Zanzibar 2020 Zanzibar wapiga kura ya mapema. Makundi yanayoshiriki ni Watumishi wa ZEC na Vyombo vya Ulinzi na Usalama (Oktoba 27, 2020)

Kura ya mapema ukiitafakari vema ni UIZI mtupu. Eti makundi maalum yakapige kura ya wawakilishi na Raisi wa Zanzibar Leo, kisha kesho yarudi tena yakapige za nafasi za Muungano..!!!
Hapo ndo utamjua Maalim Seif yupo kundi gani. Aliondoa wawakilishi wake wasigombee ili Baraza libaki na CCM peke yao wapitishe Sheria wanazozitaka na wamepitisha Sheria leo anakuja kuwadhihaki ACT wazalendo eti hajui kwanini Kuna uchaguzi wa awali wakati yeye ndio alisababisha hiyo Sheria ipitishwe bila kupingwa.

Wapinzani mnapata taabu Sana kwa kujali matumbo yenu.
 
Afadhali wewe umewaambia ukweli chadema maana wasije sema wameibiwa kura wakati watakazopata ndo hizohizo.
Safi Sana kwa kuwa mkweli.
 
Kura zinapigwa mara mbili kuwapa vyombo vya ulinzi na usalama nafasi ya kuhudumu vizuri siku ya kesho, sasa mnapo vuruga na siku ya leo mnaendelea kuthibitisha kuwa mnapenda vurugu na walioweka siku mbili tofauti walikuwa sahihi kabisa
Wanaoelewa hiyo dhana wengi ni Saa Mbovu. Haiingii akilini wapiga Kura 500,000 tu mnatofautishe Siku za Kupiga Kura. Je wanaosimamia wapigakura 29,000,000 wa NEC pamoja na Vyombo vya wizi na uhasama watapiga Kura lini?? Au Huku bara Vyombo vya Dola na hao watumishi wa NEC hawatapiga Kura?
 
Huko Zanzibar kila kituo kikimaliza kupiga kura kihesabu kwenye kitabu kimetoa karatasi ngapi za kupiga kura kibaki na hiyo idadi kesho kabla hazijahesabiwa zikaguliwe Kama zinaendana na kitabu idadi yake ndo zichanganywe ikiwa vinginevyo waweke record hiyo ya wizi, na hao wanaopiga leo hawachovi wino? Ili kesho wasijirudie? Ndo vitu vya kufatilia Sasa hivi ili hata ukiwekwa Kati uweze kuonyesha mashaka yako yaliyonamsingi hata kwa wasomi na Dunia.
 
Sasa kwanini Shein naye anapiga kura leo? Ile clip ya Mwinyi itamghalimu.
 
Mnaibiwa vipi wakati mna mawakala?
Vijana wa CCM walioletwa kutoka Tanganyika wameanza kupiga Kura jana usiku huku wakibebwa kwenye Magari ya Polisi
Uzuri ni kwamba Zanzibar ni Visiwa na wanajuana kwa Sura na ubini Magufuli aache Wizi yeye si anasema anapendwa anamuweka ndani hata Upendo na wanamtomasatomasa
 
Ushahidi juu ya haya? Picha,video na hata sauti.
 
Kura zinapigwa mara mbili kuwapa vyombo vya ulinzi na usalama nafasi ya kuhudumu vizuri siku ya kesho
Bara hakuna Vyombo cha Usalama na Ulinzi?mbona hatupigi mara mbili?
 
Kura zinapigwa mara mbili kuwapa vyombo vya ulinzi na usalama nafasi ya kuhudumu vizuri siku ya kesho, sasa mnapo vuruga na siku ya leo mnaendelea kuthibitisha kuwa mnapenda vurugu na walioweka siku mbili tofauti walikuwa sahihi kabisa

Usiku wa Leo kura zinalala kwa Nani?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…