Yusuph Mwenda: Kati ya watanzania Milioni 62, wanaolipa kodi ni Milioni 2 tu

Yusuph Mwenda: Kati ya watanzania Milioni 62, wanaolipa kodi ni Milioni 2 tu

ChoiceVariable

JF-Expert Member
Joined
May 23, 2017
Posts
66,537
Reaction score
75,687

Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Yusuph Mwenda amesema Tanzania yenye idadi ya watu zaidi ya milioni 60 lakini walipa kodi hawazidi watu milioni 2 jambo ambalo linasababisha watu hao wachache wanaolipa kodi kulazimika kubeba mzigo mkubwa na hivyo wakati mwingine kusababisha malalamiko ambayo kwenye mazingira ya kawaida yangeweza kuepukika​

Akizungumza katika wa kikao kazi kilichowakutanisha TRA na viongozi wa wafanyabiashara Tanzania chini ya uratibu wa TPSF kilichofanyika Johari Rotana Hotel jijini Dar es Salaam leo, Alhamisi Julai 18, 2024 Mwenda aliyeteuliwa kushika nafasi hiyo hivi karibuni amesema mkakati alioingianao ofisini kwa sasa ni kuhakikisha namba ya walipa kodi inaongezeka nchini.

Pia soma hapa Tunduma: Rais Samia Awataka Wafanyabiashara Walipe Kodi na Tozo kuepuka mikopo. Asema Haziendi Kwenye Mifuko ya Viongozi

Kamishna Mkuu wa TRA bwana Yusuf Mwenda amewataka Wafanyabiashara wasirubuniwe na maofisa wachache wahuni wa TRA

====

My Take
Population structure ya Tanzania ni Pyramid in shape, tuna kundi kubwa la Vijana ambao sio wazalishaji Bali wategemezi.👇👇

Tunawatu milioni 2 kati ya milioni 62 wanaolipa kodi Tanzania. Sasa Kuna mzigo mkubwa unaobebwa na watu wachache halafu kusapoti zaidi ya asilimia 98 ambao hawalipi kodi na katika hao milioni mbili sio kila mmoja analipa kodi kila mwezi. Hivyo tulikaa chini ili kuona ni jinsi gani tunaweza kurahisisha usimamizi wa ulipaji kodi ili kuvutia walipaji kodi wengi na hata kupunguza baadhi ya viwango ambavyo hawa watu wanazilipa.

Tulishauri tuwe tunakaa kila robo ya mwaka ili kuhakikisha tunafanya assessment ya mazingira ya biashara hasa katika usimamizi wa mambo ya kodi" - Raphael Maganga - Mkurugenzi Mtendaji TPSF
 
Labda angesema direct tax ila indirect tax tunalipa wote mfano kwenye luku kila mtu anakatwa kodi, kununua bando la simu unakatwa kodi, kununua soda unakatwa kodi maana VAT ni shift able na tunaoilipa ni watumiaji wote wa mwisho.

So direct tax wanalipa million 2 ila indirect tax wanalipa zaidi ya million 30.

Kingine watu million 62 hawazalishi, mind you zaidi ya 50% ya waTanzania ni under 18 yaani watoto. So ilipaswa takwimu zake ziwe kwenye labor kwamba watu wangapi wanaozalisha hawalipi kodi. Utakuta wenye kazi au biashara ni million 10 pekee so takwimu zinakua tofauti na ukitoa general population
 
Aisee,Sasa wale Wanasiasa wanaotoa matamko ya kuwaruhusu machinga kupanga bidhaa zao katika Barbara za miji huku wakijuwa hawalipi Kodi,maslahi Yao Huwa ni nini ?
Watanzania hamtaki kulipa Kodi ila mnadai maendeleo sijui mnayegemea yatatokea wapi.

Serikali ikikopa mnasema inakopa sana.

Serikali ikiwabana watu Walipe Kodi mnasema inawaonea , yaani hii Nchi Kila kitu lawama
 
safi sana,

mee.jpg
 
Labda angesema direct tax ila indirect tax tunalipa wote mfano kwenye luku kila mtu anakatwa kodi, kununua bando la simu unakatwa kodi, kununua soda unakatwa kodi maana VAT ni shift able na tunaoilipa ni watumiaji wote wa mwisho.

So direct tax wanalipa million 2 ila indirect tax wanalipa zaidi ya million 30.

Kingine watu million 62 hawazalishi, mind you zaidi ya 50% ya waTanzania ni under 18 yaani watoto. So ilipaswa takwimu zake ziwe kwenye labor kwamba watu wangapi wanaozalisha hawalipi kodi. Utakuta wenye kazi au biashara ni million 10 pekee so takwimu zinakua tofauti na ukitoa general population
Sio Kila mtu,kaya ziko ngapi?
 
Kamishna Mkuu wa TRA bwana Yusuf Mwenda amesema Anakerwa na kushangaa sana Nchi kuwa na idadi ndogo ya walipakodi licha ya kuwa na watu zaidi ya mil.62 ikiwa ni Nchi ya 5 Kwa Wingi wa watu Afrika.👇👇

View: https://www.instagram.com/reel/C9j3xwGqyB-/?igsh=ZmV2N3h5aXF5b2Ew

My Take
Population structure ya Tanzania ni Pyramid in shape ,tuna kundi kubwa la Vijana ambao sio wazalishaji Bali wategemezi.

View: https://www.instagram.com/p/C9mAfWGtK5h/?igsh=bWlvOTgxeDh5OW9q

Ili wanunue ma V8?
 
Asishangae sana, maana hata serikali yake haijaajiri hata watu milioni moja. Yaani unashangaaje wakati wewe mwenyewe hujakidhi vigezo vya kulipwa direct tax?

Penye umasikini usitegemee upate walipa kodi directly hata 10% coz wengi ni tegemezi. Ajiri watu, tengeneza fursa za sekta binafsi kuajiri, tengeneza fursa kwa sekta isiyo rasmi watu wajiajiri na wape mikopo ili waweze kuwa na biashara za kati na juu.

It's foolishness kushangaa walipa kodi wa moja kwa moja 2m tu wakati wewe mwenyewe hujaajiri hata watu 1m kati ya watanzania wote.
 
Labda angesema direct tax ila indirect tax tunalipa wote mfano kwenye luku kila mtu anakatwa kodi, kununua bando la simu unakatwa kodi, kununua soda unakatwa kodi maana VAT ni shift able na tunaoilipa ni watumiaji wote wa mwisho.

So direct tax wanalipa million 2 ila indirect tax wanalipa zaidi ya million 30.

Kingine watu million 62 hawazalishi, mind you zaidi ya 50% ya waTanzania ni under 18 yaani watoto. So ilipaswa takwimu zake ziwe kwenye labor kwamba watu wangapi wanaozalisha hawalipi kodi. Utakuta wenye kazi au biashara ni million 10 pekee so takwimu zinakua tofauti na ukitoa general population
wastahili maua kwa lugha ya mitaani lakini kwangu mimi nikikupa maua tutaharibu chakula cha wadudu wakiwemo vipepeo na nyuki tukakosa asali na kusababisha eti serikali ikose kodi kwa maua tuliyokupa.
hawa jamaa wanafikiri huku mtaani bado kuna vilaza kama juzi!? ikiwa D mbili na wenyewe wamekuwa interictal
 
Hivi hii ni kodi gani wanayozungumzia?
kuna PAYE kwa mfanyakazi
Kuna ushuru wa mazao kwa mkulima
kuna ushuru kwa mfugaji
Kuna kodi kibao kwenye LUKU
Kodi kibao kwenye petrol
Wafanyabiashara nao wana kodi zao...
Sasa hapa anasema ipi hailipwi?
 
Back
Top Bottom