Zamaradi acha makelele, hamuwezi ku-control kila kitu


mmmh hii ndo jf
 
Ni kiherehere huyu demu yaan kila kitu anajifanya anajua nikisikilizaga Leo tena ananichefuaga anatakaga aongee yy tu ndo anajua zaid na kutupia kiswangilish kwenye maongez yake!anapenda kudakia mambo Leo tena
 
Hata mtitu naye kashikilia hili bango. But this is a free market, sijui hawalioni hilo...

Watafute mfanyabiashara anayenunua kazi zao kwa bei kubwa labda hawajui maana ya soko huria
 
Watafute mfanyabiashara anayenunua kazi zao kwa bei kubwa labda hawajui maana ya soko huria

Hahahaaa.. Ukiwakosoa wanakuita mnafiki, mpinga harakati zao..huoni wanaita wakina JB wasaliti?
 

Kumbe hajamzui mtu kuuza mwenyewe hahahahah sion tatizo lake yeye anataka kupata faida. Mfano bakhresa akishusha bei ya unga mtalalamika? Kwan mwanzo sinema za kibongo zilikiwa zinauzwa shilling ngapi maana hata cjawah kununua. Kwa upande wa solution n kwamba wao waliojitoa kwa steps wajikite ktk kutengeneza movie zenye viwango na hata wauze 10000 kila moja na co kilalamika mfano kwa waliosafir safar za zenj wanaelewa bei ya boat za kilimanjaro n 23000 wakat wengine(ajar njenje) had 16000. Na watu bado wanagombea usafir wa kilimanjaro wa 23000. Steps hajawakataza kuama kwake, kuuza wenyewe, na hata kumgomea kumpekelea kazi zao. Waache uvivu wa kufikir
 

hii nondo nimeipenda
 

exactly haya.mambo yanahitaji shule mkuu .

.
 

salute mkuu@chige serikali inazuia over price siyo under price tena ya films mbona huku mitaani watu wanauza buku kitambo
 

Ni ngumu kidogo kujadili nawe hii issue, kwa sababu kinachojadiliwa hapa wewe hukijua kama ambavyo umeeleza kwenye red hapo. Nadhani ndio sababu umetoa mifano iliyo nje kabisa ya mada. Labda angalau ungesoma na kuelewa michango iliyopo hapa ukajua pa kuanzia ili twende sambamba.
Ila asante kwa kushiriki kwenye mada hii, kwani kwa ujumla wake inazungumzia ajira na maendeleo ya kiuchumi, kwani filamu zimerasimishwa kwa sasa na TRA wameshaanza kukusanya kodi kwenye filamu tangu mwanzoni mwa mwaka huu, nadhani mwezi June tutapata fursa ya kujua filamu zimechangia kiasi gani pato la Taifa.
Ova
 
Ukweli ulio wazi ni kwamba filamu za Kibongo ni dhaifu sana, na hatuwezi kukuza filamu za Kitanzania kwa kubeza tu udhaifu wake, bali kwa kukosoa mahali wanakokosea, na ni lazima tuziunge mkono kwani nazo sasa zinachangia pato la Taifa na kwa kiasi fulani zinatoa ajira binafsi kwa watu wenye viwango mbalimbali vya elimu.
Ieleweke kuwa, hakuna filamu iliyowahi kutengenezwa duniani bila kuwa na makosa (mchemko) yoyote, ila filamu yenye makosa machache ndio filamu bora, na yenye makosa mengi ndio filamu mbovu. Hivyo akina chige (Bongo Movies) waongeze ujuzi na bidii katika kupunguza makosa kwenye filamu zao ili ziwe bora.
Kwa utafiti wangu mdogo nimegundua kwamba tatizo kubwa la kwenye tasnia ya filamu ni kukosa utaalamu, kwa maana ya kutegemea kipaji pekee katika kazi zao. Pia, kutengeneza filamu kwa budget ndogo, ambayo haitoshi kuweza kuchukua kampuni zenye wataalamu wa kutengeneza filamu zao.
Bila shaka wengi wetu tumesikia gharama zinazotajwa na wanamuziki kwa kutengeneza video tu ya muziki zisizozidi dakika saba. Kwa maana hiyo filamu zetu zinahitaji uwekezaji wa uhakika sio mwekezaji asiyetaka kuwekeza kwa msanii, badala yake anafikiria kumkomoa msanii.
Kitu kibaya wanachofanya hawa wasanii wa Bongo Movies, ni kuamua kubaguana (au kufanywa wabaguane), kwa misingi ya umaarufu, kuwa na uwezo kifedha, kuwa chipukizi au kuwa na uwezo mdogo kifedha. Hii inawafanya washindwe kuwa na kauli ya kuwasaidia kwa umoja wao.
Nadhani miaka mitatu au minne iliyopita, script writers wa Hollywood waligoma kwa ajili ya kushinikiza kupanda kwa maslahi yao, na kweli shughuli ya utengenezaji wa filamu mpya zikazimama nadhani kwa muda wa mwezi mmoja hadi wakasikilizwa madai yao, kisha kazi kuendelea.
Sasa kwa mgogoro wao wa sasa alichofanya Steps ni kuwachukua wasanii wachache kisha kuwaahidi pepo ya dunia kwa makubaliano ya kumtetea, kwa kuwa wanaijua shida yao ni kuwa na pesa za kuwaonesha watu kuwa wanazo pesa nyingi na magari ya fahari. Wamemtii Steps na wamewageuka wenzao.
Wakati Kanumba akiwa hai alikuwa akiendesha Lexus nyeusi, lakini ilikuwa na mambo mengi nyuma ya pazia. Kwa gari lile alikuwa na deni la filamu nne kwa Steps, na bado gari lile alilipa nusu, hivyo bado alikuwa anadaiwa. Alifanikiwa kuacha filamu mbili ambazo zilitoka baada ya kifo chake, na akafa na deni la filamu mbili.
Nini kilichotokea baada ya kifo chake? Mwenye gari akadai sehemu iliyobaki ya pesa yake, ikabidi gari liuzwe kwa bei ya hasara, kisha likalipwa deni. Kwa bahati mbaya marehemu alikuwa na madeni mengine ya msingi, ikabidi mali zake nyingine ziuzwe ili kuyalipa, na baada ya miezi mitatu hakukuwa tena na mali inayoweza kuitwa ya Kanumba.
Na hilo ndilo lililofanya Mama Kanumba awalilie Steps angalau wampe sehemu ya mauzo ya filamu mbili alizoacha, lakini akaambiwa marehemu alishalipwa na bado anadaiwa. Ndipo aliposhauriwa acheze filamu ya maisha ya Kanumba, akacheza na haikufanya vizuri, akasogezwa mbali kabisa na sasa ameshasahaulika.
Tatizo la hawa wasanii wanapenda kujionesha kwamba wana uwezo mkubwa kipesa na wananufaika sana kwa mapato ya filamu zao, ndilo ambalo huwafanya wakose utetezi, lakini ukweli ni kwamba wana hali mbaya. Baada ya kifo cha Kanumba, JK ndipo alipopata fursa ya kuujua ukweli juu ya wasanii wa filamu, akasikitika sana na kuamua kufanya nao kikao binafsi, Ikulu.
Na alichosema JB kwenye hicho kikao, nadhani ndicho kilichofanya Rais aanze kuwa nao mbali mpaka hii leo. Nikipata muda baadaye nitaeleza kuhusu hicho kikao, kwani nilikuwepo kikaoni licha ya kwamba sio mmoja wa hao wasanii wa filamu, majukumu yangu ndio yalifanya niwe pale. Huwezi jua pengine nilikuwa muandaa juice ya wageni (hahahahahaaa).
Ova
 
Last edited by a moderator:
comment yako hapo juu inajitosheleza kabisa kufunguliwa uzi wa peke yake! tunasubiri yaliyojiri katika hicho kikao cha JK na akina JB hasa kuhusiana na hiyo kauli ya JB... Mdakuzi
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Mdakuzi,
Kwanza big up kwa kuuendeleza mnakasha huu. Mkuu dawa yenu, sina shaka kabisa kwa hivi sasa kwamba nawe ni mfuasi mkubwa sana wa haya mambo huku ukitamani kuona tasnia inasonga mbele! Tunahitaji mchango wako vile vile katika hili.

Back to the topic... hapa nianze na hilo la ubora wa filamu zetu! Hapa naungana mkono na Mdakuzi kwa 101% kwamba hakuna filamu duniani isiyo na mapungufu... HAKUNA! Tofauti pekee kati yetu na yao ni kwamba mapungufu yetu mengine yanatokana na stupid mistakes! Aidha niseme kwamba, mapungufu makuu ya filamu yapo ya aina mbili... mapungufu ya kiufundi/technical weaknesses na matatizo ya kisanaa/artistic weaknesses. Hapa ielekeweke kwamba, mapungufu ya kiufundi huwezi sana kuwalaumu watengenezaji wa filamu zetu kwani mengine yapo juu ya uwezo wao kv kukosa dhana bora za kutengenezea filamu!

Hata hivyo, bahati mzuri ni kwamba matatizo ya kiufundi yana nafasi ndogo sana ya kufanya filamu isivutie! Kwa sie tulio na umri wa kuanzia miaka 25 na kuendelea tumewahi kuangalia filamu kupitia VHS/kanda! Bado tunakumbuka jinsi VHS zilivyokuwa zinatoa low quality motion pictures huku zikinasa nasa kila wakati lakini bado uhondo wa filamu tuliendelea kuupata! Tuliendelea kuupata utamu wa filamu coz' filamu is all about mpangilio na msuko mzuri wa matukio! Mpangilio na msuko mzuri wa matukio hausababishwi na advanced equipment bali upangiliaji wa sanaa yenyewe... kuanzia kwenye script hadi directing! Hapa ni pale endapo scene inasema character anakimbia basi kweli aonekane anakimbia na kwanini anakimbia! Kama character anakimbia kutokana na hatari inayomkabili basi kweli aonekane anaikimbia hatari inayomkabili na kama ni ukimbiaji wa kutaka kuwahi aendako basi kweli i-reflect kwamba huyu character anakimbia kutokana na haraka aliyonayo! Hili halihitaji advanced equipment coz' hata kamera ya kwenye simu ina uwezo wa kumuonesha character anakimbia kutokana na hatar inayomkabili au anakimbia kwa ajili ya kuwahi aendako au anafanya mazuri... hapa kinachohitajika ni weledi tu wa Director wa kutengeneza uhalisia! Hili ndio moja ya matatizo ya msingi kabisa ya upungufu wa filamu zetu!!!

Tatizo lingine kubwa kabisa la filamu zetu ni stori/script! Hakuna kitu ambacho wasanii wetu hawakipi kipaumbele kama script wakati script ndio msingi wa filamu yenyewe! UKishakuwa na script mbovu, basi hata kama utakuwa na vifaa bora kuliko vyote duniani na waigizaji bora kuliko wote duniani bado filamu itakuwa mbovu tu! Kama nilivyosema hapo awali, filamu is all about mpangalio na msuko mzuri wa matukio linapokuja suala la artistic issues! Msuko wa matukio unatengenezwa kwenye script na sio kwenye kamera! Kwa bahati mbaya kabisa, wasanii wetu wanadhani kila mtu anaweza kuandika script! Ni rahisi sana kum-train mtu na akaigiza kwa kiwango cha juu kabisa tena ndani ya siku chache hata kama alikuwa hajawahi kuigiza kuliko kum-train mtu kuandika script! Script comes from inner feelings,so huwezi kuingia kwenye inner feelings za mtu! Hivyo basi, ikiwa huna ujuzi wa kuandika script bado utabaki kutokuwa na ujuzi unless upitie mafunzo maalumu ambayo hapa kwetu kwa bahati mbaya hakuna! Hata hivyo, wasanii wetu wengi wanaandika script huku karibu wote wakiwa hawana hata hiyo talent ya kuandika creative stories! Kuna siku niliwahi kumchoma mkuki wa moyo mdau mmoja baada ya kusema kwamba, ikiwa wewe umesoma darasa la kwanza hadi la saba, kisha form one hadi form four na hatimae kuanzia five hadi six na kote huko hukuwahi kuandika story basi hesabu kwamba wewe talent ya utunzi hauna! Kwavile hatuna shule maalumu basi talent ndiyo inayotakiwa kuchukua nafasi na more often than not, talent huanza kuonekana mapema kabisa lakini wengi wao wamejifunza kuandika ukubwani tena baada ya kuingia kwenye filamu! Katika mazingira kama haya usitarajie mtu kama huyo akatoa script yenye msuko mzuri wa matukio ambayo ndio msingi wenyewe wa filamu!!!

Suala la ushirikiano, kama ulivyosema nalo ni tatizo lingine! Umetoa mfano mzuri wa waandishi wa scriot wa Hollywood. Labda kwa kuweka kumbukumvu sawa, strike ile ilikuwa ni muda kidogo... kama sikosei ilianzia mwishoni mwa mwaka 2007 na kwisha mwanzoni mwa mwaka 2008. Ule mgogoro ulichukua takribani miezi minne na uliathiri hadi utolewaji wa TV Show maarufu ya 24 Season 7 coz' baada ya kuoneshwa Season 6, mgogoro ule ukasababisha Season 7 iwe delayed kwa mwaka mzima na katika kutowanyima watazamani uhondo, ndipo wakaingiza Season ambayo waliipa jina la Redemption... ile season inayomuonesha Jack Bauer yupo Afrika nchini Sangala!!!

Hili la Screenwriters wa Hollywood kugoma kupitia chama chao cha WGA(East & West) liliwezekana kwa sababu tu wana ushirikiano mkubwa; ushirikiano ambao huku kwetu haupo! Kutokana na kutokuwa na ushirikiano, ndio maana utakuta Shirikisho la Filamu (TAFF) linaburuzwa na Bongo Movie Club! Hawa TAFF wanaburuzwa kwavile bado ni dhaifu sana! Wasanii wengi wasio na majina wanailalamikia sana TAFF huku wakisahau kwamba udhaifu wa TAFF unatokana na udhaifu wa associations zinazounda TAFF... associations zinazotokana na wasanii wenyewe kv chama cha waandishi wa script, cinematographers, Chama cha Waongozaji wa filamu, chama cha waigizaji na kadhalika! Kwavile hivi vyama havina nguvu au ni sahihi kabisa tukiviita ni goi goi, ndio maana utakuta waliojipanga vizuri kama Bongo Movie (Club) ndio wanaonekana wana sauti hata mbele ya TAFF yenyewe ambayo nayo ni goi goi kutokana na wanachama wake nao kuwa goi goi!!

Pamoja na yote hayo, hapa tuweke jambo moja sawa... Bongo Movie (Club) hawapo kwa ajili ya maslahi ya wasanii wa tasnia ya filamu nchini bali wapo kwa ajili ya maslahi yao wenyewe (wana-Bongo Movie) ingawaje hata wao kwa wao bado kuna wanaojiita waanzilishi na wahamiaji! Hivyo basi, taasisi pekee ambayo ingeweza kupambana na Steps Entertainment kwa niaba ya wasanii wote ni TAFF na sio Bongo Movie! Kwa bahati mbaya kabisa, TAFF wenyewe ndio hao ambao tumeshayaeleza mapungufu yao!
 
Last edited by a moderator:
walivyokuwa wanauza elfu tano walikuwa wanatengeza parti tu kwa lazima, hii ya buku 1 ndio watatuuzia movie moja ina pati 7!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…