Zanzibar: Watalii wanne kutoka Israeli watimuliwa Hotelini kwa kulalamika kuhusu gari kuandikwa "Free Palestine"

Taifa linapaswa kupokea watalii wasio wendawazimu ili kuepukana na kadhia mbalimbali.

Ni vyema viwanja vya ndege viwe vinapima kwanza akili watalii kabla ya kuwa ruhusu kuingia nchini vichaa dunia hii wanazidi kuwa wengi.
Okey.
 
Hapana. Katika hili utatengeneza tatizo kubwa sana iwapo hali itafikia hatua ya kwamba kuna hoteli team palestina na hoteli team Israel.
Hata zikiwepo hakuna tatizo kwani ni mambo mangapi mmeweka matabaka na wala hamfikiri kuyavunja ?!.
 
Acha utumwa, kwani si kila mtu ana uhuru wake. Angefanyia Israel walikuwa na haki lakini sisi hatuna chuki na Palestina kwa nini wao watulazimishe kuwachukia.
Umahiri,umakini na kumjali mteja siyo utumwa.Hata Waizraeli hawana chuki na sisi.Kwa nini Wapalestina watufanye tuwachukie Waizraeli?
 
Kwa hiyo ile ni hoteli au kituo cha wapigania "uhuru"?
Ukristo Fake usiofahamu biblia unakusumbua! Yaani bila aibu unaweka kifunga na kifungua semi kwenye neno uhuru? Btw, hadi uhoji kama ni kituo cha kupigani uhuru; kwani umeambiwa hao Wayahudu wenzako walikuta mafunzo ya kijeshi?!
 

Kama kweli walifukuzwa hotelini kwa sababu tu ya kutaka kujua usalama wao, then huo ni unyanyasaji...

Wayahudi na Wapalestina huwa hawakai chungu kimoja, na mara nyingi Myahudi akishajua kuna Mpalestina maeneo alipo na si salama kwake, huwa anajitenga na eneo hilo...

they were eventually kicked out after complaining that the vehicle was causing them "concern."

Sentensi hii inaonesha kabisa hao Wayahaufi walitaka tu kujua usalama wao ukoje, maana haioneshi kama walianzisha timbwili au fujo yeyote...
 
Timu mnaleta ninyi katika mazingira ya kawaida watu kutofautiana tamaduni, mitazamo, dini, idikadi za kisiasa na mengineyo ..ni kawaida sana hivyo kama unaona hapafanani na wewe ondoka tu au jaribu kuwa na tolerance na utaratibu wa eneo husika..
Ujinga ujinga tu. Huwezi jenga banda la nguruwe mbele ya msikiti sababu wewe ni mkatoliki na una mitazamo yako na kiwanja ni chako.
 
Bro nitakupa mfano, ile sikukuu ya Xmas Hotel kibao mwezi mzima zinapambwa na kuendeshwa ki Xmas, hadi wafanyakazi unakuta wanavaa mavazi ya ki_xmas, na wakati wote huo si kwamba hotel haipokei wenye mitazamo tofauti na uwepo na Xmas na si kwamba hawakwaziki, bali wamechagua kunyamaza...

Hawataki kujiweka kwenye umuhimu ambao hata hautowasaidia wakiwa ndani ya nchi ya watu na ni kwasababu wanajua hiyo ni hotel inahost watu tofauti tofauti... Hao waisraeli ni hulka yao ya ukorofi na kujikweza na kutaka kuogopwa na kuhurumiwa kila waendako

Niliuliza huko juu, hiyo gari ingekuwa ni ya mgeni hapo hotelini, wangeenda kugombana na mgeni mwenzao..??
 
Wana haki ya kuishi, sio kuuliwa kama kuku na kufanywa watumwa.
Nasi waafrika tulikuwa na haki ya kuishi sio kubebwa kwenye magunia kama mbuzi tukapigania tukaupata uhuru wa kwanza.

Wapalestine wapo njia sahihi
 
Hao wanatoa hela? Hao wanajua ku spend hela?
Hilo sijui mkuu. Ninachojua nchi inahitaji watalii na tunawahudumia kwa usawa. Zanzibar inapokea hadi mashoga ya kizungu na inayapa huduma na meneja haweki stika za kupinga ushoga kwenye gari yake.
 
Ukristo Fake usiofahamu biblia unakusumbua! Yaani bila aibu unaweka kifunga na kifungua semi kwenye neno uhuru? Btw, hadi uhoji kama ni kituo cha kupigani uhuru; kwani umeambiwa hao Wayahudu wenzako walikuta mafunzo ya kijeshi?!
Mambo ya ukristo umeyaandika wewe dugu yangu veve!Hiyo ni hoteli na inapaswa kuwa strictly for businesses. Siyo kuanzisha harakati za kisiasa hotelini!Mind you,big fella!
 
Unless tunataka watalii kutoka nchi za kiarabu tu.
Acha kujidanganya! Hao Zionists wanapingwa na nchi kibao tu! Tumebaki Miafrika tunaoshindwa kutofautisha kati Ukristo, Judaism, Jews na Zionists. Hata nchi zinazowaunga mkono, huo uungaji mkono ni wa serikali zao; na hizo serikali zao zinafanya hivyo kutokana kuona Israel ndie Mshirika pekee unayeweza kumtegemea na kummwanini kwa 100% kwa Mashariki ya Kati.
 
Watu wanajisahau sana, kama hawakupendezwa na hilo wangehama hoteli kimyakimya na sio kuanzisha fujo. Upo nchi za watu unataka kupangia watu maisha?

Bendera imebandikwa juu ya gari na sio kwenye vizimba au kuta za hoteli...

Kwa muisrael yeyote ambaye yupo ugenini lazima awe concerned kwenye situation kama hiyo, what if ni gari la Wapalestina kweli nao wapo hapo hotelini kwa nia ya kulipiza kisasi?

Hao watalii wameuliza tu ili kuhakikishiwa usalama wao, soma vizuri hii habari...
 
Ujinga ujinga tu. Huwezi jenga banda la nguruwe mbele ya msikiti sababu wewe ni mkatoliki na una mitazamo yako na kiwanja ni chako.
Hakuna ujinga kwenye miliki ya kiwanja chake unless wewe ndie mjinga mwenyewe uliyekubuhu kwa sababu naye anaweza kuona msikiti unamleta makele kwake.
 
Nasi waafrika tulikuwa na haki ya kuishi sio kubebwa kwenye magunia kama mbuzi tukapigania tukaupata uhuru wa kwanza.

Wapalestine wapo njia sahihi
MM sisemi wapalestina wanahaki ya kinachowakuta. Siongozwi na mihemko ya kidini. Ninachosema ni meneja kuwa chawa wa palestina kwa wateja wa kiisrael si sawa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…