kavulata
JF-Expert Member
- Aug 2, 2012
- 13,778
- 14,214
Nadhani kuna tatizo la Zanzibar ndani ya muungano hata kama ni hairuhusiwi watu kusema hivi.
Sijui tunamsubiri nani aje kututatulia shida hii.
Nilikuwa ninafuatilia mashindano ya CECAFA kikamilifu yaliyomalizikia kwa Kenya kutwaa kombe na Zanzibar kuwa mshindi wa pili. Mimi nilikuwa nikishangilia timu zote za nyumbani Kilimanjaro na Zanzibar zinazoshiriki michuano ile. Baada ya Kili kutolewa nikahamia kikamilifu Zanzibar.
Lakini kilichokuwa kinanishangaza ni kuona watu wa Zanzibar wakiishabikia timu ya Zanzibar kama timu inayotoka Zanzibar pekee sio Tanzania. Hakuna pahala popote mashabiki na viongozi wa Zanzibar walikuwa wanaiona timu ya Zanzibar kama timu inayotoka Tanzania. Yaani Zanzibar ipo, inaweza na inatakiwa kuwepo.
Timu ya Zanzibar kufanya vizuri kwenye mashindano yale ilikuwa kama kilinge cha kuikweza Zanzibar kama Zanzibar kimataifa na sio Zanzibar ya Tanzania.
Kuna kitu watanzania tunatakiwa tukifanye sisi wenyewe kwa hiari yetu, uwazi na maelewano ili wazanzibari walidhike na waache kutafuta njia mbadala za kunung'unikia kama inavyofanyika sasa.
Hata kama tukijifanya ionekane kuwa hakuna tatizo tutaendelea kujidanganya sisi wewe, tatizo lipo bhana, na wakati ni huu wa kulitatua.
Sijui tunamsubiri nani aje kututatulia shida hii.
Nilikuwa ninafuatilia mashindano ya CECAFA kikamilifu yaliyomalizikia kwa Kenya kutwaa kombe na Zanzibar kuwa mshindi wa pili. Mimi nilikuwa nikishangilia timu zote za nyumbani Kilimanjaro na Zanzibar zinazoshiriki michuano ile. Baada ya Kili kutolewa nikahamia kikamilifu Zanzibar.
Lakini kilichokuwa kinanishangaza ni kuona watu wa Zanzibar wakiishabikia timu ya Zanzibar kama timu inayotoka Zanzibar pekee sio Tanzania. Hakuna pahala popote mashabiki na viongozi wa Zanzibar walikuwa wanaiona timu ya Zanzibar kama timu inayotoka Tanzania. Yaani Zanzibar ipo, inaweza na inatakiwa kuwepo.
Timu ya Zanzibar kufanya vizuri kwenye mashindano yale ilikuwa kama kilinge cha kuikweza Zanzibar kama Zanzibar kimataifa na sio Zanzibar ya Tanzania.
Kuna kitu watanzania tunatakiwa tukifanye sisi wenyewe kwa hiari yetu, uwazi na maelewano ili wazanzibari walidhike na waache kutafuta njia mbadala za kunung'unikia kama inavyofanyika sasa.
Hata kama tukijifanya ionekane kuwa hakuna tatizo tutaendelea kujidanganya sisi wewe, tatizo lipo bhana, na wakati ni huu wa kulitatua.