Zamani jina la Mgombea kiti cha Uspika lilikuwa mjadala kusubiri Moshi mweupe, Leo hii hata CCM hawataki kujadili kama agenda wamemwachia Mwenyekiti

Zamani jina la Mgombea kiti cha Uspika lilikuwa mjadala kusubiri Moshi mweupe, Leo hii hata CCM hawataki kujadili kama agenda wamemwachia Mwenyekiti

Beatrice Kamugisha

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2019
Posts
762
Reaction score
6,984
Nakumbuka enzi za Pius Msekwa, Sita na hata Makinda kidogo kulikuwa na mjadala mkali na mpambano wa fikra kuhusu qualities za mtu wa kushika Nafasi hii nyeti.

Ila Kwa miaka ya hivi Karibuni kiti Cha spika kimekuwa kama mchakato wa kumpata mwenyekiti wa Kijiji na siyo vijiji vyote.

Spika ameonekana kama katibu wa Chama, ameonekana kama mwenezi na wakati mwingine ameonekana kama kampeni meneji asiye na ukomo. Kiti Cha spika kimekuwa Mali ya yeyote atakayeonekana anafaa na Mwenyekiti wa Chama. Hakuna mjumbe anayeweza kutamka neno, hakuna wajumbe wanaoweza kuonyesha wanamuunga mkono nani Kati ya wachukua fomu, maana yake mwenye mamlaka ni mtu mmoja tu na huyo hakuna mwenye nguvu yakujadili wish yake.

Kwa mfumo huu hakuna spike Bali Kuna mwakilishi wa Chama kwenye Bunge. Kwa mfumo huu lazima anayeteua awe na mamlaka yakutengua, Kwa mfumo huu spika anakalia Kiti na kuendelea kukalia kiti pale TU mahusiano yake na Mwenyekiti yanapokuwa sawa . Wakikinzana wabunge wanategemea kupotishwa n mwenyekiti watamtoa Ili wapitishwe Tena.

VYOMBO vya habari vimejikiti kuripoti kinachotokea, havina mamlaka yakuchambua na kuonyesha wanaofaa, wao kazi Yao nikueleza kimetokea nn na hakuna kumkosoa mwenyekiti kwamba ameleta asiyefaa. Tuliona VYOMBO vya habari vikimsifia Ndugai kama Malaika, alipozingua tu vikaachana naye nakumpaka matope kama vile ni mpya kwenye uongoz kumbe alipoteza zamani dira ila tukamkalia kimya.

Tunakoelekea tutafika tumechoka Sana Kwa sababu tumeamua aliyepo sahihi siku zote ni mwenyekiti na atakosolewa pale TU atakapoachia kiti, vinginevyo hata afanye uovu vipi akiwa madarakani atutamsema Kwa sababu atatuma wasaidizi wake waje kutusaidia kujibeba
 
Zamani ulikuwa ni ushamba tu na kujitia uzalendo njaa tu ukiachilia mbali uhaba na ulasimu wa vyombo vya habari

USSR
 
For once,Beatrice anampinga rais.
Beatrice unaandika manylleno ya kihuni. "Kuzingua"
 
Zamani ulikuwa ni ushamba tu na kujitia uzalendo njaa tu ukiachilia mbali uhaba na ulasimu wa vyombo vya habari

USSR
Kna walewale kwenye Poli la zamani.
 
Chadema humu nyuzi nyingi ni kuhusu spika wa CCM na mapendekezo kibao

CCM baba lao nyie ajenda yenu hanna kazi kudakia tu matukio ya CCM
 
Ingekua Ulaya wapinzani wangetumia Mgogoro huu kuwaondoa CCM madarakani lakini Tanzania wao wanajadili ajenda za CCM aisee !!
 
VYOMBO vya habari vimejikiti kuripoti kinachotokea, havina mamlaka yakuchambua na kuonyesha wanaofaa, wao kazi Yao nikueleza kimetokea nn na hakuna kumkosoa mwenyekiti kwamba ameleta asiyefaa. Tuliona VYOMBO vya habari vikimsifia Ndugai kama Malaika, alipozingua tu vikaachana naye nakumpaka matope kama vile ni mpya kwenye uongoz kumbe alipoteza zamani dira ila tukamkalia kimya.
Mkuu Beatrice Kamugisha, hili la media ni kweli, Vyombo vya habari hatukutimiza wajibu wetu kikamilifu katika jukumu la kuhakikisha taifa tutapata Spika Bora.
Vibrant media ilipaswa kufanya analysis ya waliojitokeza ili kuonyeshea Spika Bora.
P
 
Aibu kwa taifa kuwa na watu zaidi 60M wajinga wote isipokuwa mtu mmoja tu anaendesha nchi kwa akili yake pekee
 
Ingekua Ulaya wapinzani wangetumia Mgogoro huu kuwaondoa CCM madarakani lakini Tanzania wao wanajadili ajenda za CCM aisee !!
Uwaondoe kwa NEC ipi? kule sheria zinafuatwa na kila mtu na kulindwa huku unaendeshwa kwa matakwa ya mtu mmoja
 
Ingekua Ulaya wapinzani wangetumia Mgogoro huu kuwaondoa CCM madarakani lakini Tanzania wao wanajadili ajenda za CCM aisee !!
Kwa wenzetu chansi kama hii ni lulu haswa ... maana hutokea mara chache
 
Mkuu Beatrice Kamugisha, hili la media ni kweli, Vyombo vya habari hatukutimiza wajibu wetu kutupatia Spika Bora.
Vibrant media ilipaswa kufanya analysis ya waliojitokeza ili kuonyeshea Spika Bora.
P

ED4EA354-D4B0-4437-9D1B-08F8A96EB527.jpeg
 
Mkuu Beatrice Kamugisha, hili la media ni kweli, Vyombo vya habari hatukutimiza wajibu wetu kutupatia Spika Bora.
Vibrant media ilipaswa kufanya analysis ya waliojitokeza ili kuonyeshea Spika Bora.
P
Comrade hivi unaposema vyombo vya habari hamkutimiza wajibu, ina maana hamkujua kuwa kuna wajibu au unataka kusema media editors woote nchini hamkujua kuna jambo hapo?.

Behind kama mimi najua hofu iliyopo nchini kuhusu kutoa habari zozote ngumu zinazoigusa serikali na mihimili yake although you know uliwahi kuwa mfano pale ulipoitwa kwenye kamati ya bunge is a part of hili la kuona habari na kuacha kuifuatilia.
 
Siku hizi vyeo wanagawiana tu wao kwa wao. Ukoo unamahela kibao, badala ya kujiingoza wafungue viwanda watanzania wapate ajira, wale wale ndio wanaomba kupewa uwaziri halafu bila Soni wanawaambia vijana wajiajiri. Ok. Vijana Ni wabunifu lkn hawana mitaji wameona waanze na umachinga then baadae watajiongeza wajenge viwanda. Hao hao wamachinga mmewafuata na masoko yao kwa bahati mbaya yanaungua.
Vijana Hawa watajiajiri vipi?
Hamna wasiwasi maana siku hizi hata hizo kura za wamachinga hamzihitaji maana si mtaiba kura.
 
Kusema anampinga ni ukosefu wa mtu aliyezoea kukubali tu bila kuuliza na kufanya utafiti.
Beatrice yuko sawa, hata Rais anakosea na tukiweka msoni yetu, yanamsaidia kuongoza vema.
Mama Samia si kama mwezetu yule aliyekiri hadarani kuwa hashauriki, na usipoteze muda wako kumpa maoni yako.
For once,Beatrice anampinga rais.
Beatrice unaandika manylleno ya kihuni. "Kuzingua"
M
 
Back
Top Bottom