Zanzibar kuendelea kunufaika na karafuu ya Morogoro, wakatazwa isiuzwe kwa ushindani, Waziri wa Kilimo, viwanda SMZ yuko Morogoro leo

Zanzibar kuendelea kunufaika na karafuu ya Morogoro, wakatazwa isiuzwe kwa ushindani, Waziri wa Kilimo, viwanda SMZ yuko Morogoro leo

Kashfa ya Karafuu inanukia.

Mkuu hebu tuwekee nyama zaidi na facts za kuthibitisha tuweze kuongeza agenda za kuikataa CCM
Subiri Leo utaona Ziara ya huyo Waziri wa Kilimo, Viwanda na Biashara wa Zanzibar.
 
Karafuu ya Morogoro usiifananishe na karafuu ya Pemba. Its about quality.
Kuna nchi nyingi zinazalisha karafuu duniani, lakini Zanzibar ni number one by quality.
Sasa kama ni namba one wanang'ang'ania ya Morogoro kwa lipi?
 
Karafuu ya Morogoro usiifananishe na karafuu ya Pemba. Its about quality.
Kuna nchi nyingi zinazalisha karafuu duniani, lakini Zanzibar ni number one by quality.

Hiyo quality inatokana na nini na umeipima vipi?
 
Nina shamba hapo Morogoro la Karafuu. Mwaka wa jana walikuja wa indonesia (Barozi wa Indonesia Tanzania), kuingia mkataba Kijiji cha Konde Matombo Morogoro, Mkataba uliingiwa mbele ya Mkurugenzi wa Halimashauri Rehema Bwasi, Mkuu wa Wilaya(Albert Msando) na Wanasheria wa Ubarozi na Halimashauri. Wa indonesia hao pia wamewekeza Zanzibar kwahiyo wamekuja na Wazanzibar wengi. Mkataba unataja ujenzi wa kiwanda cha majani ya Karafuu kuzalisha mafuta, na Ununuzi wa Karafuu yenyewe. Utekelezaji wa mradi hauweleweki mpaka sasa. Kuna benki ilikuja kutoka Mikopo, pia nayo ikaingia mkataba na wanakijiji ikawaadaa ikaondoka. Naona hata waziri wa Zanzibar anaenda nae atawapiga kiswahili pia ataondoka. Morogoro Milima ya Uluguru (Matombo) kwa sasa wanaongoza kulima mazao ya viungo (Karafuu) kwa Tanzania, na miaka 3 ijayo itatoa karafuu mara 4 ya Zanzibar, lakini Serikali imewaacha wakulima, ambao kwa nguvu zao na kujitafuta wamebuni Njia za kulima zao hilo bila msaada wa serikali wala ushauri wao. Wanaofaidika na karafuu ya Morogoro ni Kenya, ambao utumia madalali wa kitanzania kukodisha Miti kabla haijazaa na kuwanyonya wakulima huku Serikali ikiangalia. Karafuu hiyo uenda Kenya sababu madalali wameshika soko. Nini cha kufanya. i. Kuanzisha chama cha ushirika ambacho wakulima watauza, watapata mikopo, na watapata ushauri wa kilimo, Mkurugenzi na Mkuu wa Wilaya walisema wataanzisha mbele ya mkutano wa wananchi lakini hakuna kilichoanzishwa yalikuwa maneno. ii. Wananchi wanajitaidi kulima lakini moundombinu ni duni, Barabara ya Matombo - Konde KM 4 ni mbovu na Injinia wa Halimashauri aliwaambia wananchi kwamba ataijenga lakini hakuna kinachoendelea. iii. Umeme umevutwa kijijini na transfoma zimefungwa 2 lakini huu ni mwaka wa 3 haujawashwa kwahiyo wananchi wamechoka. iv. Wananchi wameongopewa sana na wanasiasa kwa namna nyingine wamechoka. Kijiji kimoja kinatoa tani 300 za karafuu, kg 1 inauzwa 14,000/. hadi elf 22,000/. Lakini kijiji barabara mbovu, zahanati hakuna, shule msingi mbovu, sekondari hakuna na Umeme hakuna. Serikali vikumbukeni vijiji watu wanapambana lakini msaada hakuna. Vijiji vinavyolima Karafuu Milima ya Uluguru ni Konde, Lubwe, Tegetero, Kinore, Sanzani, Kitungwa, Lugogo, Kibwege, na vinginevyo.
Tatizo lenu mnaitegemea serikali kwa kila kitu! Hata chama cha ushirika mnataka serikali iwaanzishie. Katika dunia ya leo ya mtandao, tafuteni soko wenyewe. Jipangeni ili mjijengee barabara maana itawafaa sana.

Amandla...
 
Juhudi za Mkoa wa Morogoro kuwakwamua wakulima wa karafuu kupata mnunuzi mwenye bei nzuri zimegonga mwamba baada ya kulazimishwa kuwa lazima karafuu inayozalishwa Morogoro basi iuzwe kwa SMZ ili wao wauze nje kwa bei kubwa zaidi.

kwa wasiojua, Morogoro vijijini wanazalisha karafuu nyingi kuliko Zanzibar yote. Uongozi wa Morogoro kwa muda mrefu umekuwa ukipambana ili ipate wanunuzi watakaoshindana badala ya kuendelea kulanguliwa na SMZ na wao kupata bei kubwa katika soko la dunia.

siku ya leo Waziri wa Viwanda, Kilimo na Biashara wa Zanzibar anafanya ziara huko Morogoro vijijini wanakolima karafuu. Awali walilazimisha Uongozi wa Mkoa wa Morogoro uingie nao mkataba wa kuwa hakuna mtu mwingine kununua karafuu ya Morogoro isipokuwa wao SMZ.

Ikumbukwe karafuu ni zao ghali sana duniani. bei yake kimataifa ni kubwa sana. Siku zote SMZ ilikuwa inajificha chini ya mawakala kuinunua lakini sasa wamekuja wenyewe.

sasa huu Muungano ni kama hauna maana kama utakuwa unanufaisha kasehemu kadogo huku majority wakiumia. haya maagizo kutoka juu yanatuumiza watanganyika. walianza kukopa pesa nyingi kupeleka kwao, wamekuja kubinafsisha bandari zetu zote, wakasema wana ardhi yao Bagamoyo huku watu wa bara hawaruhusiwi kumiliki ardhi kule, sasa leo wamekuja kwenye karafuu Morogoro.
Wacha uwongo.mjinga mmoja wewe! Karafu ya morogoro inauzwa Kenya. Na chengine naona unazubgumzia vitu huvijui. Taasisi inayoshubulikia karafuu ni ZSTC ambayo.ikonchini ya wizara ya biashara ya znz na siyo.kilimo.
Rudi tena kajipange ulete uchongani mwengine.
 
Tatizo lenu mnaitegemea serikali kwa kila kitu! Hata chama cha ushirika mnataka serikali iwaanzishie. Katika dunia ya leo ya mtandao, tafuteni soko wenyewe. Jipangeni ili mjijengee barabara maana itawafaa sana.

Amandla...
Wewe unaonekana unajua sana. Hiyo barabara ya Km 4 wamejenga wao wenyewe, mazingira ni ya Milima kwahiyo unaitaji maboresho ya kiufundi. Karafuu na Vannila sio mahindi unauza kwa kila mtu, either iende Kenya, Mauritius, Indonesia,China, India, France au Holland nchi zinazodili na Spice Foodstaff, na dawa za meno. Ili usafirishe karafuu au Vannila lazima u- meet international standard katika kuzikausha na perking. Lazima uwe na mnyololo wa kuchuma - kuchambua - kukausha - kuifadhi - Kusafirisha - Soko la Wakati.Ukikosea hapo kwenye mnyololo Zinakua uchafu Sokoni. Ndio maana Zanzibar serikali inasimamia kila kitu, maana mkulima hawezi. Ushirika wananchi wameshajisajiri kazi ni kwa viongozi kutimiza walichohaidi.
 
kwa wasiojua, Morogoro vijijini wanazalisha karafuu nyingi kuliko Zanzibar yote. Uongozi wa Morogoro kwa muda mrefu umekuwa ukipambana ili ipate wanunuzi watakaoshindana badala ya kuendelea kulanguliwa na SMZ na wao kupata bei kubwa katika soko la dunia.
lete data zinazoonyesha Morogoro inazalisha karafuu nyingi kuliko Zanzibar
 
Wewe unaonekana unajua sana. Hiyo barabara ya Km 4 wamejenga wao wenyewe, mazingira ni ya Milima kwahiyo unaitaji maboresho ya kiufundi. Karafuu na Vannila sio mahindi unauza kwa kila mtu, either iende Kenya, Mauritius, Indonesia,China, India, France au Holland nchi zinazodili na Spice Foodstaff, na dawa za meno. Ili usafirishe karafuu au Vannila lazima u- meet international standard katika kuzikausha na perking. Lazima uwe na mnyololo wa kuchuma - kuchambua - kukausha - kuifadhi - Kusafirisha - Soko la Wakati.Ukikosea hapo kwenye mnyololo Zinakua uchafu Sokoni. Ndio maana Zanzibar serikali inasimamia kila kitu, maana mkulima hawezi. Ushirika wananchi wameshajisajiri kazi ni kwa viongozi kutimiza walichohaidi.
Mkuu hongera sana nmekuelewa vzr ila kwa utandawazi huu mmekwama hata nyie wenyewe kujikusanya na kuweka miundombinu Rafiki kama sehemu Safi za kuchambulia na kadhalika adi kuisubiri serikali ambayo ipo bize kuuza bandari
 
Mkuu umemwaga madini muhimu, natamani kuingia kwenye hiki kilimo naomba nije pm kwa maongezi zaidi.
Aliyosema ni kweli kabisa, nimeenda chama cha ushirika wa kilimo cha mazao ya viungo kinole, aiseee kule pana kila kitu, hali ya hewa nzuri mvua na manyunyu muda wote, wanalima viungo vyote
 
Wacha uwongo.mjinga mmoja wewe! Karafu ya morogoro inauzwa Kenya. Na chengine naona unazubgumzia vitu huvijui. Taasisi inayoshubulikia karafuu ni ZSTC ambayo.ikonchini ya wizara ya biashara ya znz na siyo.kilimo.
Rudi tena kajipange ulete uchongani mwengine.
Wewe ni Waziri au mchepuko wa Waziri?
 
Wewe unaonekana unajua sana. Hiyo barabara ya Km 4 wamejenga wao wenyewe, mazingira ni ya Milima kwahiyo unaitaji maboresho ya kiufundi. Karafuu na Vannila sio mahindi unauza kwa kila mtu, either iende Kenya, Mauritius, Indonesia,China, India, France au Holland nchi zinazodili na Spice Foodstaff, na dawa za meno. Ili usafirishe karafuu au Vannila lazima u- meet international standard katika kuzikausha na perking. Lazima uwe na mnyololo wa kuchuma - kuchambua - kukausha - kuifadhi - Kusafirisha - Soko la Wakati.Ukikosea hapo kwenye mnyololo Zinakua uchafu Sokoni. Ndio maana Zanzibar serikali inasimamia kila kitu, maana mkulima hawezi. Ushirika wananchi wameshajisajiri kazi ni kwa viongozi kutimiza walichohaidi.
Brother unaelewa unachofanya sababu wewe ni mkulima. Hawa wadangaji wasiojua kuhusu Kilimo waache waendelee kuhangaika na kutoelewa kwao.
 
Mkuu hongera sana nmekuelewa vzr ila kwa utandawazi huu mmekwama hata nyie wenyewe kujikusanya na kuweka miundombinu Rafiki kama sehemu Safi za kuchambulia na kadhalika adi kuisubiri serikali ambayo ipo bize kuuza bandari
Morogoro ina vitu vizuri lakini kitu kinaitwa Economic lobbying hakuna. Ushawishi uku upo kwa wanasiasa tu, ila wananchi wenyewe hatuwezi. Mwanasiasa akisikia una kikundi chenye nguvu ya kwa ajiri ya Maendeleo na yeye mwanasiasa hana nafasi katika iko kikundi basi atapambana akiue, au umuingize ili apige siasa, na mchelewe chelewe. Ila tutafika tu.
 
Wewe uliyofika ndio unakuwa shuhuda mzuri.

Hongera sana
Aliyosema ni kweli kabisa, nimeenda chama cha ushirika wa kilimo cha mazao ya viungo kinole, aiseee kule pana kila kitu, hali ya hewa nzuri mvua na manyunyu muda wote, wanalima viungo vyote
U
 
Back
Top Bottom