Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
Simulizi : ZAWADI TOKA IKULU
Mwandishi : EMMANUEL VENANCE
Imeletwa kwenu na: BURE SERIES
Sehemu ya 1
Ni jumapili tulivu sana ambayo imejidhihilisha tangu jua linachoza, kwani hakukuwa hata na dalili ya wingu angani kukionekana safi na kumependeza kwa rangi ya bluu bahari.
Baada ya kutoka kanisani nilikaa nyumbani kwangu nikiwa mpweke kani nilikuwa peke yangu. Nyumba niliiona kubwa mno kwasababu kila nilipokanyaga nilikuwa peke yangu, sina wakuongea naye wala kushirikiana naye kwa lolote lile, hali iliyonipa hudhuni wakati wote.
Nimezoea kusndinda kazini na nikirejea hapa nyumbani huwa nimechoka nafikia kulala, lakini kwa siku za mwisho wa wiki huwa ni ngumu sana kwangu maana inanilazimu kushinda nyumbani, kwasababu huwa hatuendi kazini. Na leo ni moja ya siku hizo nisizozipenda katika maisha yangu.
Nilijaribu kufanya hiki na kile lakini haikuwezekana na baada ya muda mfupi kidogo niliamua kutoka nyumbani kwangu maeneo ya Busweru. Nilitaka nitafute sehemu ya kwenda kupumzika yaani kujichanganya na marafiki angalau tubadilishane mawazo.
Baada ya mwendo mfupi nilipokuwa nikitembea huku nikiwaza pakuanzia niliona ni bora nikamtembelee swahiba wangu wa nguvu bwan Domini Martin Kalyanze. Niliamua kumpigia simu kwanza ili nijue kama yupo nyumbani kabla sijaanza safari. Bila shaka majibu ya hiyo simu yalikuwa sawa na matarajio yangu rafiki yangu alikuwepo nyumbani na alikuwa tayari nionane naye.
Dominic ni mfanyakazi mwenzangu ni mkurugenzi wa Mauzo katika kampuni ya mawasiliano ya simu za mkononi ya Vodacom Kanda ya ziwa. Na mimi ni Meneja wa mauzo, si hilo tu lililotufanya tushibane na kuwa marafiki lakini Martin ni rafiki yangu tuliye soma pamoja Pale IFM chuo cha usimamizi wa fedha na tuliomba kazi pamoja na bahati nzuri tukaajiriwa siku moja na sehemu moja, hivyo niseme wazi kuwa huyu jamaa tunapendana sana tena sana.
Nilifika kwa Dominic nikakuta anajiandaa kwa kufuta vumbi gari lake lakini aliponiona aliniangalia sana na kutikisa kichwa, nilimuuliza “kwani vipi kaka mbona kukodoleana macho hivyo?
“mbona umekuja kwa miguu?” Dominic alihoji.Nilimjibu kwa maneno yaliyoambatana na kicheko.
“Aaah! ndugu yangu sijali, sijisikii kuendesha leo kwahiyo nimepanda daladala nikashuka hapo kituoni maana siyo mbali kuja hapa, nimeona pia niwape ridhiki makonda wetu si unajua ndiyo waliotulea toka tunasoma chekechea kwenda shule na kurudi mpaka hapa tulipo leo?. Na pia huu ni usafiri wa umma bwana, tusivimbe saana na vigari vyetu tukajisahau maana tukumbuke kuna kupanda na kushuka ipo siku tunaweza urudi kwenye haya maisha sasa yanini kujikweza” Baada ya majibu hayo wote tuliangua kicheko na tukasalimiana na kuingia ndani. Tulipiga stori mbili tatu kabla ya kupata kifungua kinywa, na baada ya zoezi hilo kuisha tuliamua kutoka.