Zanzibar na ndizi za mjane!

Zanzibar na ndizi za mjane!

Zanzibar ni kanchi kabaguzi kanakopenda kubebwa na Bara. Kuna walakini mkubwa katika huu muungano wetu. Lazima serikali ya Muungano (kama ndiyo ya Tangangika) iamke na kutetea raia wake wanaonyanyaswa na Wazanzibar.
 
Kama kuna habari inakera, kufedhesha na kutia hasira wiki hii ni jinsi serikali ya Zanzibar ilivyoshughulikia suala la ndizi za mjane aitwaye Veronica Mwanjala.

Kosa la Veronica ni kupeleka ndizi Zanzibar ili ajikimu kimaisha yeye na watoto wake. Kilichotokea pale bandarini ni maelezo yanayo ashiria hisia za kibaguzi dhidi ya watu wa Bara.

Tunaambiwa eti Veronica ndizi zake hazihitajiki soko la Zanzibar, mara zina vidudu, mara hazina vibali, na faini ya elf 50 juu!

Suala hili ni dogo lakini limeleta hisia za kibaguzi kutoka kwa wazanzibari, tena serikali, dhidi ya Watanzania bara.

Wote tunaelewa jinsi wazanzibari na wapemba wanavyovumiliwa kwa mengi hapa Bara na hawachukuliwi kama raia wa nje kama ipasavyo.

Mnaya zaidi serikali ya Zanziba na waziri wake wamemfanyia uharamia mama mjane!

Hili halikubaliki!

Mwenye namba ya Veronica Mwanjala atupatie ili JF tuanze mchango wa kurejesha mtaji wa huyu mama aliyedhulumiwa.
Wewe unaliita hili jambo "swala dogo."

Mimi silioni kuwa swala dogo hata kidogo, ni swala kubwa sana katika uhai wa nchi yetu ya Muungano.

Kiufupi ni kwamba matendo haya yanayofanywa huko Zanzibar, ni mkakati maalum wa kuchochea hisia toka Tanganyika, ili wenye lengo lao la kuuvunja Muungano lifanikiwe.

Huu ni mkakati maalum kwa wenye lengo lao.

Naunga mkono uhitaji wa Simu ya huyo mama, achangiwe.
 
KIJESHI IDARA ZOTE ZNZ SIO NCHI.
ubaguzi huu ulitakiwa kutolewa pande mbili bara na visiwani,kiufupi hakuna cha raisi huko wala TRA YA KWAO
 
Huu Muungano sisi ndio tumeshika mkono, wenzetu hawana time kabisa na sisi.
 
Pamoja na kumsapoti mama Samia, masuala haya ya unafiki wa wazi yaakera sana.
Inabidi huyo mama wamrudishie mtaji wake.
Hapa huwa ninashindwa kabisa kukuelewa wewe ni binaadam wa namna gani. Unayo 'conflict' kubwa sana ndani yako.

Niliwahi kuzozana nawe juu ya Magufuli enzi zile, humu humu JF..., leo ninakuona ukimshangilia huyu mrithi anayefanya makosa makubwa ya kuugawa Muungano huu, na bado unatoa visababu!

Ninashindwa kabisa kukuelewa.
 
Hebu ngoja.

Hivi huyo mama, Veronica hawezi kwenda mahakamani kudai afidiwe?

Hakuna wanasheria wanaoweza kumwongoza huyu mjane atafute haki yake?
 
Hapa jino kwa jino tu.
Kama wamefikia kutunyanyapaa kwa wazi wazi na sisi tulianzishe mbona tunaishi nao huku uraiani?! Tuone upande upi utaumia zaidi.
 
Kama kuna habari inakera, kufedhesha na kutia hasira wiki hii ni jinsi serikali ya Zanzibar ilivyoshughulikia suala la ndizi za mjane aitwaye Veronica Mwanjala.

Kosa la Veronica ni kupeleka ndizi Zanzibar ili ajikimu kimaisha yeye na watoto wake. Kilichotokea pale bandarini ni maelezo yanayo ashiria hisia za kibaguzi dhidi ya watu wa Bara.

Tunaambiwa eti Veronica ndizi zake hazihitajiki soko la Zanzibar, mara zina vidudu, mara hazina vibali, na faini ya elf 50 juu!

Suala hili ni dogo lakini limeleta hisia za kibaguzi kutoka kwa wazanzibari, tena serikali, dhidi ya Watanzania bara.

Wote tunaelewa jinsi wazanzibari na wapemba wanavyovumiliwa kwa mengi hapa Bara na hawachukuliwi kama raia wa nje kama ipasavyo.

Mnaya zaidi serikali ya Zanziba na waziri wake wamemfanyia uharamia mama mjane!

Hili halikubaliki!

Mwenye namba ya Veronica Mwanjala atupatie ili JF tuanze mchango wa kurejesha mtaji wa huyu mama aliyedhulumiwa.
Kweli kabisa !!
 
Back
Top Bottom