Zanzibar: Askari wanne wa SMZ na maofisa 3 wa Idara ya Misitu mbaroni kwa mauaji ya Katibu wa ACT-Wazalendo tawi la Mwembemakumbu

Zanzibar: Askari wanne wa SMZ na maofisa 3 wa Idara ya Misitu mbaroni kwa mauaji ya Katibu wa ACT-Wazalendo tawi la Mwembemakumbu

Amebainisha kuwa askari hao walichukua mkokoteni huo kwa lengo la kuupeleka katika ofisi zao zilizopo Maruhubi lakini muda mfupi baadaye walivamiwa na kundi la vijana wakiwa na mapanga na silaha mbalimbali, akidai kuwa walitaka kuwazuia polisi na maofisa hao kutoondoka na gari walilokuwa wamepanda.

Kwa hii kauli tayari polisi washamaliza mchezo.
 
Kwa nini unataja nafasi yake ya kisiasa ktk taarifa ya maafa kama haya! Je, mauaji yake ni ya kisiasa? Kama ni ya kisiasa, maafisa misitu wanahusikaje? Kama siyo ya kisiasa, inatosha kuandika jina lake tu maana naamini alikuwa anayo kazi nyingine ya kuendesha maisha yake.
Waninga hawa, wanatafuta Kiki tu.
 
Habari njema,..

Vile vile wawajibishe na wale wotewalio uwa na kuwatesa raia wasiokuwa na hatia wakati wa Uchaguzi..

Nchi inaendeshwa na Sheria ndio inaoongoza Nchi
Ndio maana Sheria ukisema usiandamane, ukaenda, kinacho kupata ni halali yako
 
Kwa nini unataja nafasi yake ya kisiasa ktk taarifa ya maafa kama haya! Je, mauaji yake ni ya kisiasa? Kama ni ya kisiasa, maafisa misitu wanahusikaje? Kama siyo ya kisiasa, inatosha kuandika jina lake tu maana naamini alikuwa anayo kazi nyingine ya kuendesha maisha yake.
Imekuchoomaaa kama pasi eeeeh?? Meza tikiti maji basi...
 
ALAFU SIJUI KWA NINI ASKARI HASA POLISI HUWA HAWASTUKI ....YAANI KAZI YAO IKISHAKUWA IMEISHA WANAWATOA KAFARA KAMA USHAHIDI .....KAMA YULE POLISI ALIYEMUUWA MWANDISHI WA HABARI IRINGA.....KAMA KWELI WAKO SERIOUS WAKAMATE MAZOMBI WOTE ....
 
Maelezo dhaifu sana, hivi kweli vijana wenye mapanga na marungu wanaweza kujitokeza hivyo kwa suala la mkokoteni wenye mchanga!
 
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja linawashikilia askari wanne wa vikosi vya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) na maofisa watatu wa Idara ya misitu kwa tuhuma za mauaji ya Katibu wa ACT Wazalendo tawi la Mwembemakumbu, Said Salum Suleiman.


Video hii inamuonyesh SAID MMANGA SULEIMAN, Mwenyekiti wa ACT Wazalendo, tawi la Mwembe Makumbi, aliyepigwa risasi na polisi na kufariki baada ya muda, kwa kosa lakukamatwa na mchanga katika maeneo ya Muembe Makumbi Mkoa wa Mjini Magharib

----
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja linawashikilia watu saba kwa tuhuma za mauaji ya Said Salum Suleiman (32) mkazi wa Mwembemakumbi mjini Unguja.

Wanaoshikiliwa kwa tuhuma za mauaji ya Suleiman ambaye alikuwa katibu wa ACT-Wazalendo tawi la Mwembemakumbu ni askari wanne wa vikosi vya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) na maofisa watatu wa idara ya misitu.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Alhamisi Novemba 12, 2020 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi, Awadh Juma Haji amesema tukio hilo limetokea jana saa 8 mchana ikidaiwa kuwa alipigwa risasi na maofisa hao eneo la Mwembemakumbi.

Amesema askari hao wakiwa wameambatana na maofisa wa idara ya misitu walikuwa katika doria maalumu kuwabaini wanaojihusisha na uhalifu wa mazao ya misitu na uharibifu wa mazingira.

Amesema wakiwa wanatokea katikati ya mji wakiwa na gari lenye namba za usajili SMZ 451B aina ya Mitsubishi walimkuta Suleiman akiwa na mkokoteni uliopakiwa mchanga.

Amesema mkokoteni huo ulikuwa ukivutwa na punda na alikuwa akitokea eneo la bondeni kuingia barabarani lakini alipowaona alikimbia na kuacha mkokoteni huo.

Amebainisha kuwa askari hao walichukua mkokoteni huo kwa lengo la kuupeleka katika ofisi zao zilizopo Maruhubi lakini muda mfupi baadaye walivamiwa na kundi la vijana wakiwa na mapanga na silaha mbalimbali, akidai kuwa walitaka kuwazuia polisi na maofisa hao kutoondoka na gari walilokuwa wamepanda.

Amesema katika kile alichokiita mapambano watu hao walivunja kioo cha nyuma cha gari na kusababisha askari kufyatua risasi iliyompata Suleiman.

“Baada ya kutokea kwa tukio hilo maofisa hao waliondoka mara moja katika eneo hilo na kuwaachia wananchi wakitoa msaada kwa Suleiman ikiwa ni pamoja na kumpakia kwenye gari kwa lengo la kumpeleka hospitali,” amesema.

Chanzo: Mwananchi
Tayari hapo Polisi wamekwishadai eti wao ndo walishambuliwa
 
Picha za watuhumiwa ziko wapi?
Nimemkumbuka Kamanda Muroto
 
Walimjua Ni act WAZALENDO ndo maana wakampiga risasi
Kwa nini unataja nafasi yake ya kisiasa ktk taarifa ya maafa kama haya! Je, mauaji yake ni ya kisiasa? Kama ni ya kisiasa, maafisa misitu wanahusikaje? Kama siyo ya kisiasa, inatosha kuandika jina lake tu maana naamini alikuwa anayo kazi nyingine ya kuendesha maisha yake.
 
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja linawashikilia askari wanne wa vikosi vya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) na maofisa watatu wa Idara ya misitu kwa tuhuma za mauaji ya Katibu wa ACT Wazalendo tawi la Mwembemakumbu, Said Salum Suleiman.


Video hii inamuonyesh SAID MMANGA SULEIMAN, Mwenyekiti wa ACT Wazalendo, tawi la Mwembe Makumbi, aliyepigwa risasi na polisi na kufariki baada ya muda, kwa kosa lakukamatwa na mchanga katika maeneo ya Muembe Makumbi Mkoa wa Mjini Magharib

----
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja linawashikilia watu saba kwa tuhuma za mauaji ya Said Salum Suleiman (32) mkazi wa Mwembemakumbi mjini Unguja.

Wanaoshikiliwa kwa tuhuma za mauaji ya Suleiman ambaye alikuwa katibu wa ACT-Wazalendo tawi la Mwembemakumbu ni askari wanne wa vikosi vya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) na maofisa watatu wa idara ya misitu.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Alhamisi Novemba 12, 2020 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi, Awadh Juma Haji amesema tukio hilo limetokea jana saa 8 mchana ikidaiwa kuwa alipigwa risasi na maofisa hao eneo la Mwembemakumbi.

Amesema askari hao wakiwa wameambatana na maofisa wa idara ya misitu walikuwa katika doria maalumu kuwabaini wanaojihusisha na uhalifu wa mazao ya misitu na uharibifu wa mazingira.

Amesema wakiwa wanatokea katikati ya mji wakiwa na gari lenye namba za usajili SMZ 451B aina ya Mitsubishi walimkuta Suleiman akiwa na mkokoteni uliopakiwa mchanga.

Amesema mkokoteni huo ulikuwa ukivutwa na punda na alikuwa akitokea eneo la bondeni kuingia barabarani lakini alipowaona alikimbia na kuacha mkokoteni huo.

Amebainisha kuwa askari hao walichukua mkokoteni huo kwa lengo la kuupeleka katika ofisi zao zilizopo Maruhubi lakini muda mfupi baadaye walivamiwa na kundi la vijana wakiwa na mapanga na silaha mbalimbali, akidai kuwa walitaka kuwazuia polisi na maofisa hao kutoondoka na gari walilokuwa wamepanda.

Amesema katika kile alichokiita mapambano watu hao walivunja kioo cha nyuma cha gari na kusababisha askari kufyatua risasi iliyompata Suleiman.

“Baada ya kutokea kwa tukio hilo maofisa hao waliondoka mara moja katika eneo hilo na kuwaachia wananchi wakitoa msaada kwa Suleiman ikiwa ni pamoja na kumpakia kwenye gari kwa lengo la kumpeleka hospitali,” amesema.

Chanzo: Mwananchi
Maelezo yanasema alikimbia.....
Sasa tunaona tena kapigwa risasi!
 
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja linawashikilia askari wanne wa vikosi vya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) na maofisa watatu wa Idara ya misitu kwa tuhuma za mauaji ya Katibu wa ACT Wazalendo tawi la Mwembemakumbu, Said Salum Suleiman.


Video hii inamuonyesh SAID MMANGA SULEIMAN, Mwenyekiti wa ACT Wazalendo, tawi la Mwembe Makumbi, aliyepigwa risasi na polisi na kufariki baada ya muda, kwa kosa lakukamatwa na mchanga katika maeneo ya Muembe Makumbi Mkoa wa Mjini Magharib

----
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja linawashikilia watu saba kwa tuhuma za mauaji ya Said Salum Suleiman (32) mkazi wa Mwembemakumbi mjini Unguja.

Wanaoshikiliwa kwa tuhuma za mauaji ya Suleiman ambaye alikuwa katibu wa ACT-Wazalendo tawi la Mwembemakumbu ni askari wanne wa vikosi vya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) na maofisa watatu wa idara ya misitu.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Alhamisi Novemba 12, 2020 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi, Awadh Juma Haji amesema tukio hilo limetokea jana saa 8 mchana ikidaiwa kuwa alipigwa risasi na maofisa hao eneo la Mwembemakumbi.

Amesema askari hao wakiwa wameambatana na maofisa wa idara ya misitu walikuwa katika doria maalumu kuwabaini wanaojihusisha na uhalifu wa mazao ya misitu na uharibifu wa mazingira.

Amesema wakiwa wanatokea katikati ya mji wakiwa na gari lenye namba za usajili SMZ 451B aina ya Mitsubishi walimkuta Suleiman akiwa na mkokoteni uliopakiwa mchanga.

Amesema mkokoteni huo ulikuwa ukivutwa na punda na alikuwa akitokea eneo la bondeni kuingia barabarani lakini alipowaona alikimbia na kuacha mkokoteni huo.

Amebainisha kuwa askari hao walichukua mkokoteni huo kwa lengo la kuupeleka katika ofisi zao zilizopo Maruhubi lakini muda mfupi baadaye walivamiwa na kundi la vijana wakiwa na mapanga na silaha mbalimbali, akidai kuwa walitaka kuwazuia polisi na maofisa hao kutoondoka na gari walilokuwa wamepanda.

Amesema katika kile alichokiita mapambano watu hao walivunja kioo cha nyuma cha gari na kusababisha askari kufyatua risasi iliyompata Suleiman.

“Baada ya kutokea kwa tukio hilo maofisa hao waliondoka mara moja katika eneo hilo na kuwaachia wananchi wakitoa msaada kwa Suleiman ikiwa ni pamoja na kumpakia kwenye gari kwa lengo la kumpeleka hospitali,” amesema.

Chanzo: Mwananchi

Jamani hivi ni hadi lini hawa jamaa wanapotowa taarifa zao za uongo wanafikiri kuwa sisi wananchi hatuna uwezo wa kujua kama wasemacho ni uongo?

1. Tunaambiwa kuwa wananchi walijitokeza na mapanga na silaha mbali mbali. Suali video hio hapo mbona hakuna hata mmoja mwenye silaha yeyote hata fimbo?

2. Tunaambiwa kuwa askari hao walichukua mkomkoteni kwa lengo la kuupeleka kituoni kwao. Suali hivi walikuwa wanataka kumpakia punda na mkomkoteni wake katika gari yao?

3. Tunaambiwa kuwa Slemani alikimbia alipowaona askari na aliwacha mkokoteni na punda wake, sasa ajabu ni kuwa tunazidi kuambiwa kuwa baada ya wananchi kuwavamia askari hao walifyatua risasi amabyo ilimpiga Slemani. Suali Hivi askari hawa wana shabaha ya aina gani kiasi cha kuweza kufyatua risasi na ikawakosa wale wote waliowavamia na kumpata Slemani ambae alikwisha kimbia katika eneo hilo?

4. Kama walivyatua risasi baada ya kuvamiwa na wananchi ni kwa nini hivi sasa wako mahabusu? Kwa nini hawakusimamishwa kazi tu wakati uchunguzi unaendelea?

Msitufanye sie watoto wadogo jamani!!!!!

Kwa taarifa tunazozipokea ni kuwa Slemani hata hakupigwa risasi hapo alipokutwa, ila askari walimtupa hapo baada ya kumpiga risasi sehemu nyengine kabisa.
 
Japo taarifa inajikanganya sana kwenye majina na tittle ya muhusika ila kitendo cha kumuuwa binaadam yeyote ni ukosefu wa utu. Nimejaribu kutazama hapo kwa hao watu sijaona hata mmoja mwenye jiwe sembuse mapanga yaliyotajwa. Pia inaonesha aliyeuawa sio aliyekimbia na kama ni aliyekimbia kwa kukutwa na mkokoteni wa mchanga ni wazi aliuwa mapema kabla ya wananchi kuwazingira hao askari.

Kama nchi tumefikia hatua mbaya sana ambayo wenye mamlaka ya kutulinda wanaona rahisi sana kutuuwa. Inaumiza sana.... Poleni sana wafiwa.
 
Nami nasema hapana! Tumeifanya nafasi ya kisiasa kuwa jambo muhimu sana ktk nchi kiasi kwamba, sasa kila mpuuzi anataka kuwa mwanasiasa. Hata diwani akifumaniwa tunaona ni sahihi sana kumzomea kwa kutumia nafasi yake ya kisiasa. Tunakoelekea ni kama sasa maisha ni siasa tu!

Kila siku watu wanauwa wake zao lakini hatusikii wakitaja kazi zao za maisha, badala yake akiwa nafasi ya kisiasa ndo inatajwa. Huu ni udhaifu tunaoulea kwa lengo la kuamini chama cha siasa ndo kila kitu.
Hivi wewe ulisoma hiki ulichokiandika hapa kabla ya kubonyeza "post reply"
 
Back
Top Bottom