misasa
JF-Expert Member
- Feb 5, 2014
- 14,244
- 10,073
Hapa ndio NGAO yake ilipokuwepo mkongomanMkimfukuza mna hela za kumpa?
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hapa ndio NGAO yake ilipokuwepo mkongomanMkimfukuza mna hela za kumpa?
Yanga wajeuri huu ni ukweli mtupu kabisa ameongea mzee wangu ZaheraKocha wa Yanga, Mwinyi Zahera amesema kuwa hawezi kuwasikiliza mashabiki wanachokisema kwa sasa baada ya kufungwa na Pyramids FC bali anawasiliana na uongozi ambao ulimpa mkataba.
Hayo yamekuja kufuatia mashabiki wa klabu hiyo kutoa malalamiko yao wakimtaka Zahera kuondoka kutokana na matatizo wanayosema yamekithiri kwenye kikosi ikiwemo kushindwa kupanga vizuri kikosi cha kwanza pamoja na mbinu.
"Mimi sikuajiriwa na mashabiki wa Yanga bali nilisaini mkataba na viongozi, kwahiyo siku viongozi wakinitaka kiwaachie timu nitafanya hivyo, sitokwenda mazoezini", amesema Zahera.
"Nina uzoefu mkubwa ila hapa Afrika, mashabiki wanakasirika. Hakuna mchezaji yoyote wa Yanga anayeweza kucheza Pyramids FC na lingine ni kwamba wakati tunasajili wachezaji, hatukusajili kwa ajili ya Klabu Bingwa Afrika ila tulisajili kwa ajili ya ligi", ameongeza.
Aidha Zahera amesema kuwa mashabiki hawapaswi kumlaumu yeye kwa matokeo ya Klabu Bingwa kwani kikosi chake kiliandaliwa kwa ajili ya ligi kuu, ambako hawapo katika nafasi mbaya mpaka sasa, wakiwa wamecheza mechi chache.
Yanga inatarajia kusafiri hadi nchini Misri kuvaana na Pyramids katika mchezo wa marudio utakaopigwa wikiendi hii, ikiwa nyuma kwa kufungwa mabao 2-1.
Kocha mkweli sana huyu. Msimu uliopita tuliona Timu inashindwa hata kulipa mishahara ya wachezaji, hadi kina Dante hadi leo wapo mtaani. Usajili ulifanyika kabla ya CAF haijatupatia nafasi 4 za ushiriki wa timu zetu. Yanga mkimtimua kocha Zahera laana yake itawaandama.
Mimi ni mmoja WA watu waliokuwa wakimuamini Sana zahera,lakini sasa nimeamini huyu kocha ni porojo mingi hii ni timu kubwa na hakikuandaliwa kwa ajili ya ushindi WA ligi ya ndani tu tunaitaji ushindi,asituone tunambabaikia ........
Ngoja nikagugo Mtani. 🚶♂️🚶♂️🚶♂️
Kocha mkweli sana huyu. Msimu uliopita tuliona Timu inashindwa hata kulipa mishahara ya wachezaji, hadi kina Dante hadi leo wapo mtaani. Usajili ulifanyika kabla ya CAF haijatupatia nafasi 4 za ushiriki wa timu zetu. Yanga mkimtimua kocha Zahera laana yake itawaandama.
Hahaa...anakaa jukwaani kuwatuliza mashabikiHahahaaa aise hivi bondia molinga aliletwa kwa shughuli ipi hasa wadau
kwani zahera bado ni kochatu jmnKocha wa Yanga, Mwinyi Zahera amesema kuwa hawezi kuwasikiliza mashabiki wanachokisema kwa sasa baada ya kufungwa na Pyramids FC bali anawasiliana na uongozi ambao ulimpa mkataba.
Hayo yamekuja kufuatia mashabiki wa klabu hiyo kutoa malalamiko yao wakimtaka Zahera kuondoka kutokana na matatizo wanayosema yamekithiri kwenye kikosi ikiwemo kushindwa kupanga vizuri kikosi cha kwanza pamoja na mbinu.
"Mimi sikuajiriwa na mashabiki wa Yanga bali nilisaini mkataba na viongozi, kwahiyo siku viongozi wakinitaka kiwaachie timu nitafanya hivyo, sitokwenda mazoezini", amesema Zahera.
"Nina uzoefu mkubwa ila hapa Afrika, mashabiki wanakasirika. Hakuna mchezaji yoyote wa Yanga anayeweza kucheza Pyramids FC na lingine ni kwamba wakati tunasajili wachezaji, hatukusajili kwa ajili ya Klabu Bingwa Afrika ila tulisajili kwa ajili ya ligi", ameongeza.
Aidha Zahera amesema kuwa mashabiki hawapaswi kumlaumu yeye kwa matokeo ya Klabu Bingwa kwani kikosi chake kiliandaliwa kwa ajili ya ligi kuu, ambako hawapo katika nafasi mbaya mpaka sasa, wakiwa wamecheza mechi chache.
Yanga inatarajia kusafiri hadi nchini Misri kuvaana na Pyramids katika mchezo wa marudio utakaopigwa wikiendi hii, ikiwa nyuma kwa kufungwa mabao 2-1.
Amecheza game 4, amewin 2 amepoteza 1 droo 1 = POINT 7Hiyo ligi kuu amefanya nini kama alisajiri kwa ajil ya ligi kuu?
Muwe mnafuatilia habari kabla ya kuropoka.....Hahahaaa aise hivi bondia molinga aliletwa kwa shughuli ipi hasa wadau