Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #21
21.
Ilinibidi kubadilisha mikao kwanza mana sasa nilikuwa naongea na serikali, kwani ni mtoto wa rais namzungumzia mwana wa mtawala wa taifa hili, namaanisha mwana wa mkuu wanchi hii daah!. Kwa tafsiri nyepesi ni mtawala wa watoto pia katika nchi hii ana sauti kuliko spika za tamasha la mziki.
Nilianza kutetemeka ghafula maana sikuwa na amani tena moyoni mwangu, sikuwa najiamini tena niliona matatizo nayatafuta tena kwa miguu miwili. Tukiachana tu na kile cheo chake cha Urais cha baba yake, kiongozi wetu ana maamzi magumu kuliko hata chuma cha pua, ni mkali zaidi ya moto wa gesi, ukimchokoza hana huruma kama tanulu la tofali.
Ila uzuri nikwamba taarifa hutufikia sisi wananchi juu ya yale anayoyaamua kwa watu wanaokwenda kinyume na matakwa yake, kwani anastaili zake za kuwanyoosha wale wanaomchokoza. Chakushangaza zaidi nilijiona na mimi nilikuwa nimejiandaa kumchokoza, nilikuwa namtafuta ugomvi, nikama nimeamua kushusha mbendera ya taifa iliyo katikati ya kambi ya jeshi tena mchana kweupe.
Nilijiona ninagonga geti la ikulu huku nimelewa na nikitoa matusi machafu najua unakijua kitakachofuata. Bado niliona nnachotaka kukifanya ni kuweka kiganja cha mkono kwenye domo la nguruwe mwenye njaa kali na kitakachotokea ninakijua.
Niligundua nilichokuwa nakifanya ni sawa na kukwea mnazi ukweni huku nimefungamsuli na ndani pakiwa patupu kitakachotokea ni fasihi simulizi itakayodumu milele na milele.
Ulifuata ukimya na ulikuwa ni ukimya wa kustajabisha, wakati nikiyawaza hayo kumbe Jesca alikuwa akinisemesha kwa muda, sikumsikia nilikuwa mbali kimawazo, maana tayari ameesha iharibu kabisa siku yangu. Ninampenda Jesca wangu lakini naanzaje kumueleza hilo?. Mtoto wa Rais sistahili hata kukigusa kiganja cha mkono wake, hivi itakuwaje nikimwambia harafu akakataana kunikasirikia si nitafia jela mimi?. Hudhuni majonzi na kukata tama kulitanda moyoni, mawazo yangu yote yalijikita upande hasi,. Niliwaza tena au akikubali harafu yule mzee akajua itakuwaje?. Jamie we Jamie. Umekuwaje . Hivi unanisikia kweli?.. sikuwa nasikia muda wote huo Jesca alioniita sana na sasa aliamua kuja kunigusa nikashituka kama mtu aliyekuwa usingizini. Jesca alikuja karibu yangu akaketi huku akinipapasa shavuni aliniuliza vipi unaumwa?.... mbona umekuwa hivi ghafla jamani? duh! mikono laini iliusisimua mwili wangu na kujikuta naishiwa nguvu, lakini sauti laini nyembembe na tamu ikaiburudisha nafsi yangu.
Nilihisi nabembelezwa mimi, nilihisi kudeka kwa muda kitu ambacho nimekuwa sikipati kwa muda penzini, nilikuwa nikiisikia sauti yake juu ya kifua change ikiniburudisha, natamani awe wangu natamani sana, nilijihisi niko peponi.
Lakini nilipomkumbuka Mh. Rais na heka heka zake sikuwa na chakumjibu nilinyanyuka na kuamua kuondoka kabisa nikitembea kwa mwendo wa unyonge usiyoweza kuelezeka.
Kwa kifupi nilikuwa nimevurugwa, niliufungua mlango na kutoka nje nilikutana na wasichana wawili warembo waliovalia vizuri suti za kijivu na miwani myeusi. Walionekana si watu wa kawaida kimuonekano tu. Bila shaka walikuwa ni walinzi wa Jesca, sasa naanza kupata picha halisi na nilianza kuyaamini macho na masikio yangu.
Ilinibidi kubadilisha mikao kwanza mana sasa nilikuwa naongea na serikali, kwani ni mtoto wa rais namzungumzia mwana wa mtawala wa taifa hili, namaanisha mwana wa mkuu wanchi hii daah!. Kwa tafsiri nyepesi ni mtawala wa watoto pia katika nchi hii ana sauti kuliko spika za tamasha la mziki.
Nilianza kutetemeka ghafula maana sikuwa na amani tena moyoni mwangu, sikuwa najiamini tena niliona matatizo nayatafuta tena kwa miguu miwili. Tukiachana tu na kile cheo chake cha Urais cha baba yake, kiongozi wetu ana maamzi magumu kuliko hata chuma cha pua, ni mkali zaidi ya moto wa gesi, ukimchokoza hana huruma kama tanulu la tofali.
Ila uzuri nikwamba taarifa hutufikia sisi wananchi juu ya yale anayoyaamua kwa watu wanaokwenda kinyume na matakwa yake, kwani anastaili zake za kuwanyoosha wale wanaomchokoza. Chakushangaza zaidi nilijiona na mimi nilikuwa nimejiandaa kumchokoza, nilikuwa namtafuta ugomvi, nikama nimeamua kushusha mbendera ya taifa iliyo katikati ya kambi ya jeshi tena mchana kweupe.
Nilijiona ninagonga geti la ikulu huku nimelewa na nikitoa matusi machafu najua unakijua kitakachofuata. Bado niliona nnachotaka kukifanya ni kuweka kiganja cha mkono kwenye domo la nguruwe mwenye njaa kali na kitakachotokea ninakijua.
Niligundua nilichokuwa nakifanya ni sawa na kukwea mnazi ukweni huku nimefungamsuli na ndani pakiwa patupu kitakachotokea ni fasihi simulizi itakayodumu milele na milele.
Ulifuata ukimya na ulikuwa ni ukimya wa kustajabisha, wakati nikiyawaza hayo kumbe Jesca alikuwa akinisemesha kwa muda, sikumsikia nilikuwa mbali kimawazo, maana tayari ameesha iharibu kabisa siku yangu. Ninampenda Jesca wangu lakini naanzaje kumueleza hilo?. Mtoto wa Rais sistahili hata kukigusa kiganja cha mkono wake, hivi itakuwaje nikimwambia harafu akakataana kunikasirikia si nitafia jela mimi?. Hudhuni majonzi na kukata tama kulitanda moyoni, mawazo yangu yote yalijikita upande hasi,. Niliwaza tena au akikubali harafu yule mzee akajua itakuwaje?. Jamie we Jamie. Umekuwaje . Hivi unanisikia kweli?.. sikuwa nasikia muda wote huo Jesca alioniita sana na sasa aliamua kuja kunigusa nikashituka kama mtu aliyekuwa usingizini. Jesca alikuja karibu yangu akaketi huku akinipapasa shavuni aliniuliza vipi unaumwa?.... mbona umekuwa hivi ghafla jamani? duh! mikono laini iliusisimua mwili wangu na kujikuta naishiwa nguvu, lakini sauti laini nyembembe na tamu ikaiburudisha nafsi yangu.
Nilihisi nabembelezwa mimi, nilihisi kudeka kwa muda kitu ambacho nimekuwa sikipati kwa muda penzini, nilikuwa nikiisikia sauti yake juu ya kifua change ikiniburudisha, natamani awe wangu natamani sana, nilijihisi niko peponi.
Lakini nilipomkumbuka Mh. Rais na heka heka zake sikuwa na chakumjibu nilinyanyuka na kuamua kuondoka kabisa nikitembea kwa mwendo wa unyonge usiyoweza kuelezeka.
Kwa kifupi nilikuwa nimevurugwa, niliufungua mlango na kutoka nje nilikutana na wasichana wawili warembo waliovalia vizuri suti za kijivu na miwani myeusi. Walionekana si watu wa kawaida kimuonekano tu. Bila shaka walikuwa ni walinzi wa Jesca, sasa naanza kupata picha halisi na nilianza kuyaamini macho na masikio yangu.