Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #61
55.
Nilitafakari sana juu ya maisha yangu, inawezekanaje kila ninapokaribia kuipata furaha matatizo huibuka tena na kunikatisha tamaa. Inamaanisha katika maisha yangu haitatokea siku nikawa na furaha hasa katika mapenzi. Nimetafuta pesa kwa nguvu zote na bado najaribu kuitafuta kwa hali na mali lakini bado furaha kwangu limebaki kuwa neno la kichina lililoandikwa kwa lugha ya kichina kwa upeo wangu stokaa nilisome katu.
Sikutaka kuyasikia maneno yaliyosemwa na Jesca yaliniumiza mno, nadhani kwa mara ya kwanza katika mapenzi nakutana na jeraha kubwa lenye maumivu makali moyoni mwangu.
Naweza kusema sikuhii ilikuwa ni moja ya siku zilizoharibu furaha yangu na kuyaona maisha niliyonayo na pesa nilizonazo si lolote na si chochote. Sikuwa na amini kuwa ipo siku nitaikosa furaha kwa kulikosa penzi la Jesca kipenzi changu, lakiniu leo imetimia. Nilijiona sina mbele wala nyuma, kushoto wala kulia. Hakuna maumivu mabaya kama kumpoteza unayempenda tena kizembe, naweza kusema nimempoteza kizembe sana mpenzi wangu.
Wakati kichwa kiuma kwa mawazo simu iliita na nilipoitazama alikuwa inaonesha jina la Jesca Manguli, sikuipokea maana moyo wangu ulikuwa unaniuma mno kumpoteza mpenzi wangu niliyempenda kwa dhati. Simu ilizidi kunisumbua na sikutaka kabisa kuipokea maana moyo wangu umeesha umia na sikutaka kuumiza tena. Kulingana na hali niliyokuwa nilijikuta nikiiogopa kabisa simu yangu. Simu iliyokuwa ikiita muda wote na sikutegemea kuipokea lakini kulinganza na usumbufu na kutokuchoka kwa mpigaji nilijikuta nikiipokea.
“vipi Jesca mbona usumbufu rafiki yangu?”
“Usinichukie Jamie najua umeumia sana juu ya tarifa nilizokupa, najua umechukia kuliko kawaida kumbuka haya yote sikuyapanga mimi ni tofauti zetu na kukosekana kwa mawasiliano na ushahidi wa kutosha ndo kilichotufikisha yatokee haya”
“najua Jesca lakini ukashindwa kweli kunisubiri japo dakika moja tu…. Yani moja tu mpenzi yangu” niliongea kwa kwikwi huku machozi yakinitoka.
“Nikweli inauma na naweza kusema nibora kungekuwa na mawasiliano lakini ujinga wangu wakutokukusikiliza ona sasa naumia mwenzio nitaiweka wapi mimi sura yangu, nitamueleza nini mimi baba yangu mpaka akanielewa, huu ni mtihani na najuta kukutenda mpenzi wangu.”
“No!... usiseme hivyo Jesca wangu hakuna aliyejua nini kinaendelea katika maisha yetu.”
“nikweli Jamie mimi ndo chanzo ningekusikiliza haya yote yasingetokea ona sasa nilijifanya mwenye hasira na leo ona ninakupoteza mpenzi wangu inaniuma sana mme wangu niliyekutarajia, leo sina haki yakukupata tena?”
“Nakuomba mpenzi wangu, nakuomba tafadhali haya yamesha pita tafadhari acha kulia, acha kulaumu Mungu atakusaidia hata huyo uliyempata atakuwa mme mwema kwako, naamini mnapendana na Mungu atawasimamia” najua nilikuwa ninaumia kuliko kawaida ila sikuwa na budi kumpa moyo.
Mazungumzo yetu yalitawaliwa na vilio hayakuwa mazuri, ila uchungu kwa kila mmoja wetu, Jesca ilimuuma sana kunipoteza na hata mimi iliniuma sana kumpoteza. Kulingana na vilio kutawala mazungumzo yetu hayakudumu ,yalishindikana na vilio vikashika nafasi. Hakuna aliyekumbuka kuzima simu iliendelea kuwa hewani, huku tukiendelea kulia kwa uchungu hakuna aliefurahishwa na kilichokuwa kikiendelea kati yetu. Naamini kila mtu alitamani penzi letu lirejee lakini haikuwa kazi rahisi.
Nilimuomba Jesca avunje uhusiano, alikataa na akautaja ugumu wa kuvunja uhusiano huo na nilimuelewa maana kulikuwa na ugumu na ulikuwa ni ugumu kweli. Jesca aliniambia ameingia kwenye mahusiano na mtoto wa kiongozi wa zamani wa nchi hii ambaye amewahi kuitumikia kama waziri mkuu miaka ya zamani na sasa ni bilionea Kenedy Gao mtoto wake ajulikanaye kwa jina la Pius Von Gao ndiye hasa alitaka kumuoa Jesca.
Von Gao alipomuona alimtuma baba yake nyumbani kwao Jesca kulingana na ukaribu uliokuwepo kati yake na baba yake Jesca ilikuwa rahisi sana kushawishika na kujikuta akiingia kwenye mahusiano. Kulingana na kuwa yuko single kwa kipindi hicho hakuona sababu ya kumuangusha baba yake alikubali. Ukaribu wa familia zao ndiyo uliolirahisisha swala hili na pia Jesca alikuwa akitafuta furaha na aliamini huenda Von Gao anaweza kutoa furaha kubwa kwa Jesca.
Mazungumzo yaliyofanyika kutoka pande zote mbili yalifikia mwisho na makualiano ya mahali yalifikiwa. Jesca alitolewa mahali kimyakimya. Nihadithi aliyonisimulia na iliniumiza mno, aliendelea kusema kuwa “Von Gao ni mtu ambaye haishi hapa nchini na siwezi kusema kuwa namfahamu kiundani zaidi ya kumjua juu juu tu.
Niliamua kuolewa tu kwasababu nilijua umeniumiza na niliamini sina mpenzi kwa wakati huu. Jamie umerejea na wewe ndiye mtu pekee katika maisha yangu niliekuchagua na kukulidhia bila shuruti uwe mpenzi wangu naamini Mungu alikuwa na maksudi nasisi lakini huenda nimeharibu, na ninaamini nimevuruga.
Natamani kuurudisha moyo wangu lakini kunakitanzi kimening’inizwa mbele yangu. Nitamueleza nini baba yangu na nitaipokeaje hali hii, mbaya zaidi nilikubali kwa hiali yangu sasa itakuwaje na nitawashawishi vipi wazazi wangu kuliahilisha zoezi hili.
Naamini siyo kitu kidogo hili ni tatizo kubwa na utatuzi wake unahitaji busara wala siyo nguvu. Niliamini ukitumia nguvu unaweza kuharibu kila kitu.” Nikweli alikuwa na kitanzi shingoni familia ya Rais ni familia mashuhuri mno, kuvunja uchumba ambao tayari wazazi wameshiriki kwa asilimia miamoja na mhusika alikubali itakuwa ni skendo kubwa kuwahi kutokea. Kwa unyonge niliamini hapa sina changu na nilikuwa mpole na kukubaliana na maelezo.
Ilikuwa ni siku ya Jumamosi nilifika ofisini kwangu majira ya saa mbili asubuhi mitaa ya Karuta Katikati ya jiji la Mwanza hapa ndipo yalikuwa makao makuu ya Himaya ChapaKazi niliegesha gari langu na nilipo ingia ndani mapokezi nilimkuta msichana mrembo kajiinamia nilimsogerea maana alikuwa peke yake.
Nilimgusa alipoinua uso alikuwa ni Jesca Manguli kwanza nilishituka maana ni kitu amabacho sikukitarajia kabisa. Nilimwinua na kumkumbatia kwa nguvu alikuwa akilia na nilipomkumbatia alilia kwa nguvu kiasi kwamba wafanyakazi wangu baadhi walitoka ofisini wakitaka kujua nini kinaendelea.
Kwa kifupi sikuona kama ni hali nzuri kuwepo pale nilijikaza nikamshika mkono, Jesca nikamuingiza kwenye gari sikutaka mazungumzo naye niliwasha gari na safari ilielekea nyumbani kwangu Isamilo ambako nimehamia hivi karibuni baada ya kununua nyumba karibu na kituo cha utafiti wa magonjwa ya mifugo na binadamu. Nilimkaribisha ndani ya jengo langu la kifahali nilililinunua toka kwa mmiliki wake wa awali shirika la Care international na ilikuwa ni nyumba ya mkurugenzi wa shirika hili nchini Tanzania ambaye alihamisha makazi yake hapa jijini.
Nilitafakari sana juu ya maisha yangu, inawezekanaje kila ninapokaribia kuipata furaha matatizo huibuka tena na kunikatisha tamaa. Inamaanisha katika maisha yangu haitatokea siku nikawa na furaha hasa katika mapenzi. Nimetafuta pesa kwa nguvu zote na bado najaribu kuitafuta kwa hali na mali lakini bado furaha kwangu limebaki kuwa neno la kichina lililoandikwa kwa lugha ya kichina kwa upeo wangu stokaa nilisome katu.
Sikutaka kuyasikia maneno yaliyosemwa na Jesca yaliniumiza mno, nadhani kwa mara ya kwanza katika mapenzi nakutana na jeraha kubwa lenye maumivu makali moyoni mwangu.
Naweza kusema sikuhii ilikuwa ni moja ya siku zilizoharibu furaha yangu na kuyaona maisha niliyonayo na pesa nilizonazo si lolote na si chochote. Sikuwa na amini kuwa ipo siku nitaikosa furaha kwa kulikosa penzi la Jesca kipenzi changu, lakiniu leo imetimia. Nilijiona sina mbele wala nyuma, kushoto wala kulia. Hakuna maumivu mabaya kama kumpoteza unayempenda tena kizembe, naweza kusema nimempoteza kizembe sana mpenzi wangu.
Wakati kichwa kiuma kwa mawazo simu iliita na nilipoitazama alikuwa inaonesha jina la Jesca Manguli, sikuipokea maana moyo wangu ulikuwa unaniuma mno kumpoteza mpenzi wangu niliyempenda kwa dhati. Simu ilizidi kunisumbua na sikutaka kabisa kuipokea maana moyo wangu umeesha umia na sikutaka kuumiza tena. Kulingana na hali niliyokuwa nilijikuta nikiiogopa kabisa simu yangu. Simu iliyokuwa ikiita muda wote na sikutegemea kuipokea lakini kulinganza na usumbufu na kutokuchoka kwa mpigaji nilijikuta nikiipokea.
“vipi Jesca mbona usumbufu rafiki yangu?”
“Usinichukie Jamie najua umeumia sana juu ya tarifa nilizokupa, najua umechukia kuliko kawaida kumbuka haya yote sikuyapanga mimi ni tofauti zetu na kukosekana kwa mawasiliano na ushahidi wa kutosha ndo kilichotufikisha yatokee haya”
“najua Jesca lakini ukashindwa kweli kunisubiri japo dakika moja tu…. Yani moja tu mpenzi yangu” niliongea kwa kwikwi huku machozi yakinitoka.
“Nikweli inauma na naweza kusema nibora kungekuwa na mawasiliano lakini ujinga wangu wakutokukusikiliza ona sasa naumia mwenzio nitaiweka wapi mimi sura yangu, nitamueleza nini mimi baba yangu mpaka akanielewa, huu ni mtihani na najuta kukutenda mpenzi wangu.”
“No!... usiseme hivyo Jesca wangu hakuna aliyejua nini kinaendelea katika maisha yetu.”
“nikweli Jamie mimi ndo chanzo ningekusikiliza haya yote yasingetokea ona sasa nilijifanya mwenye hasira na leo ona ninakupoteza mpenzi wangu inaniuma sana mme wangu niliyekutarajia, leo sina haki yakukupata tena?”
“Nakuomba mpenzi wangu, nakuomba tafadhali haya yamesha pita tafadhari acha kulia, acha kulaumu Mungu atakusaidia hata huyo uliyempata atakuwa mme mwema kwako, naamini mnapendana na Mungu atawasimamia” najua nilikuwa ninaumia kuliko kawaida ila sikuwa na budi kumpa moyo.
Mazungumzo yetu yalitawaliwa na vilio hayakuwa mazuri, ila uchungu kwa kila mmoja wetu, Jesca ilimuuma sana kunipoteza na hata mimi iliniuma sana kumpoteza. Kulingana na vilio kutawala mazungumzo yetu hayakudumu ,yalishindikana na vilio vikashika nafasi. Hakuna aliyekumbuka kuzima simu iliendelea kuwa hewani, huku tukiendelea kulia kwa uchungu hakuna aliefurahishwa na kilichokuwa kikiendelea kati yetu. Naamini kila mtu alitamani penzi letu lirejee lakini haikuwa kazi rahisi.
Nilimuomba Jesca avunje uhusiano, alikataa na akautaja ugumu wa kuvunja uhusiano huo na nilimuelewa maana kulikuwa na ugumu na ulikuwa ni ugumu kweli. Jesca aliniambia ameingia kwenye mahusiano na mtoto wa kiongozi wa zamani wa nchi hii ambaye amewahi kuitumikia kama waziri mkuu miaka ya zamani na sasa ni bilionea Kenedy Gao mtoto wake ajulikanaye kwa jina la Pius Von Gao ndiye hasa alitaka kumuoa Jesca.
Von Gao alipomuona alimtuma baba yake nyumbani kwao Jesca kulingana na ukaribu uliokuwepo kati yake na baba yake Jesca ilikuwa rahisi sana kushawishika na kujikuta akiingia kwenye mahusiano. Kulingana na kuwa yuko single kwa kipindi hicho hakuona sababu ya kumuangusha baba yake alikubali. Ukaribu wa familia zao ndiyo uliolirahisisha swala hili na pia Jesca alikuwa akitafuta furaha na aliamini huenda Von Gao anaweza kutoa furaha kubwa kwa Jesca.
Mazungumzo yaliyofanyika kutoka pande zote mbili yalifikia mwisho na makualiano ya mahali yalifikiwa. Jesca alitolewa mahali kimyakimya. Nihadithi aliyonisimulia na iliniumiza mno, aliendelea kusema kuwa “Von Gao ni mtu ambaye haishi hapa nchini na siwezi kusema kuwa namfahamu kiundani zaidi ya kumjua juu juu tu.
Niliamua kuolewa tu kwasababu nilijua umeniumiza na niliamini sina mpenzi kwa wakati huu. Jamie umerejea na wewe ndiye mtu pekee katika maisha yangu niliekuchagua na kukulidhia bila shuruti uwe mpenzi wangu naamini Mungu alikuwa na maksudi nasisi lakini huenda nimeharibu, na ninaamini nimevuruga.
Natamani kuurudisha moyo wangu lakini kunakitanzi kimening’inizwa mbele yangu. Nitamueleza nini baba yangu na nitaipokeaje hali hii, mbaya zaidi nilikubali kwa hiali yangu sasa itakuwaje na nitawashawishi vipi wazazi wangu kuliahilisha zoezi hili.
Naamini siyo kitu kidogo hili ni tatizo kubwa na utatuzi wake unahitaji busara wala siyo nguvu. Niliamini ukitumia nguvu unaweza kuharibu kila kitu.” Nikweli alikuwa na kitanzi shingoni familia ya Rais ni familia mashuhuri mno, kuvunja uchumba ambao tayari wazazi wameshiriki kwa asilimia miamoja na mhusika alikubali itakuwa ni skendo kubwa kuwahi kutokea. Kwa unyonge niliamini hapa sina changu na nilikuwa mpole na kukubaliana na maelezo.
Ilikuwa ni siku ya Jumamosi nilifika ofisini kwangu majira ya saa mbili asubuhi mitaa ya Karuta Katikati ya jiji la Mwanza hapa ndipo yalikuwa makao makuu ya Himaya ChapaKazi niliegesha gari langu na nilipo ingia ndani mapokezi nilimkuta msichana mrembo kajiinamia nilimsogerea maana alikuwa peke yake.
Nilimgusa alipoinua uso alikuwa ni Jesca Manguli kwanza nilishituka maana ni kitu amabacho sikukitarajia kabisa. Nilimwinua na kumkumbatia kwa nguvu alikuwa akilia na nilipomkumbatia alilia kwa nguvu kiasi kwamba wafanyakazi wangu baadhi walitoka ofisini wakitaka kujua nini kinaendelea.
Kwa kifupi sikuona kama ni hali nzuri kuwepo pale nilijikaza nikamshika mkono, Jesca nikamuingiza kwenye gari sikutaka mazungumzo naye niliwasha gari na safari ilielekea nyumbani kwangu Isamilo ambako nimehamia hivi karibuni baada ya kununua nyumba karibu na kituo cha utafiti wa magonjwa ya mifugo na binadamu. Nilimkaribisha ndani ya jengo langu la kifahali nilililinunua toka kwa mmiliki wake wa awali shirika la Care international na ilikuwa ni nyumba ya mkurugenzi wa shirika hili nchini Tanzania ambaye alihamisha makazi yake hapa jijini.