Zanzibar: Watalii wanne kutoka Israeli watimuliwa Hotelini kwa kulalamika kuhusu gari kuandikwa "Free Palestine"

Mtu asipoelewa hapa ana kichwa kigumu mnooo.
 
Sahihi.Wanafanya kazi kwa hisia za chuki tu.Wamelishwa mambo ya hovyo sana.Kuna maswali ya kujiuliza;-
-kwamba hakuna Muizraeli mwenye utu?
-kwamba kwenye hizo hoteli wahudumu na wamiliki hawajawahi kutofautiana na wateja wa mataifa mengine isipokuwa ni hao tu Waizraeli?
-Walikusudia kufikisha ujumbe gani kwa jamii?
-Wanatuhakikishiaje kwamba wameonewa na si habari zenye nia ovu?
-Walitegemea taarifa hii itafika kwa watu wenye kuchambua mambo in and out?
-Wanajua madhara hasi kwao kwa habari kama hizo?
-Walijipanga au ni habari imetokea tu?
-Tutegemee nini? N.k.
 
Huyo Manager na wahudumu hawajasoma kozi ya Sales and Marketing?
 
Mwendawazimu ni meneja anayempokea muisraeli ili ambandikie matangazo kuwa mie adui yako.
Adui yake ni sticker.

Huyu ni zaidi ya mwendawazimu kama inafika stage ya kujenga uadui mpaka na sticker
 
HEEEEEE! Yaani mtu kaweka kwenye gari lake halafu unasema kosa lake ni kuwaonesha Waisraeli kuwa yeye ni adui? Nitakueleza kama nilivyowaeleza wenzako. Hao ma-Extremists wangekuwa na haki ya kuhoji endapo stika ingekuwa INAPINGA uwepo wa Taifa la Israel lakini sio kupinga ku-advocate uhuru wa taifa linalotambuliwa na sheria za kimataifa! Extremism is extremism is extremism; iwe Islamic Extremism, Jewish Extremism or Hindu Extremism! Wanaopinga Free Palestine ni Jew Extremists and not any Jew!
 
Adui yake ni sticker.

Huyu ni zaidi ya mwendawazimu kama inafika stage ya kujenga uadui mpaka na sticker
Kwani utatumia kipimo gani kupima kiwango cha chuki aliyonayo muweka stika dhidi ya wauaji wa wapelistina?
 
Hawajauzingatia msemo "mteja ni mfalme"
 
Watu wanajisahau sana, kama hawakupendezwa na hilo wangehama hoteli kimyakimya na sio kuanzisha fujo. Upo nchi za watu unataka kupangia watu maisha?
Kwani kati ya hiyo hoteli na hao Wazungu nani anayemuhitaji mwenzake?
 
Hapa tunaangalia usalama wa biashara ya utalii sio haki za uanaharakati wa kivita, kidini au kisiasa.

Kosa linapimwa kwa matokeo, matokeo ya kufanya harakati za kivita kwa upande A ni kupoteza wateja wa upande B na tunahitaji wateja wote A na B na ndipo kosa la meneja lilipo.
 
Watu wanajisahau sana, kama hawakupendezwa na hilo wangehama hoteli kimyakimya na sio kuanzisha fujo. Upo nchi za watu unataka kupangia watu maisha?
Kwani kati ya hiyo hoteli na hao Wazungu nani anayemuhitaji mwenzake?
 
Kwa nini nipime chuki ?
Sababu wewe ni mpalestina, mwenyeji wako anayekuhudumia amekuonyesha kupitia stika kuwa anaisapoti israeli na hujui kiwango chake cha chuki dhidi ya palestina kitaishia kwenye stika tu au atakuwekea na sumu.
 
Sababu wewe ni mpalestina, mwenyeji wako anayekuhudumia amekuonyesha kupitia stika kuwa anaisapoti israeli na hujui kiwango chake cha chuki dhidi ya palestina kitaishia kwenye stika tu au atakuwekea na sumu.
Hebu soma tena ulicho andika sikuelewi hata unaandika nini ?
 

Hawa waiz-rael wanataka kutupangia vitu vya kubandika kwenye magari.
Mbona wenyewe kwao wakiweka upinde hakuna wa kuwagusa.
 
Walifanya fujo au walilalamika?

Kulalamika si kosa. Ni njia mojawapo ya kufikisha ujumbe. Watu wa Business and Public Administration wanalifahamu hilo.

Uongozi wa hoteli ulipaswa kuwasikiliza clients wao hata kama ni kwa "unafikiri". Ukimkwaza mteja mmoja anaweza kukupotezea wateja zaidi ya saba. Kwa walio makini na biashara zao, hawawezi kukubali hilo. Huzilinda biashara zao mithili ya mboni za macho.
 
Umepiga penyewe. Kuna hoteli moja Arusha(sijafika, nimesimuliwa na rafiki yangu), wao wameamua kuwajaza Wakenya mpaka walinzi wa getini baada ya kuona kuwa Watanzania "wanazingua".

Unaambiwa hiyo hoteli mpaka walinzi wa getini wanao uelewa wa "customer care", na wanapractice effectively.
 
Tukuelekeze walipo upite nao? Mtaalamu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…