Zaidi ya Tsh. Bilioni 30 zimetumika kuboresha Bandari ya Ujiji lakini inamezwa na maji, hali ni mbaya

Zaidi ya Tsh. Bilioni 30 zimetumika kuboresha Bandari ya Ujiji lakini inamezwa na maji, hali ni mbaya

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
11.jpg

BANDARI KIGOMA (3).jpg
Miaka ya hivi karibuni Serikali ilitangaza kuanza kufanya maboresho ya Bandari ya Ujiji, sina uhakika na kiwango lakini niliona taarifa ya Serikali kuwa inatarajiwa kutumiwa Shilingi Bilioni 32.5 kuboresha bandari hiyo na nyingine ya Kibirizi ambazo zote zipo maeneo Jirani.

Mradi huo wa bandari mbili ulianza Mwaka 2019 na ulitarajiwa kumalizika Mwaka 2021 lakini baadaye yakafanyika mabadiliko na muda kuongezwa.

Sisi Wananchi wa hapa tukaanza kujua neema imekuja japokuwa tulikuwa na wasiwasi kuhusu bandari hizo kutokana na historia ya eneo hilo kuwahi kuwa sehemu ya Ziwa Tanganyika.
BANDARI KIGOMA (2).jpg
Viongozi kadhaa wa Serikali na wale wengine wa Kisiasa walifika kwenye miradi hii kufanya ukaguzi na wakaoneshwa kuridhika na kinachoendelea.

Ukipita eneo la Bandari zote hizo mbili kwa asilimia kubwa zipo ndani ya maji, kwa ufupi ni kuwa haiwezekani tena miradi kufanyika.

Inawezekana wanaweza kusema kina cha maji kimeongezeka lakini hilo walitakiwa kulijua mapema, wao ni wataalam kuliko mimi raia wa kawaida.

Hali ilivyo kwa sasa ni mbaya na wengi wetu tumelazimika kukimbia maeneo yote ya karibu na Bandari, maji amekuwa mengi.

Ninachokiwaza zile bilioni 30+ zilizotengwa kwa ajili ya maboresho inamaana ndio zimepotea hivyo?

Mimi sio Mkandarasi ila akili ya kawaida ilitakiwa kutumika, hapo ninavyoona kuna mambo mawili, inawezekana utafiti haukufanyika kwa usahihi, ndio maana mambo yameharibika au ulifanyika lakini Wakandarasi wakapuuzia utafiti na historia ya sehemu hiyo kujaa maji.

1.jpg

GY3A9963.jpg

Ilivyokuwa wakati wa ziara ya Kinana, Tarehe 1, Steptemba 2022
Pia soma
~ Bandari ya Ujiji imedumaa tofauti na matarajio yetu wana Kigoma Ujiji
~ Kinana akagua mradi ujenzi wa Gati la Bandari ya Ujiji Mkoani Kigoma, Septemba 1, 2022
~ Rais Samia aweka Jiwe la Msingi Mradi wa ujenzi Makao Makuu ya Bandari ya Ziwa Tanganyika, Oktoba 18, 2022
 
Kunachangamoto za hali ya mabadiliko ya hali ya hewa
Ziwa tanganyika limefurika na hata Victoria
 
Picha
 

Attachments

  • JamiiForums1192137444.jpeg
    JamiiForums1192137444.jpeg
    41.6 KB · Views: 9
Back
Top Bottom