Zambia wananchi wapanga foleni kununua unga. Inasikitisha sana

Zambia wananchi wapanga foleni kununua unga. Inasikitisha sana

MamaSamia2025

JF-Expert Member
Joined
Mar 29, 2012
Posts
14,588
Reaction score
32,361
Pichani ni wananchi kwenye miji mbalimbali nchini Zambia wakiwa kwenye foleni za kununua unga wa mahindi. Kwa sasa Zambia inakabiliana na uhaba mkubwa wa unga wa mahindi maarufu kwa jina la MEALIE MEAL.

Inadaiwa kuwa uhaba huo umetokana na Serikali kuruhusu uuzwaji holela nje ya nchi wa mahindi toka kwenye akiba ya taifa. Sababu nyingine imetokana na uhaba wa mahindi kwa nchi ya Tanzania kutokana na Tanzania & Zambia kuwa nchi mbili pekee kwa ukanda huu zinazolima mahindi halisi na sio GMO.

Kwa sasa taifa hilo limezuia uuzwaji wa mahindi au unga wa mahindi nje ya nchi hasa katika nchi ya DRC. Ikumbukwe DRC ni mnunuzi mkubwa wa miaka yote wa mahindi toka Zambia. Mpakani mwa DRC & Zambia katika mji wa Kasumbalesa kuna kamata kamata kubwa kwa malori yanayotaka kuvusha mahindi na unga kihuni kuelekea DRC. Pia watu binafsi wenye shehena za unga wamekuwa wakikamatwa na kupewa tuhuma za ulanguzi kitu ambacho kimepingwa na wengi na kuonekana ni uonevu.

Tanzania tunaishukuru Serikali ya Chama Cha Mapinduzi kwa uongozi imara na kuivusha nchi kwenye aibu ndogondogo kama hizi. Kwa sasa Zambia inaongozwa na HH wa chama cha UPND ambacho kinasifiwa sana na wapinzani wa CCM hapa nchini bila kujua wanachosifia.

FB_IMG_1681677781582.jpg
FB_IMG_1681677563583.jpg

 
Kama sio juzi ni juzi nyingine nimemsikia Waziri wa Kilimo na chakula wa Kenya akiwahakikishia Wakenya kwamba wameingia mkataba na Zambia kuwalimia mahindi na baada ya miezi minne bei ya unga itashuka maradufu Kenya maana watakuwa na uhakika wa chakula.
Afrika yangu.
 
aise!!
sio kosa la Rais Wala Serikali bali ni uhaba uliosababishwa na ukame kama ilivyo kwa jirani zetu wa Kenya.

Jambo la msingi kwa sisi watanzania ni kujifunza na kuchukua hatua madhubuti..

Wakulima tujitume kulima mazao ya vhakula.

Wizara ya kilimo ikae chonjo, ichukue tahadhari lkn pia iweke mikakati madhubuti
 
Africapitalism therefore means we cannot leave the business of development up to our governments, donor countries and philanthropic organizations alone.
The kind of challenges we face on the continent require not only vision but also patience and perseverance.
 
And also Africapitalism is the nexus between the ability of the private sector to create value and the government’s creation of a business friendly environment.
Companies that incorporate local value creation will be both more sustainable and more profitable in Africa in the long term.
 
Daah! Kwa hiyo hao walio kwenye foleni kubwa namna hiyo ni wale wanaonunua wakauzie wengine au ndio wale wa nusu kilo na kilo moja.
 
Daah! Kwa hiyo hao walio kwenye foleni kubwa namna hiyo ni wale wanaonunua wakauzie wengine au ndio wale wa nusu kilo na kilo moja.
Mkuu, you just look at this people's how they looks poor....🤔 this are the one of nusu kilo and kilo moja taking home for the kids..🤨
 
Hii inakuja hata hapa ,unless uwe si mtu anayefuatilia mambo , utashangaa siku moja unaamka hamna kitu kwenye masoko ndio akili zitawakaa vizuri ,
Sisi tuna BBT tutawalisha wao, muulize Bashe
 
Pichani ni wananchi kwenye miji mbalimbali nchini Zambia wakiwa kwenye foleni za kununua unga wa mahindi. Kwa sasa Zambia inakabiliana na uhaba mkubwa wa unga wa mahindi maarufu kwa jina la MEALIE MEAL.

Inadaiwa kuwa uhaba huo umetokana na Serikali kuruhusu uuzwaji holela nje ya nchi wa mahindi toka kwenye akiba ya taifa. Sababu nyingine imetokana na uhaba wa mahindi kwa nchi ya Tanzania kutokana na Tanzania & Zambia kuwa nchi mbili pekee kwa ukanda huu zinazolima mahindi halisi na sio GMO.

Kwa sasa taifa hilo limezuia uuzwaji wa mahindi au unga wa mahindi nje ya nchi hasa katika nchi ya DRC. Ikumbukwe DRC ni mnunuzi mkubwa wa miaka yote wa mahindi toka Zambia. Mpakani mwa DRC & Zambia katika mji wa Kasumbalesa kuna kamata kamata kubwa kwa malori yanayotaka kuvusha mahindi na unga kihuni kuelekea DRC. Pia watu binafsi wenye shehena za unga wamekuwa wakikamatwa na kupewa tuhuma za ulanguzi kitu ambacho kimepingwa na wengi na kuonekana ni uonevu.

Tanzania tunaishukuru Serikali ya Chama Cha Mapinduzi kwa uongozi imara na kuivusha nchi kwenye aibu ndogondogo kama hizi. Kwa sasa Zambia inaongozwa na HH wa chama cha UPND ambacho kinasifiwa sana na wapinzani wa CCM hapa nchini bila kujua wanachosifia.

Kwa hiyo ukosefu wa mahindi Zambia, ndio inahalalisha waTz kununua mahindi kwa 2000 kilo!? Au ndio inamaanisha ubora wa Samia( huyu wa kila mtu ale urefu wa kamba) juu ya Hichilema!? Sometimes mfiche upumbavu wenu Aisee. Mnajidhalilisha sana kama machoko.
 
Back
Top Bottom