Zanzibar: Wadaiwa kuitwa Mgogoni kwa Rais Samia na kupewa msaada wa Tsh. 5,000

Zanzibar: Wadaiwa kuitwa Mgogoni kwa Rais Samia na kupewa msaada wa Tsh. 5,000

Abraham Lincolnn

JF-Expert Member
Joined
Apr 12, 2018
Posts
2,754
Reaction score
4,975
Nimeshangaa sana kiongozi mkubwa kutumia fedha kufanya ushawishi na kampeni wakati huo huo ulikuwa na nafasi ya kubadilisha maisha ya hao wanaopokea fedha hiyo kwa kuandaa mazingira rafiki ili uchumi wao uweze kukua! Fedha hiyo ingetumika kujenga masoko mazuri na miundombinu bora ili kina mama wauze samaki zao bila shida yoyote ingekuwa na manufaa zaidi kuliko kutumia fedha hiyo kufanya "Cheap Politics".


"Nipo Mgogoni, kwa Mama Samia Suluhu Hassan, nimekuja kuchukua msaada, lakini nimefungua bahasha nimekuta shilingi 5,000, hata haijafikia nauli niliyotumia kufika hapa. Kweli sijaitwa lakini nilipata taarifa kutoka kwa waliombiwa pelekeni ujumbe kwa wenzenu waje kupata msaada. Bora wangetuacha majumbani kwetu wasingeleta hata hiyo taarifa! Elfu tano mama Samia Suluhu Hassan, kweli ungewapa wafanyakazi wako?" Amesikika mama huyo kwenye video.

Pia soma: Aliyerekodi video akieleza amepewa bahasha yenye Tsh. 5,000 huko Kizimkazi asibughuziwe, kama mamlaka zina ushahidi kadanganya waseme

RC Amour: Rais Samia hahusiki na sadaka ya Tsh. 5000 Pemba, ni upotoshaji
 
Dola inatukosea Sana watz!!MTU kama kashindwa SI mwambieni.akae pembeni TU kistaarabu!!?

Ujinga huu,jamhuri inaaibika kabisa kama hiki ndicho kilichotokea maana yake vetting ilifeli,ujasusi was kiuongozi umefeli Sasa nyie kama Dola mmefaulu nini kumpa huyu anaefanya haya!!?

So sad!
 
Tumepiga hatua kubwa sana kiuchumi.
Kwanza ilikuwa ni CHUMVI,MCHE WA SABUNI.
Kila nikipita barabarani kila baada ya magari manne linalofuata ni NUMBER E,hivyo anayedai kuwa sisi ni masikini huyo ana lake jambo labda AHAMIE BURUNDI.

Sasa kutoka kwenye kupewa CHUMVI,MCHE WA SABUNI sasa hivi ni 5K!
MAKOFI TAFADHARI!!!!👏👏👏👏👏👏👏
 
Atukuzwe Mama Samia Suluhu Hassan...soon ataitwa Mtukufu kama alivyoitwa Daniel Arap Moi

Nani kama yeye?

Hakika mama anaupiga mwingi
 
Tuko mfungoni lkn tunashuhudia maajabu na ulaghai sasa mfungo ukiisha sijui itakuwaje!!
Teuzi za kulazimisha ushindi kinguvu alafu mtu anajinasib na 4 Ara huku rushwa zinamwagwa na maigizo kibaoo!!
 
Pumzi mbona imekata mapema?

Yaani uchaguzi 2025 oct, RUSHWA unagaiwa apr 2024😀
 
Back
Top Bottom