Zembwela wa Wasafi FM aitaka Serikali iruhusu Uvutaji wa Bangi kwa Wanaohitaji huku akiisifia mno

Zembwela wa Wasafi FM aitaka Serikali iruhusu Uvutaji wa Bangi kwa Wanaohitaji huku akiisifia mno

Siku hizi Wadai haki za Kizandiki wanaongezeka kila uchwao , Mtu kujitokeza na kuhamasisha watu watumie dawa za Kulevya huwezi kumtofautisha na hawa wadai haki za Kishoga
Sahihi mkuu. Huwa mambo yanaanza hivi hivi taratibu kimasiara baadae yanakua kwa kasi na kupata wafuasi wa kuyapambania yahalalishwe.
 
Mkuu GENTAMYCINE si unajua huyo jamaa ni comedian? Huenda alikuwa anachekesha tu watanzania turuhusiwe kuvuta bangi. Kwa kuwa tunajua madhara ya bangi wengine hatutavuta bangi hata kama ikiruhusiwa kama ilivyo tumbaku
 
"Nchi nyingi Siku hizi tena zilizoendelea kama ninayosafiri sana ya Netherlands na nyinginezo zinaruhusu Uvutaji wa Bangi kwa Raia wake wanapotaka sioni sababu ya Tanzania kuzuia wakati Bangi nayo ni Burudani na ina Starehe yake" amesema Mtangazaji wa Wasafi FM Zembwela (Hillary Daud) akiwa Nyumbani kwa Spika wa Bunge na Watangazaji Wenzake ambako kwa Asubuhi ya Leo wanafanyia Kipindi hapo.

Kwa GENTAMYCINE ninayemjua ndani nje Zembwela tokea akiwa Comedian na Rafiki yake Marehemu Max, alipokuwa East Africa Radio na East Africa Tv na Mitaani Sinza, Tandale, Mwenge na Magomeni na nini hasa anachokitumia ndiyo maana Macho yake 24/7 huwa ni Mekundu na Mdomo wake una Uweusi mwingi ngoja ninyamaze na niishie hapa tu.tafadhali.

TCRA Kazi Kwenu na Zembwela alivyo wa hovyo hovyo baada ya Awali katika Maelezo yake kutaka Watanzania tuvute Bangi muda si mrefu Kiunafiki kabisa ametengua hiyo Kauli na Kuzuga kwa kusema Tanzania hairuhusu Uvutaji wa Bangi.

Tafadhali achukuliwe hatua haraka pamoja na hiyo Redio ( Wasafi FM ) kwani kwa Kauli yake tu ya Awali kututaka Watanzania tuvute Bangi na Kuiomba Serikali iruhusu Uvutaji huo wa Bangi tena Hewani ( On Air ) imeleta Usumbufu na inaweza kupokelewa vibaya na tusiovuta Bangi hiyo akina GENTAMYCINE tukashawishika kuanza Kuivuta na Kulanduka nayo vilevile.
Yani mru kutoa maoni yake tu ndiyo iwe nongwa mpaka unataka TCRA wamchukulie hatua? Sasa Uhuru wa maoni upo wapi?

Kwa zembwela ninayemjua mimi endapo mwandika uzi angekuwa anakufahamu kwa jinsi ulivyoandika ukuda na kumkanyagia hivi,leo ungeumuka mwili Kama mkate maana angekupiga kata funua nyingi sana.
 
Sahihi mkuu. Huwa mambo yanaanza hivi hivi taratibu kimasiara baadae yanakua kwa kasi na kupata wafuasi wa kuyapambania yahalalishwe.

Wasafi inabidi wapigwe ban haraka sana kwa kukiuka taratibu na kutoa Maudhui yasiyofaa kwa public, huku ni kudhorotesha juhudi zinazofanywa na Serikali
 
Nakumbuka mwaka 2002 pale diamond jubilee kulikuwa na tamasha pale la wasanii kipindi hicho akina jumla nature wapo jukwaaani wanatumbuiza huyu zembwela na wahuni wenzake walikuwa wanavuta bangi chooni na wengine wanasaga unga, zamani uvutaji bangi mbele za watu ilikuwa fashion
 
Turuhusu wawekezaji waje kusindika bangi na kuuza. Tutoe elimu namna ya kulima bangi ambayo tunaweza uza ata kimataifa.

Bangi oye, zembwela oye, Tulia oye
 
Yani mru kutoa maoni yake tu ndiyo iwe nongwa mpaka unataka TCRA wamchukulie hatua? Sasa Uhuru wa maoni upo wapi?

Kwa zembwela ninayemjua mimi endapo mwandika uzi angekuwa anakufahamu kwa jinsi ulivyoandika ukuda na kumkanyagia hivi,leo ungeumuka mwili Kama mkate maana angekupiga kata funua nyingi sana.
Tena usinitibue kabisa nikayaanika yake mengineyo hapa na mkamdharau mazima.
 
Kuhamasisha uvutaji wa bangi hakuna tofauti kubwa na kuhamasisha ushoga, wasiotumia bangi watakasirika lakini wanaoivuta kama hayati Bob Marley hutawaambia kitu. Wanaoiona bangi nzuri ni wale wanaoivuta na haijawahi kuwaletea madhara yeyote kiafya. Hivi umewahi kushuhudia vijana waliopatwa na maradhi ya akili kisa kuvuta bangi?, unaweza kukisia takwimu za wale waliochanganyikia akii shauri ya kuvuta bangi? Sasa elewa tu kwamba wale waliokaa na kuharamisha bangi siyo vichaa na walielewa fika madhara ya mmea huu.

Ubongo wa kila mwanadamu ni tofauti na hatulingani katika viwango vya kuhimili madhara yatokanayo na kemikali au dawa mbalimbali. Kuna watu huvuta sigara mpaka miaka hata 100 na hawapatwi na kansa kabisa lakini wapo watu wengi tu hata kuwa karibu na mvuta sigara kwa muda mrefu unasikia tayari kapatwa na kansa. Sasa akili ya kuambiwa changanya na yakwako usiwe juha kufuata kila anachosema au kufanya mtu maarufu hata ikiwa ni Bob marley au Zembwela, huwezi jua ubongo wako ni dhaifu kiasi gani wewe kabugie mimoshi ya bange, utakapokuwa ukihangaika Muhimbili au Mwananyamala ni shauri lako. Nina ushahidi Bangi ni moja kati ya vitu vinavyochangia kutibuka kwa magonjwa ya akili. Hakuna binadamu asiyekuwa kichaa ila kichaa halisi huja baada mtu kupalilia vichokoo vyake.
 
Acheni upopoma.. bangi iruhusiwe. Marais karibia wote wa marekani, tukianzia Clinton, Bush junior, Obama na mkewe, hata Rais mpendwa mno wa marekani John Kennedy, walikuwa wavutaji wazuri wa bangi. Nyinyi ni nani mapopoma mpaka muipinge bangi?

Screenshot_20230504-115935_1.jpg
 
"Nchi nyingi Siku hizi tena zilizoendelea kama ninayosafiri sana ya Netherlands na nyinginezo zinaruhusu Uvutaji wa Bangi kwa Raia wake wanapotaka sioni sababu ya Tanzania kuzuia wakati Bangi nayo ni Burudani na ina Starehe yake" amesema Mtangazaji wa Wasafi FM Zembwela (Hillary Daud) akiwa Nyumbani kwa Spika wa Bunge na Watangazaji Wenzake ambako kwa Asubuhi ya Leo wanafanyia Kipindi hapo.

Kwa GENTAMYCINE ninayemjua ndani nje Zembwela tokea akiwa Comedian na Rafiki yake Marehemu Max, alipokuwa East Africa Radio na East Africa Tv na Mitaani Sinza, Tandale, Mwenge na Magomeni na nini hasa anachokitumia ndiyo maana Macho yake 24/7 huwa ni Mekundu na Mdomo wake una Uweusi mwingi ngoja ninyamaze na niishie hapa tu.tafadhali.

TCRA Kazi Kwenu na Zembwela alivyo wa hovyo hovyo baada ya Awali katika Maelezo yake kutaka Watanzania tuvute Bangi muda si mrefu Kiunafiki kabisa ametengua hiyo Kauli na Kuzuga kwa kusema Tanzania hairuhusu Uvutaji wa Bangi.

Tafadhali achukuliwe hatua haraka pamoja na hiyo Redio ( Wasafi FM ) kwani kwa Kauli yake tu ya Awali kututaka Watanzania tuvute Bangi na Kuiomba Serikali iruhusu Uvutaji huo wa Bangi tena Hewani ( On Air ) imeleta Usumbufu na inaweza kupokelewa vibaya na tusiovuta Bangi hiyo akina GENTAMYCINE tukashawishika kuanza Kuivuta na Kulanduka nayo vilevile.
Shida ya hawa watu wasio na taaluma ya utangazaji ni kubwa
 
Back
Top Bottom