Tetesi: Yusuph Manji ndiye Meya wa Jiji la Dar ajaye

Status
Not open for further replies.
Ukumbuke CUF kuna kizungumkuti, anaweza kugawa faranga kwa UKAWA, halafu ukashangaa ni meya wa jiji
UKAWA unaowaona wameshinda ubunge basi walikataa hongo ya kijani, wale ni wazalendo. Ninadhani umenielewa.
 
Tatizo lako kijana unafikiri kwa kutumia ........... Usikurupuke kama mtu aliyefumwa akijisaidia shambani. CUF weshatangaza kujitoa nakura zao ni muhimu katika huo uchaguzi au hukusikia tangazo lao? Pole sana.
 
Tatizo lako kijana unafikiri kwa kutumia ........... Usikurupuke kama mtu aliyefumwa akijisaidia shambani. CUF weshatangaza kujitoa nakura zao ni muhimu katika huo uchaguzi au hukusikia tangazo lao? Pole sana.
Ww Endelea KUKARIRISHWA Tu Na Propaganda Za Lumumba!! Alafu Usidhani Humu Kuna Vijana Pekee!! Mi Sio Kijana Kama Unadhani Ww!! Naelewa Vyema Ninachokisema!! Ww Endelea Tu KUKARIRI Matamko Ya Propaganda Na Huyo Muhindi Wako!! Jiji Hili This Time Ni Ngome Ya UKAWA!!
 
Mwaka huu mabmo yalivyopigwa KATA FUNUA hata huyu Manji hana hamu na huo udiwani yale mambo ya kuishi kijanjajanja yameondoka na mkwere wavaa kijani ndio wanao ISOMA NAMBA sasa, huo umeya utakuwa mzigo tu kwake hataweza kuupigia dili tena na lile la ufukwe alilotaka kujimilikisha limebuma.
 
Labda kule porini kwenu Mbagala lkn sio huku mjini kwetu kwani lazima atuambie katokea wapi na uFISADI wake uwe wazi! Meya ni ukawa baba hapa sio kwa wahindi matapeli!
 
Naona Magufuli katoa indirect warning to CCM mkishindwa kubalini kushindwa.Nadhani Mzee kaambiwa Manji ndiyo Mgombea wa Umeya.Kazi ipo.
 
binafsi napinga sana huu utaratibu wa kuwaendekeza hao wahindi kwenye siasa eti kisa tu wana hela. hayo ya wabunge wa morogoro na sehemu zingine imetosha.
Acha ubaguzi na wivu wa kijinga, hawa ni watanzania na wana haki kama mtanzania yeyote, kama ana sifa ya kugombania nafasi yeyote ana haki ya kugombania kama mwananchi yeyote, siyo umuhukumu kwa rangi, kabila, au dini yake.
 
inawezekana si anafedha nini kitashindikana kwa mtu mwenye fedha nini kitashindikana ndani ya CCM?
KIFO TU NDO TUNAFANANA NA HAWATAKIKWEPA KAMA WALIOCHANWA BAGAMOYO,,MADEREVA WOTE WALALE SALAMA,,WRONGLY PLACE AT THE WRONG TIME WITH WRONG PEOPLE...WAPATE FARAJA WAFIWA,,INILLAH INILLAH
 
Ni nani ajuae, labda ile kauli iliyotolewa pale magogoni ya watu kujimilikisha fukwe na kufutwa mkataba wa umiliki ndio jamaa anataka ajibu mapigo kwa kuonyesha kuwa ana nguvu zaidi ya alivyotarajiwa. Lakini huyu jamaa akiwa meya itakuwa aibu sio kwa dsm bali taifa zima, na kama udiwani uliwezekana basi hakuna cha ajabu kwa umeya pia!
 
Huyu jamaa chizi nimemvulia kofia. alisema kuwa Dr Slaa ni mnafiki kama sikosei mwaka juzi akataja udhaifu wake ikawa kweli. akasema lowassa hatokuwa Rais tulimponda sana ikawa kweli. akasema Manji anataka Udiwani then Umeya. Kweli manji akagombea udiwan Hii ni post ya mwaka 2013 July. na ninavyoona sasa inawezekana Manji akawa Meya kama Mkuu wa Nchi asipoingilia. Maana jamaa anasema mhusika anajipanga sana.
 
Kwa ticket ya Chama gani ACT au Ccm maana naona UKAWA kwa mahesabu wako juu.
 
alieturoga watu wa Morogoro, alituweza sana!
binafsi napinga sana huu utaratibu wa kuwaendekeza hao wahindi kwenye siasa eti kisa tu wana hela. hayo ya wabunge wa morogoro na sehemu zingine imetosha.
 
Meya wa jiji hajuwi kiswahili?Labda jiji la mumbai india
MBONA AMIR JAMAL NA ALNOOR KASSAM WALIWAHI KUWA WAZIRI WANDAMIZI TU WAKATI KISHWAHILI CHAO AFADHALI YA MANJI? WACHA UBAGUZI USIO NA MAANA. DIWANI YOYOTE YULE NI MEYA MTARAJIWA
 
Manji huyu huyu aliyeiuzia Matela mabovu Manispaa ya Kinondoni Na Mh.Lukuvi akiwa Mkuu wa mkoa wa Dar akagoma kuyazindua? Kweli CCM in ile ile Rais Magufuli huyu Yusuf Manji Hafai Tuma wasaidizi wako Mwananyamala watakuta hilo Jipu au mwulize Lukuvi
 
Acha ubaguzi na wivu wa kijinga, hawa ni watanzania na wana haki kama mtanzania yeyote, kama ana sifa ya kugombania nafasi yeyote ana haki ya kugombania kama mwananchi yeyote, siyo umuhukumu kwa rangi, kabila, au dini yake.
Acha kujipendekeza kwa ajili ya njaa zako wewe nenda basi india ukagombee udiwani uone kama utapata kama hutaishia kukatwa shingo kama ndugu zetu wa kitanzania wanavyo uwawa huko
 
Post hii sikuiona wakati huo ila haiwezi kupita bila kuungwa mkono maana bado inaishi yaani iko hai. Ni kweli Watanzania wengi ni mbumbumbu na hawataki kujishughulisha kuelewa. Lakini hao hao ndio tunawaona humu maneno meeengi na too much know.
 
Acha kujipendekeza kwa ajili ya njaa zako wewe nenda basi india ukagombee udiwani uone kama utapata kama hutaishia kukatwa shingo kama ndugu zetu wa kitanzania wanavyo uwawa huko
Hilo ndiyo tatizo la kuishi saana Tanzania bila kutoka ukaona ulimwengu, unataka kuniambia ikiwa India wanafanya makosa basi na sisi tuwafuate, sisi tunatakiwa tuende na wakati na tuige mifano ya nchi zilizoendelea ili tuendelee na kwenda na wakati, sio kutizama yanayofanywa na India nchi inayoendelea kama sisi, tutaganda hapa tulipo na watu wenye mawazo kama yako.
Hivi sasa Uingereza katika mji wa London kuna nafasi kubwa ya mhindi Khan kushinda Umeya, wao hawatizami kingine zaidi ya uwezo wa mgombania na uraia wake na hizo ndiyo nchi za kuigwa mifano yao.
 
Huyo manji anauwezo gani zaidi ya kutuibia?
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…