Tatizo tunapenda kupingana na ukweli! Kijana yeyote under 40 ambaye hajawahi kuoa wala kuwa na watoto kuoa mwanamke mwenye watoto 2 na baba wa hao watoto bado yupo around na anakuzidi kipato na bado anafanya kazi na mkeo, kutegemea furaha kwenye hiyo ndoa ni uzumbukuku! Zamaradi alitakiwa aolewe na mzee mwenye watoto kadhaa tena wengine wanalingana naye umri. Hata mimi angekua dada yangu ningemuozesha ila ningetaja mahari ndogo kwa sababu najua any day nitadaiwa. Nikuulize na wewe huyo dogo angekua kaka yako ungemshauri nini? Usijibu kinafiki
Mimi nitaangalia huyo dada anatabia ya aina gani maana wanawake huachwa kwa sababu tofauti....yaweza kuwa yeye anatabia mbaya na kashindikana ama ni mtu mzuri ila amekutana na mtu kilaza ndio maana ameamua kufanya yake.
Sasa katika hali ya kawaida, kama mwanamke yuko poa kitabia sioni shida akiolewa na ndugu yangu maana najua atakuwa na furaha.
Na kama wewe una hayo mawazo ya kwamba mwanamke ni kama gari kuwa unachagua used au mpya kabisa jua unakosea. Kama ukikutana na mwanamke anayejitambua na ni mstaarabu kitabia na kimwenendo, usije ukaona ni kosa kuwa naye hata kama ana watoto wawili.
Hauoi mwanamke sababu ya mashindano ya miss world mind you. Unaoa a life companion, unaoa rafiki, mtu atakaye kuwa na weww benet na kukupa msaada ya mawazo na kukupa ahuweni katika kipigo cha maisha unachopata daily.
Hizo itikadi za kuopoa mwanamke mwenye tako kubwa, bikira, sijui muonekano wa kimiss sijui mbwembwe gani waachie mabwana wadogo wanaopevuka maana by the way hayo ni matamanio ya kingono na kimwili ndio yanaendesha hisia zako.
Unaweza pata huyo bikira wako ila akaja kukupa stress humo ndani hadi ukashindwa kufurahia hayo mahusiano ila huyo mwenye watoto wa wawili akaitambua nafasi yake na akakupa mahaba na upendo ukasahau stress za dunia na ukaanza kunawiri na kupendeza sababu ya upendo unaopewa.....
So dont judge my brother.....let life be