ndio ninyi wataalamu sasa ndio mnapoingia. Fanyeni uchambuzi. Leteni faida na hasara ya mifumo hii mipya ya uendeshaji. Ikiwezekana sio mbaya pia kuonyesha njia, ni wapi wanachama wapite kufikia malengo yao.

Kuwalaumu tu wanachama haitoshi na haisaidii. Kwa mfano kumtaka mwanachama wa kawaida kutoka Mpigwa huko Urambo au hata Tandare Uzuri hapa jijini ajue thamani halisi ya Simba, ni kumtwisha mzigo sui wake!!
Sawa kabisa mkuu Baba Kiki nafurahi kwamba umelisoma bandiko na umeelewa. tafashali niambie sehemu ambayo sijatosheleza maelezo nifafanue kwa kina. Mimi nimefanya utafiti mrefu na wa kina juu ya mifumo yote. Nawakaribisha kama mna maswali ya msingi mkuu
 
Simba wanaelewa wanachofanya

Yanga hata hawajui wanafanya nini....wamekurupukaaaaaaa
 
Simba wanaelewa wanachofanya

Yanga hata hawajui wanafanya nini....wamekurupukaaaaaaa
Mkuu labda ungefafanua zaidi. Ni kwa vipi yanga hawajui wanachofanya na Simba wanajua.Fafanua.
 
Hili swala watu wanaliongelea kiushabiki kila mtu akivutia kwake kwa hiyo hata kwa wale wasioelewa kweli wanashindwa kujua yupi ni bora mo au manji
 
Mkuu labda ungefafanua zaidi. Ni kwa vipi yanga hawajui wanachofanya na Simba wanajua.Fafanua.

Mchakato wa Simba umekuwa shirikishi sana na unapelekwa Proffesionally

Wanachama sasa kwa miezi sita wanaingia katika phase ya kupewa elimu

Then mabadiliko ya katiba yatafanyika

Then valuation ya timu pamoja na determination ya share Price itafanyika ndani ya hiyo miezi sita

Jana imekubaliwa kuwa Memorandum of Understanding itasainiwa ndani ya mwezi mmoja kutoa room ya kufanya process zingine.

Simba hakuna conflict of interest.....MO yuko nje ya kamati tendaji ya timu hivyo anatoa room ya process hii kuangaliwa kiumakini bila yeye ku influence decision.

Simba wanaelewa wanachofanya kwa sababu wao ndio walianza hii process..wiki moja baadaye manji kakurupuka na kuita kikao cha dharura pasipo kiongozi yeyote mwenzake kujua ni nini kinaenda kujadiliwa

Simba ilishaanza mjadala wa kubadili mfumo muda wa miaka miwili iliyopita kabla ya mkutano mkuu uliopita ...tofauti na Yanga walioambiwa ndani ya dakika kumi...wakakurupuka na kuanza kushangilia
 
Yanga bana nyie mpeni uyo kwa miaka 10 ndo mtajua faida yenu sisi acha tule bil20 na 49% baada ya iyo miaka 10 ndo mtajua simba iko wapi na nyie mko wapi
 
Ngoja nmpge ng'ombe alie moooo
Ha ha ha
Jangwan ulipita upepo wa vumbi tuu ila leo n upepo wa neema ya ngao ya jamii
Naipenda Yanga
 
Mchakato wa Simba umekuwa shirikishi sana na unapelekwa Proffesionally

Wanachama sasa kwa miezi sita wanaingia katika phase ya kupewa elimu

Then mabadiliko ya katiba yatafanyika

Then valuation ya timu pamoja na determination ya share Price itafanyika ndani ya hiyo miezi sita

Jana imekubaliwa kuwa Memorandum of Understanding itasainiwa ndani ya mwezi mmoja kutoa room ya kufanya process zingine.

Simba hakuna conflict of interest.....MO yuko nje ya kamati tendaji ya timu hivyo anatoa room ya process hii kuangaliwa kiumakini bila yeye ku influence decision.

Simba wanaelewa wanachofanya kwa sababu wao ndio walianza hii process..wiki moja baadaye manji kakurupuka na kuita kikao cha dharura pasipo kiongozi yeyote mwenzake kujua ni nini kinaenda kujadiliwa

Simba ilishaanza mjadala wa kubadili mfumo muda wa miaka miwili iliyopita kabla ya mkutano mkuu uliopita ...tofauti na Yanga walioambiwa ndani ya dakika kumi...wakakurupuka na kuanza kushangilia
Mkuu
1. Sikubaliani sana na IMANI YAKO kwamba Yanga inakurupuka- As a matter of fact mchakato huu ulipendekezwa Yanga 10+ years ago
2. Manji anachoungumza sasa baada ya kuibeba sana Yanga single-handedly ni kuifanya isimame kwa miguu yake. Kuna leo na kesho
3.Mo ananunua timu. Maandalizi ya mchakato wa Simba lazima uwe mrefu kwasababu there's no turning back.
4.Manji anakodisha timu, analeta proposal in no time wenye timu wakikubaliana na dau na muda zinawekwa procedure.
Sasa naomba nikukumbushe
a) Mo amekuja kununua Simba (being a major share holder tena kwa kuuziwa 51% shares at the rate of Tshs 20B ina maana wanasimba wengi hawataweza kuweza kununua atleast 1% ya shares)
b)Mo amekuja na technocrats wake na hata mikataba inajadiliwa kwake (premises) una uhakika gani hana interest
c)Umesahau yaliyotokea kwenye mkutano wa Simba wanachama hawakutaka hata kusikia kuhusu kingine walivyofika kwenye topic ya process. What is the difference?
d)Manji amegharamikia billions kwa ajili a Yanga as a chairman(through up&downs) ; Mo alivyoona timu imeyumba akaenda nunua Africa Lyon. Mbona hamuanzi kuogopa kua atawaambia tumefilisika tugawane mali tuvunje kampuni?
 
· Manji anaingia ubia na Yanga na kuamua kuchukua asilimia 75 ya mapato huku akiiachia klabu asilimia 25 na kubeba hasara yote. Kumbuka Mzigo wa gharama zote pamoja na hasara za timu zitabebwa na Manji, Mishahara pamoja na gharama zote za uendeshaji zitabebwa na Manji na baada ya miaka 10 timu itabaki kuwa mali ya wanachama huku akiwa amependekeza kama ni suala la kiwanja yeye hatopenda kijengwe nje ya mji kwakuwa watazamaji hawajitokezi pindi kiwanja kinapokuwa nje ya mji na kama wanachama wataridhia basi kwahiyo asilimia 25 itakayopatikana ataitumia kujenga uwanja kama wengi walivyopendekeza katika mkutano wa dharula uliofanyika Diamond Jubilee. Anachotaka Manji ni kuiendesha klabu kwa mfumo wa kibiashara kitu ambacho timu zetu zimeshindwa kufanya kwa Zaidi ya miaka 80.

· Mo’ Dewji kwa upande wake anafanya ujanja ujanja anaichukua Simba BURE kwa kudai anainunua timu kwa bilioni 20 huku akiitumia pesa hiyohyo kununua treasury bonds (hisa za serikali kisha mapato yatokanayo na faida ya kununua hisa hizo za serikali, atagawana na klabu na kuchukua asilimia 51 ya faida hiyo huku akiipatia Simba asilimia 49 wakati huo huo akiwa ameinunua timu. Ikumbukwe Hanspope kwa sasa ana hali mbaya kifedha toka sakata la sukari lichukue sura mipango yake ya kifedha imeenda kombo, Kaburu alikuwa anategemea mchongo wa kibali cha kuingiza mbolea ambacho alijipatia uwakala wa Afrika Mashariki na kati na hakuna mbolea iliyokuwa inaingia hapa nchini bila kupitia kwake, huo ujanja ujanja kwa Magufuli umekwisha nae ana hali mbaya kifedha, Aveva sio siri huyu alikuwa mfanyakazi wa Mo’ na alikuwa Mo’ Foundation.

Kwahiyo kwa hili ni wazi kuwa Mo’ amewaingiza mkenge wana Simba kiujanjaunja MILELE na hii yote inatokana na kuhujumu timu ifanye vbaya ili washabiki wasiingie uwanjani ili ikose mapato na nguvu ya ushindani ili kipindi anajitokeza na dau lake aonekane kama Mungu mtu na muokozi wa timu na kiukweli dhamira yake imefanikiwa mpaka sasa. Na ukizingatia yeye ni mwanasiasa akaongeza na nguvu ya wanasiasa wapenda dezo ili kuipigia makelele ishu ya Manji na Yanga ambayo wanachama wamebariki kwa asilimia 200 ili suala lake la kuwalaghai wanasimba lipite bila kelele.

Wote tumeona jinsi mkuu wa mkoa alivyoshikwa mabega uwanja wa taifa na kulishwa keki siku ya Simba Day wakiashiria kubariki ulaghai huo ila chakushangaza baada ya kushiba keki Makonda kaanza kushikilia bango suala la Yanga na Manji akielewa fika kuwa Mo ataumbuka endapo watanzania watagundua utapeli anaofanya Mo.

· Ikumbukwe bilioni 20 alizotoa Mo ni bei aliyojiamulia yeye bila kuweka wazi vigezo alivyotumia kufikia kwnye uamuzi wa kutoa dau hilo, Simba ni timu na inavitega uchumi. Kwahiyo kununua asilimia 51 za hisa ni kujipa umiliki wa mali zote za klabu. Ni Dhahiri kwamba bei ya hisa za timu itapanda baada ya uwekezaji hivo ni wazi kabisa hapo baadae hakuna mwanachama ambaye atakuwa na uwezo wa kununua hisa za timu, Mo atarudi tena na wazo la kumalizia sehemu za hisa hivyo basi kuwa mmiliki wa asilimia 100, wakati upande wa pili Yanga itabaki na mali zake zote yani timu na vitega uchumu vya klabu; Jangwani na nyumba ya Mafia.
View attachment 382720
#YangayetuSimbayake
Sasa ndio umeandika nini hapa,unatuharibia taaruma zetu,kama una degree yoyote kajichungulie form four ulipata nini!huwezi kusema mtu ananunua hisa 51% kwa billion 20 unasema kapewa bure bora aliekodi?unajua kila kitu unachosikia Mo anaongelea kipo dunia nzima,kasome Company law alafu uniambie alichofanya Manji mpaka sasa wasomi wote wameshindwa kumuelewa maana kwenye form ya partnership hakuna kukodi kwenye share hakuna stahili hiyo,alafu unakuja mbele ya wanaume unaongea ongea utumbo,kama jambo hujui kwani lazima uandike,nyie ndio mnaofanya sisi wasomi wachache tudharaulike kwa upumbavu wenu humu,kaa uliza watu hivi alichofanya Manji na Mo kunatofauti gani au kuna fanana katika kipi,wanaojua mambo watakuja hapa wakupe shule,usikulupuke tena dogo.
 
Back
Top Bottom