Zama za Kilimanjaro Express zimeisha

Zama za Kilimanjaro Express zimeisha

Wapo hovyo sio uongo...
Hayo luxury nilipanda siku moja walisema iko na choo ndani kumbe ni haja ndogo tu... Sasa kuna mwanamke mmoja akafanya kubwa badala ya ndogo Aisee gari zima ilinuka safari ilikuwa chungu sana na watu walikuwa wanalalamika mno kuna harufu kali ndani..wakiwasha ac ni kama wanasambaza harufu tulikuwa tunasafiri kama tupo ndani ya choo tena ambacho hakiflash
 
Aisee uliichosema ni ukweli 100%. Nilikuwa nikisafiri Dar-Ars sipandi basi lingine tofauti na KLM. January nimesafiri na basi lao T 860 BVA limechoka mnooo, tangu hapo sina hamu na KLM tena.

Basi zina miaka 15 barabarani hiyo ni faida kwake, lakin kwa mimi abiria nipande ya nini wakati zipo Yutong na Zhongtong Upgrade mpyaaa

Sawaya abadilike kuendana na soko, watu wanashusha mchina wanatumia miaka 2 wanauza wanashusha mpya unakuta kampuni ina gari mpya kila siku mfno, Shabiby & BM. ila huyo jamaa anakomaa na zile APD, ASM, AXR, AWY miaka na miaka atleast zile G7 DHY & DMH
 
Achana kipengele cha AC nenda na hoja ya msingi, Dar maridi itoke wapi, wewe ulipokuja umetukuta tunatembea na makoti mchana kutwa kama huko.
Usiwe mkali basi jombaa🤣🤣🤣🤣 kwani umelipa shilingi ngapi? Kama ni 35k mi saivi haifiki sa6 nshaichoma kiberiti bar
Supu7k
Bia kumi Heineken 30k nyama choma au kuku nusu 9k kwa Dodoma
So tulia nextime panda BM
😅😅😅
 
Hapo mdau lazima atakuwa aliondoka na bus la saa 12 alfajiri, makampuni yenye mabasi mengi huweka magari ya zamani routes za alfajiri wakijua kabisa mteja huna option hasa kwa njia ambazo kuna gari kuanzia asubuhi mpaka mchana alafu za kuanzia saa 1 asubuhi na kuendelea ndio unakutana na michuma ya maana
 
Tatizo la nchi yetu bado ni lilelile la kwenda na ulimwengu wa Analogia wakati dunia iko Digitali.

Mi nadhani wizara ya uchukuzi ingeanzisha utaratibu wa Application au vipeperushi ambavyo vinakuwa vinaonyesha mikoa husika na aina ya ma-bus yanayoelekea huko.

Kwa mfano:

MKOA WA KILIMANJARO

LUXURY BUSES NA HUDUMA NDANI YA BUS

1.TILISHO - AC,WI-FI, etc.

2.BM - AC,WI-FI,VINYWAJI VYA AINA ZOTE.......etc

3.KIMBINYIKO -..........................

SEMI LUXURY BUSES

1.TILISHO - AC,HAKUNA WI-FI etc.

2.BM - WI-FI,HAKUNA AC WALA VINYWAJI

3.KIMBINYIKO - ....................

Huo ni mfano tu nimetolea na hivyo nisieleweke vibaya.

Sasa nadhani hii itaondoa ukakasi wa wale wapiga debe ambao huwa wanawajaza maneno mengi ya faraja abiria na ukiingia kwenye bus unakuta ni vice vesa,pia serikali kupitia wanaosimamia hayo ma-bus au usafirishaji abiria,unapoenda kukata tiketi kuwe kuna ulazima yule mkata tiketi akupe kitabu kitakachoonyesha aina ya bus na huduma zitolewazo na wewe unapaswa kulipia kile utakachokipenda.
Ili ukishalipa hiyo tiketi na ukapandishwa gari isiyokuwa na hizo huduma basi urudishiwe pesa yako na pesa ya kufidia muda wako.

Kinachotugharimu abiria wengi ni kwasababu hakuna mahali ambapo naweza kuona maelezo au taarifa zinazohusu hayo makampuni ya buses na huduma zitolewazo.
Kumbuka hakuna abiria anayependa kusafiri kwenda umbali wa kilometa nyingi kwa usumbufu na kero.

Taarifa ziwepo kuhusu hayo ma-bus na gharama husika ili kila abiria ajikadirie kwa uwezo wa mfuko wake,siyo nakuja stendi kukata tiketi nakuta bus limeandikwa ubavuni "luxury" na ukishapanda unakuta ni vice vesa.

Hebu tubadilike,tuache huu ubabaishaji wa kipumbavu.

Wao ngoja waendeleze huu ujinga na waendelee kuomba SGR isikamilike,lakini ikikamilika na ikafanya kazi kama tunavyoaminishwa,kiukweli ruti za ma-bus zitapungua,kwasababu siwezi kukaa kwenye bus kutoka Dar kwenda Mza kwa saa 17 wakati treni ni masaa 8 mpaka 10 tu.
Mkuu hakuna Luxury buses Tanzania kama wanavyozitaja.

Ni ile BM moja tu yenye seat nne mwanzoni za kuweza kuadjust na kulala comfortably na ina space ya kuweka food stuffs

Mengine yote ni matangazo tu...Mara Luxury, Mara semi luxury....hamna kitu.
 
Ngorika lipo siku hizi. Nakumbuka safari ya Kwanza toka dar to Moshi nilipanda basi linaitwa MBAZI sijui. Kwa kweli nilijuuuuuuuuuta, ndani gari ni siti 3 Kwa 2 afu ni zinabana miguu kama mtu ni mrefu nilijikuta nimekaa kupande toka dar mpaka nashuka moshi Kwa kweli nilijuta sana lile gari.
 
Back
Top Bottom