Zacharia Isaay (Mbunge Mbulu): Serikali iache kigugumizi ieleze wazi kuhusu ugonjwa wa kupumua unaomaliza watu wa Mbulu

Mbunge huyo badala ya kufukuzwa anaweza kutumika kumsafisha dikteta; na kuwa njia ya kutoka na kumtafuta wa kumlaumu

Atatangazwa kuwa ni shujaa, na hapo hapo dikteta kuanza kujipamba jinsi anavyowapigania wanyonge wake wasiangamizwe na korona.

Atatafutwa Bangusilo mmoja wa kafara na nyimbo za kumsifu dikteta zitaimbwa kila sehemu kuwa shujaa wa taifa lake.

Hiyo ndiyo kawaida ya madikiteta duniani kote.
 
Mtaalam katembelea hospitali zote ila Mbunge katembelea hospitali moja lkn wewe unamuamini Mbunge kuliko Mtaalamu maana unachopenda kukisikia kikufurahishe ni hicho cha Mbunge
 
Mkuu mbunge,

There's nothing you can do,

Rather wasting time ku argue na serikali ambayo imeamua kukaa irresponsible..

Effort/nguvu zako zielekeze kwa wananchi wa jimbo lako..

Piga kelele wananchi wako wafate guidelines;kuosha mikono, kuepuka misongamano etc

Cha pili piga kelele watu wale vyakula na dawa zinazo boost immunity
 
Halafu akitoka kuzika wapiga kura wake anarudi bungeni anajiunga na wenzie bungeni bila kuvaa barakoa
 
Mtaalam katembelea hospitali zote ila Mbunge katembelea hospitali moja lkn wewe unamuamini Mbunge kuliko Mtaalamu maana unachopenda kukisikia kikufurahishe ni hicho cha Mbunge
Mtaalam alikwenda kuwazika wapiga kura wa mbunge?

Mtaalam yupi unayemzungumzia, yule waziri wa Afya au Katibu mkuu wake?

Hivi nyinyi watu, humo vichwani mwenu mmejazwa matope?

Hata kufikiri tu kama binaadam wa kawaida hamuwezi?
 
Hata Naye ni kati ya waoga,watu wanafariki kwa matatizo ya kushindwa kupumua kwa Tanzania pekee Bali kwingineko duniani wanatoa Diagnosis ya COVID 19 ambapo hata vyombo vyetu vya habari vinawatangaza hadi majina wanaofariki.
Tujiulize wanaojifukiza na kunywa dawa za miti shamba tunaambiwa zinawasaidia,ni ugonjwa gani wanaotibu?Hatuambiwi ukweli!Kuna nini kinafichwa hadi ventilators haziwatoshi?
 
Kusema kitu ambacho kiko wazi ni ujasiri? Mbona tunashusha viwango wa mtu kuitwa jasiri namna hii? Tanzania watu wanatetekea kwa corona. Mtu akisema watu wanakufa kwa corona (jambo ambalo ni kweli ) ni ujasiri? Tena basi ameogopa hata kuutaja ugonjwa! Tuache woga ndugu zangu.
 

Mkuu kwa hali iliyopo hakuna haja ya kukaa kimya MDUDU hana macho anapiga yeyeote ,kila mtu yupo kwenye risk ya kupata FUTA.

Nampongeza pia kwa ujasili wake wa kutoa makavu live.
 
Kajitoa SADAKA NA NAMPONGEZA LAKINI PIA NAMWONEA HURAMA MAANA ATAITWA NA CHAMA
 
"mwambieni huyo mbunge asijisahau....asinichokoze.....mkumbusheni kuhusu namna ubunge wake ulivyopatikana"
Tutatafuta namna ya kusawazisha mambo kama tulivyomfanyia msukuma kwa kwenda kuzindua soko huko morogoro wakati juzi alisema miradi mingine haina tija
 
Mwanzoni mwajanuary Mheshimiwa Mbowe alitoa angalizo kwa rais kuhusu hili jinamizi la covi19, lakini aliambulia matusi yote toka vijana wa mataga na uvccm
 
Halafu akitoka kuzika wapiga kura wake anarudi bungeni anajiunga na wenzie bungeni bila kuvaa barakoa. Kazi ipo
Now you can see how naive and stupid most people are. Na watu watakwisha kwelikweli maana kama tunasubiri matamko, tutasubiri sana

Tamko la Chief Medical officer ni kwamba mnapaswa kuanza desturi ya kunawa mikono na kufanya usafi kwa ujumla ili msipate kipindupindu na Typhoid🙂
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…